Yericko Nyerere
JF-Expert Member
- Dec 22, 2010
- 16,987
- 20,271
Mh Rais, Kwasiku 100 ulizoongoza nchi zimekuwa za kutukuka sana, Taifa limepumua na kuonyesha mageuzi makubwa sana, Kwahakika nakupongeza sana sana, Umewathibitishia wazi unaweza kwa wale waliodhani huwezi kuongoza nchi.
Jambo la msingi leo naomba kuzungumzia kikao chako cha jana, ambapo nimesikiliza mazungumzo yako na Wahariri vya Vyombo vya habari nchini ambayo ni mazuri sana,
Pamoja na uzuri huo, Majibu yako kuhusu shughuli za kisiasa na mchakato wa Katiba Mpya yamenitia hofu huko tuendako kama kweli tutatibu tatizo la nchi ama tunafunika kombe la utawala uliopita.
Kimsingi jana tulitaraji utengue AMRI YA KIRAIS iliyotolewa na utawala uliopita kuhusu kusitisha shughuli za kisiasa (za wapinzani). Lakini pia tulitaraji utupe mwelekeo wa lini mchakato wa katiba mpya utaanza, Japo la Katiba ulilijibu lakini jibu lake limekuwa lilelile alilotwambia Rais Magufuli wakati anaingia madarakani.
Suala la shughuli za kisiasa ni la kikatiba na kisheria sio la hisani ya Rais, Nimelazimika kwenda kusoma sheria ya vyama vya siasa iliyofanyiwa marejeo 2019, kifungu cha 11, haki ya chama cha siasa kufanya mikutano ipo sio hisani ya mtu yoyote bali ni utekelezaji wa sheria tu.
Sasa rais wangu UMEAPA KUILINDA KATIBA NA SHERIA ZAKE, Ninakuomba sana, liangalie hili kwa umakini, huenda kuna wasaidizi wanakupotosha kuwa shughuli za vyama vya siasa zinakwamisha maendeleo, Hao wanakugombanisha na umma.
Watanzania sisi ukitaka tusikusumbue tuache tuongee, tulie na kucheka, tutanyamaza wenyewe, lakini sio utulazimishe tuongee, utulazimishe tulie wala utulazimishe kunyamaza. Kwahakika tutakusumbua kwelikweli, si jela wala mahakama havitatutibu. Shahidi utawala uliopita.
Labla nirejee nyuma kidogo, Msingi wa mpasuko wa taifa hili hadi kufika kuvuruga uchumi na mengineyo, ulitokana mwanzo kabisa kuzuia haki za watu kukutana na kutoa mawazo yao ambayo ni haki ya kikatiba na kisheria, Waliozuia walikuja na hoja hiyohiyo ambayo leo Rais umesema kuwa unanyoosha nchi.
Rais Mstaafu Jakaya Kikwete alipoanzisha mchakato wa Katiba nchi ilikuwa hivihivi wala hakuwa na kigezo cha nchi imenyooka au imepinda, na alipoahirisha nchi ilibaki vilevile, Mchakato wa Katiba mpya hauwezi kuzua miradi ya maendeleo nchini wala hauwezi kukuzuia Mh Rais kuendesha nchi. Vivyo hivyo shughuli za kisiasa.
Katiba mpya ndio msingi wa mambo yote katika nchi, Tukipata katiba mpya itaondoa kazi ya kunyoosha uchumi wa nchi unayoifanya leo Mh Rais kwakuwa hakuna atakayekuja kuipindisha nchi tena.
Na Yericko Nyerere
Jambo la msingi leo naomba kuzungumzia kikao chako cha jana, ambapo nimesikiliza mazungumzo yako na Wahariri vya Vyombo vya habari nchini ambayo ni mazuri sana,
Pamoja na uzuri huo, Majibu yako kuhusu shughuli za kisiasa na mchakato wa Katiba Mpya yamenitia hofu huko tuendako kama kweli tutatibu tatizo la nchi ama tunafunika kombe la utawala uliopita.
Kimsingi jana tulitaraji utengue AMRI YA KIRAIS iliyotolewa na utawala uliopita kuhusu kusitisha shughuli za kisiasa (za wapinzani). Lakini pia tulitaraji utupe mwelekeo wa lini mchakato wa katiba mpya utaanza, Japo la Katiba ulilijibu lakini jibu lake limekuwa lilelile alilotwambia Rais Magufuli wakati anaingia madarakani.
Suala la shughuli za kisiasa ni la kikatiba na kisheria sio la hisani ya Rais, Nimelazimika kwenda kusoma sheria ya vyama vya siasa iliyofanyiwa marejeo 2019, kifungu cha 11, haki ya chama cha siasa kufanya mikutano ipo sio hisani ya mtu yoyote bali ni utekelezaji wa sheria tu.
Sasa rais wangu UMEAPA KUILINDA KATIBA NA SHERIA ZAKE, Ninakuomba sana, liangalie hili kwa umakini, huenda kuna wasaidizi wanakupotosha kuwa shughuli za vyama vya siasa zinakwamisha maendeleo, Hao wanakugombanisha na umma.
Watanzania sisi ukitaka tusikusumbue tuache tuongee, tulie na kucheka, tutanyamaza wenyewe, lakini sio utulazimishe tuongee, utulazimishe tulie wala utulazimishe kunyamaza. Kwahakika tutakusumbua kwelikweli, si jela wala mahakama havitatutibu. Shahidi utawala uliopita.
Labla nirejee nyuma kidogo, Msingi wa mpasuko wa taifa hili hadi kufika kuvuruga uchumi na mengineyo, ulitokana mwanzo kabisa kuzuia haki za watu kukutana na kutoa mawazo yao ambayo ni haki ya kikatiba na kisheria, Waliozuia walikuja na hoja hiyohiyo ambayo leo Rais umesema kuwa unanyoosha nchi.
Rais Mstaafu Jakaya Kikwete alipoanzisha mchakato wa Katiba nchi ilikuwa hivihivi wala hakuwa na kigezo cha nchi imenyooka au imepinda, na alipoahirisha nchi ilibaki vilevile, Mchakato wa Katiba mpya hauwezi kuzua miradi ya maendeleo nchini wala hauwezi kukuzuia Mh Rais kuendesha nchi. Vivyo hivyo shughuli za kisiasa.
Katiba mpya ndio msingi wa mambo yote katika nchi, Tukipata katiba mpya itaondoa kazi ya kunyoosha uchumi wa nchi unayoifanya leo Mh Rais kwakuwa hakuna atakayekuja kuipindisha nchi tena.
Na Yericko Nyerere