Rais Samia, usiwasikilize wanasiasa uchwara wanaoshabikia ukabila, uonezi na upendeleo ulioasisiwa na mtangulizi wako

masopakyindi

Platinum Member
Jul 5, 2011
17,882
13,171
Kujenga umoja wa kitaifa ni kazi ngumu kuliko kujenga mabarabara marefu nchini.

Umoja huu wa kitaifa umejengwa mwa miaka mingi na kwa gharama kubwa kutoka Awamu ya kwanza na zilizofuatiwa.

Kuna ambao shula za kidini zilitaifishwa, hospitali zikafanya za umma, ubaguzi wa kidini, kieneo hata kikabila vilionekana ni anti progressive.

Mwalimu alifanikiwa katika hili.

Hata hivyo lets call a spade a spade, Awamu ya tano haikufanya vizuri katika kuendeleza umoja huo.

Upendeleo wa wazi wa kikabila uliwekwa mbele.

Maendeleo kiujumla yalipelekwa kule tunakokujua sasa kama kanda ya ziwa.

Kuna wananchi walinyimwahuduma kutokana na imani zao kwa vyama na hili lilisemwa wazi.

Kuponya vidonda hivi vya ubaguzi haichukui siku moja au mwaka mmoja.

Lakini tukubali kuwa Mama Samia kaanza vizuri katika kurekebisha hali hiyo kisiasa kwa matamshi yake ya awali.

Kinachotia shaka ni viongozi wale wale waliokuwa mstari wa mbele katika kubagua na kuonea, hawa siyo siri inabidi waondolewe ili kurudisha imani ya wananchi.

Waswahili wa pwani husema, akumilikaye mchana, usiku hukuchoma.

Mama Samia, hao usiwaonee haya.
 
Kusema ukweli Hayati anapewa tuhuma za upendeleo zisizo za kweli. Nimeshuhudia maendeleo yakipelekwa nchi nzima angalia.Miradi ya Dodoma eg mabarabara, uwanja wa ndege kimataifa unakuja,uwanja ua mpira wa kimatifa, Dar es Salaam ona flyovers zinazojengwa, stand kuu, mabarabara SGR imeanzia Dar, Dar la Tanzanite nk Arusha barabara njia nne, mradi mkubwa wa maji.

Pwani tumeshuhudia mradi mkubwa wa Hydro Power Rufiji, Iringa uwanja ndege, daraja la Wami etc. Kigoma barabara na meli zinatengenezwa.Hivyo kiukweli ni uzandiki kumlaumu marehemu wakati miradi yote inatokana na ilani ya uchaguzi.

Isome ilani ndiyo utaujua ukweli. Mwanza imekaa miaka mingi bila uwanja wa ndege wa kimataifa na unaojengwa haulingani na hadhi ya jiji.

Barabara za kuingia jijini ni mashimo na ni njia moja. Tuwe wakweli tusweke hisia jaribu kuongea na Wabunge wa Majimbo watakueleza maajabu yaliyofanyika kwa kila mkoa. Rais anayo picha yote ya utekelezaji wa ilani ya uchaguzi.
 
Kusema ukweli Hayati anapewa tuhuma za upendeleo zisizo za kweli. Nimeshuhudia maendeleo yakipelekwa nchi nzima angalia. Miradi ya Dodoma eg mabarabara.
Magufuli alikuwa akiongea kwa mdomo wake kuwa kuna sehemu hatapeleka maendeleo kwa vile wametofautiana.

Kuna mikoa maendeleo yalipelekwa kwa shingo upande au hakuna kabisa.

Huku Mbeya barabara ya kuingia mjini ni mbovu na ya kutisha.

Kelekea Mbalizi gari zinapita moja moja.

Ndiyo barabara kuu kuelekea Zambia na Congo hii.

Barabara za Wilayani ndiyo hakuna kwa miongo.

Mwisho unajihisi kuwa lazima kuna kitu.

Si bure!
 
Magufuli alikuwa akiongea kwa mdomo wake kuwa kuna sehemu hatapeleka maendeleo kwa vile wametofautiana.

Kuna mikoa maendeleo yalipelekwa kwa shingo upande au hakuna kabisa.
Huu ndio ukweli na alisemea ktk majukwaa bila aibu wala soni na alifanya hivyo!
Tuombe Mungu tusipate utawala wa aina ile tena Tanzania.
 
Huu ndio ukweli na alisemea ktk majukwaa bila aibu wala soni na alifanya hivyo!
Tuombe Mungu tusipate utawala wa aina ile tena Tanzania.
Kuna watu wanajaribu kufunika udhaifu huu wa ubaguzi na upendeleo uliofanywa na Magufuli kiwazi wazi kabisa.
 
Back
Top Bottom