Rais Samia upole ukizidi watataka wakae juu ya mabega yako, kuwa mkali kidogo.

Phillipo Bukililo

JF-Expert Member
Dec 29, 2015
18,488
13,608
Urais wa Samia Suluhu Hassan umeanza na upole. Umeanza na uungwana wa kuwa tayari kupoteza baadhi ya marafiki ili mradi tu taswira yake kimataifa iweze kubakia na heshima. Akaenda Ubelgiji akaonana na Tundu Lissu wakati ambao wapo wana CCM wengi tu wasingependa kumuona akijishusha (kwa mujibu wa fikra zao) namna ile.

Akamfungulia Mbowe na kumualika ikulu kufanya nae mazungumzo. Baada ya kukisia kilio cha muda mrefu cha maaskofu na wanaharakati wenye kutoa maoni yao kwa vyombo vya habari. Ameonyesha uwezo wa kujishusha na kufanya mijadala ya kimaongezi. Amejitahidi kuliishi jina lake 'suluhu' kwa vitendo.

Lakini anao maadui kwani huwezi kuongoza nchi ukakubalika kwa kila raia unayemuongoza, haijawi kutokea hali ya aina hiyo mahali popote haswa kwenye nchi zilizo katika michakato ya ukuzaji wa demokrasia ya kivitendo kama Tanzania. Binafsi nimemuelewa sana Rais Samia.

Wapo wale wenye mawazo ambayo kwa kingereza wanaitwa ni conservative. Wapo wale wenye hulka kwamba Mwanamke hana hadhi ya kuwaongoza wanaume, wapo wale waliomkubali mno hayati JPM na kile alichokuwa akikihubiri majukwaani na kukiishi kila siku. Wapo wale ambao ni 'waafrika' kweli kweli wenye mawazo yale yale ya mzungu kuvalishwa mtumba baada ya mwafrika kutengeneza nguo akaivaa na kisha akaisafirisha kuipelekea Ulaya.

Hawa wanaona siku zote kuwa viatu vya hayati JPM ni vikubwa mno kwa Samia kuweza kuvivaa na vikamtosha, tatizo lao lipo akilini zaidi. Ndani ya ufikiriaji mzima (mindset) walionao. Ni ngumu kuweza kuwabadilisha kile wanachofikiria. Hawakuweza kuijua mipango ya Mungu walidhani maadam JPM alishaapa na kuingia ikulu basi angeendelea mpaka 2025. Kipindi kile cha msiba, hawa ni miongoni mwa waliolia hadharani na kwa uchungu mkubwa.

Ni kama wana hasira fulani japokuwa wakiulizwa wanakana kwamba hawana kinyongo au ghadhabu inayowasumbua. Hawa ni maadui wanaokua katika suala zima la mbinu za kuupinga uongozi wa awamu ya sita. Walimpenda JPM lakini wanashindwa kuelewa ni kwamba Samia alikuwa msaidizi muhimu wa JPM. Wanamnyanyapaa kwa sasa wakiwa mbali ya kamera lakini enzi za uhai wa JPM walifanya hivi hadharani kabisa, hawakuijua mipango ya Muumba ni ipi.

Ninapenda kumkumbusha Rais SSH kwamba upole wa awamu yake unaweza huko mbeleni kuleta ugumu wa kuelezea haya anayoyafanya kwa sasa, kama yameyagusa maisha ya mtu mmoja mmoja. Kwa maana kwamba hawa wanaojichekesha mbele ya macho yake wanaitumia mitandao kwa mapana ili aonekane hana anachokifanya.

Hawa jamaa wa JPM wamegeuka kuwa ni mabingwa wa utengenezaji wa hizi fake news zinazozagaa mitandaoni. Tatizo ni kwamba habari inaweza kuwafikia watanzania 10000 na kati yao watakaoamini ni 9500 na pakawepo watu makini 500 wenye kuweza kuielewa hiyo propaganda kwa kina.

Lakini tayari wapo wale 9500 waliokwisha kuaminishwa na kile kinachokuwemo katika habari ya kubuni isiyo na ukweli wowote. Ikiwekwa mtandaoni habari nyingine itasomwa na watu milioni moja. Kati ya hao watakaoiamini wanaweza kuwa ni laki tisa na ile laki moja ikaweza kuitilia mashaka. Wale laki tisa ni wengi kiasi cha kuamini uzushi kuwa ni habari ya ukweli.

Rais SSH aitumie nafasi hii kulishughulikia hili tatizo kabla halijawa sugu na kukwamisha ufanisi wa kile anachokifanya ambacho kwa kiasi kikubwa na umaliziaji wa miradi iliyoachwa na hayati JPM. Akiwa hai JPM aliweza kuishughulikia mitandao inayosambaza fake news na akaogopwa kwani msimamo wake ulieleweka kwa kila mtu.

Rais SSH kwa upole na uungwana wake ataivumilia hii hali lakini itakwenda ikiharibu kile anachotaka kukifanya. Wanaopotoshwa na fake news ni wengi, na uwezo wetu wa kupima ukweli na mantiki ya kile kinachoandikwa na kusambazwa mtandaoni siku zote unatofautiana.

Wanaopaka matope ufanisi wa serikali hufanya hivyo kwa kivuli cha demokrasia hata kama wanawafanyia kazi watu wenye nia ovu dhidi ya serikali na mipango yake. Ni hali ya kuishughulikia kwa kutumia busara na umakini wa hali ya juu.
 
Kwa maoni yako inaonyesha kwamba unakubali JPM alikuwa sahihi katika kuishughulikia mitandao ya kijamii ??! Kwahiyo freedom of expression haikubaliki !! Turudi kulekuleee !!! Salaaaleeh !!! Mbona tena kwenye maelezo yako imeonyesha unawapiga za USO Hao walio upande wa JPM ??! Wanasemaga Baniani mbaya kiatu chake ni dawa !! JPM amekuwa akishambuliwa humu kwa maneno makali kwa kuwabana watu kutoa mawazo yao Leo tena ibadilike ionekane kumbe alikuwa sahihi !! Bandugu mnatuchanganya !!!
Urais wa Samia Suluhu Hassan umeanza na upole. Umeanza na uungwana wa kuwa tayari kupoteza baadhi ya marafiki ili mradi tu taswira yake kimataifa iweze kubakia na heshima. Akaenda Ubelgiji akaonana na Tundu Lissu wakati ambao wapo wana CCM wengi tu wasingependa kumuona akijishusha (kwa mujibu wa fikra zao) namna ile.

Akamfungulia Mbowe na kumualika ikulu kufanya nae mazungumzo. Baada ya kukisia kilio cha muda mrefu cha maaskofu na wanaharakati wenye kutoa maoni yao kwa vyombo vya habari. Ameonyesha uwezo wa kujishusha na kufanya mijadala ya kimaongezi. Amejitahidi kuliishi jina lake 'suluhu' kwa vitendo.

Lakini anao maadui kwani huwezi kuongoza nchi ukakubalika kwa kila raia unayemuongoza, haijawi kutokea hali ya aina hiyo mahali popote haswa kwenye nchi zilizo katika michakato ya ukuzaji wa demokrasia ya kivitendo kama Tanzania. Binafsi nimemuelewa sana Rais Samia.

Wapo wale wenye mawazo ambayo kwa kingereza wanaitwa ni conservative. Wapo wale wenye hulka kwamba Mwanamke hana hadhi ya kuwaongoza wanaume, wapo wale waliomkubali mno hayati JPM na kile alichokuwa akikihubiri majukwaani na kukiishi kila siku. Wapo wale ambao ni 'waafrika' kweli kweli wenye mawazo yale yale ya mzungu kuvalishwa mtumba baada ya mwafrika kutengeneza nguo akaivaa na kisha akaisafirisha kuipelekea Ulaya.

Hawa wanaona siku zote kuwa viatu vya hayati JPM ni vikubwa mno kwa Samia kuweza kuvivaa na vikamtosha, tatizo lao lipo akilini zaidi. Ndani ya ufikiriaji mzima (mindset) walionao. Ni ngumu kuweza kuwabadilisha kile wanachofikiria. Hawakuweza kuijua mipango ya Mungu walidhani maadam JPM alishaapa na kuingia ikulu basi angeendelea mpaka 2025. Kipindi kile cha msiba, hawa ni miongoni mwa waliolia hadharani na kwa uchungu mkubwa.

Ni kama wana hasira fulani japokuwa wakiulizwa wanakana kwamba hawana kinyongo au ghadhabu inayowasumbua. Hawa ni maadui wanaokua katika suala zima la mbinu za kuupinga uongozi wa awamu ya sita. Walimpenda JPM lakini wanashindwa kuelewa ni kwamba Samia alikuwa msaidizi muhimu wa JPM. Wanamnyanyapaa kwa sasa wakiwa mbali ya kamera lakini enzi za uhai wa JPM walifanya hivi hadharani kabisa, hawakuijua mipango ya Muumba ni ipi.

Ninapenda kumkumbusha Rais SSH kwamba upole wa awamu yake unaweza huko mbeleni kuleta ugumu wa kuelezea haya anayoyafanya kwa sasa, kama yameyagusa maisha ya mtu mmoja mmoja. Kwa maana kwamba hawa wanaojichekesha mbele ya macho yake wanaitumia mitandao kwa mapana ili aonekane hana anachokifanya.

Hawa jamaa wa JPM wamegeuka kuwa ni mabingwa wa utengenezaji wa hizi fake news zinazozagaa mitandaoni. Tatizo ni kwamba habari inaweza kuwafikia watanzania 10000 na kati yao watakaoamini ni 9500 na pakawepo watu makini 500 wenye kuweza kuielewa hiyo propaganda kwa kina.

Lakini tayari wapo wale 9500 waliokwisha kuaminishwa na kile kinachokuwemo katika habari ya kubuni isiyo na ukweli wowote. Ikiwekwa mtandaoni habari nyingine itasomwa na watu milioni moja. Kati ya hao watakaoiamini wanaweza kuwa ni laki tisa na ile laki moja ikaweza kuitilia mashaka. Wale laki tisa ni wengi kiasi cha kuamini uzushi kuwa ni habari ya ukweli.

Rais SSH aitumie nafasi hii kulishughulikia hili tatizo kabla halijawa sugu na kukwamisha ufanisi wa kile anachokifanya ambacho kwa kiasi kikubwa na umaliziaji wa miradi iliyoachwa na hayati JPM. Akiwa hai JPM aliweza kuishughulikia mitandao inayosambaza fake news na akaogopwa kwani msimamo wake ulieleweka kwa kila mtu.

Rais SSH kwa upole na uungwana wake ataivumilia hii hali lakini itakwenda ikiharibu kile anachotaka kukifanya. Wanaopotoshwa na fake news ni wengi, na uwezo wetu wa kupima ukweli na mantiki ya kile kinachoandikwa na kusambazwa mtandaoni siku zote unatofautiana.

Wanaopaka matope ufanisi wa serikali hufanya hivyo kwa kivuli cha demokrasia hata kama wanawafanyia kazi watu wenye nia ovu dhidi ya serikali na mipango yake. Ni hali ya kuishughulikia kwa kutumia busara na umakini wa hali ya juu.
 
Kwa maoni yako inaonyesha kwamba unakubali JPM alikuwa sahihi katika kuishughulikia mitandao ya kijamii ??! Kwahiyo freedom of expression haikubaliki !! Turudi kulekuleee !!! Salaaaleeh !!! Mbona tena kwenye maelezo yako imeonyesha unawapiga za USO Hao walio upande wa JPM ??! Wanasemaga Baniani mbaya kiatu chake ni dawa !! JPM amekuwa akishambuliwa humu kwa maneno makali kwa kuwabana watu kutoa mawazo yao Leo tena ibadilike ionekane kumbe alikuwa sahihi !! Bandugu mnatuchanganya !!!
Mitandao inao uwezo wa kuuremba uongo ukaonekana ni ukweli. Kwa hilo JPM hakumumunya maneno alikuwa muwazi kupinga jitihada zote za kufanya alichofanya kikaonekana ni kama upotezaji wa muda.
 
Ukikubali upande mmoja wa shilingi maana yake ni lazima ukubali na upande wake wa pili ! Hiyo ndio gharama ya freedom of expression, ukizuia utaitwa DIKTETA !! chagua kusuka au kunyoa !!!
Mitandao inao uwezo wa kuuremba uongo ukaonekana ni ukweli. Kwa hilo JPM hakumumunya maneno alikuwa muwazi kupinga jitihada zote za kufanya alichofanya kikaonekana ni kama upotezaji wa muda.
 
Rais samia sio mpole kama Kikwete au Mwinyi

Huyu Ligi anaziweza na ameziishi…ila ukijishusha kinafki mambo yako yatakunyookea sana

Kwa waliowahi kufanya kazi chini ya Maboss lady watakuwa wamenielewa
 
Mitandao inao uwezo wa kuuremba uongo ukaonekana ni ukweli. Kwa hilo JPM hakumumunya maneno alikuwa muwazi kupinga jitihada zote za kufanya alichofanya kikaonekana ni kama upotezaji wa muda.
Mkuu unasema Magufuli alifanikiwa kuzuia fake news?
Pengine kipindi cha Magufuli ndio fake news zilishamiri na watu wakawa wanaziamini zaidi kuliko kipindi cha Samia
Alikuwa akikamata watu lakini haikufua dafu, kule Twitter kulikuwa na utitiri wa akaunti zilizokuwa zikisambaza uwongo kipindi cha JPM na ndio hadi Kigogo akapata umaarufu sana

Youtube alijaribu kuidhibiti lakini wapi, account zisizosajiliwa zilikuwepo na kupost tu habari fake

Samia aje na mkakati wake tu, ila kuiga ya JPM ataonekana vibaya zaidi,
 
Urais wa Samia Suluhu Hassan umeanza na upole. Umeanza na uungwana wa kuwa tayari kupoteza baadhi ya marafiki ili mradi tu taswira yake kimataifa iweze kubakia na heshima. Akaenda Ubelgiji akaonana na Tundu Lissu wakati ambao wapo wana CCM wengi tu wasingependa kumuona akijishusha (kwa mujibu wa fikra zao) namna ile.

Akamfungulia Mbowe na kumualika ikulu kufanya nae mazungumzo. Baada ya kukisia kilio cha muda mrefu cha maaskofu na wanaharakati wenye kutoa maoni yao kwa vyombo vya habari. Ameonyesha uwezo wa kujishusha na kufanya mijadala ya kimaongezi. Amejitahidi kuliishi jina lake 'suluhu' kwa vitendo.

Lakini anao maadui kwani huwezi kuongoza nchi ukakubalika kwa kila raia unayemuongoza, haijawi kutokea hali ya aina hiyo mahali popote haswa kwenye nchi zilizo katika michakato ya ukuzaji wa demokrasia ya kivitendo kama Tanzania. Binafsi nimemuelewa sana Rais Samia.

Wapo wale wenye mawazo ambayo kwa kingereza wanaitwa ni conservative. Wapo wale wenye hulka kwamba Mwanamke hana hadhi ya kuwaongoza wanaume, wapo wale waliomkubali mno hayati JPM na kile alichokuwa akikihubiri majukwaani na kukiishi kila siku. Wapo wale ambao ni 'waafrika' kweli kweli wenye mawazo yale yale ya mzungu kuvalishwa mtumba baada ya mwafrika kutengeneza nguo akaivaa na kisha akaisafirisha kuipelekea Ulaya.

Hawa wanaona siku zote kuwa viatu vya hayati JPM ni vikubwa mno kwa Samia kuweza kuvivaa na vikamtosha, tatizo lao lipo akilini zaidi. Ndani ya ufikiriaji mzima (mindset) walionao. Ni ngumu kuweza kuwabadilisha kile wanachofikiria. Hawakuweza kuijua mipango ya Mungu walidhani maadam JPM alishaapa na kuingia ikulu basi angeendelea mpaka 2025. Kipindi kile cha msiba, hawa ni miongoni mwa waliolia hadharani na kwa uchungu mkubwa.

Ni kama wana hasira fulani japokuwa wakiulizwa wanakana kwamba hawana kinyongo au ghadhabu inayowasumbua. Hawa ni maadui wanaokua katika suala zima la mbinu za kuupinga uongozi wa awamu ya sita. Walimpenda JPM lakini wanashindwa kuelewa ni kwamba Samia alikuwa msaidizi muhimu wa JPM. Wanamnyanyapaa kwa sasa wakiwa mbali ya kamera lakini enzi za uhai wa JPM walifanya hivi hadharani kabisa, hawakuijua mipango ya Muumba ni ipi.

Ninapenda kumkumbusha Rais SSH kwamba upole wa awamu yake unaweza huko mbeleni kuleta ugumu wa kuelezea haya anayoyafanya kwa sasa, kama yameyagusa maisha ya mtu mmoja mmoja. Kwa maana kwamba hawa wanaojichekesha mbele ya macho yake wanaitumia mitandao kwa mapana ili aonekane hana anachokifanya.

Hawa jamaa wa JPM wamegeuka kuwa ni mabingwa wa utengenezaji wa hizi fake news zinazozagaa mitandaoni. Tatizo ni kwamba habari inaweza kuwafikia watanzania 10000 na kati yao watakaoamini ni 9500 na pakawepo watu makini 500 wenye kuweza kuielewa hiyo propaganda kwa kina.

Lakini tayari wapo wale 9500 waliokwisha kuaminishwa na kile kinachokuwemo katika habari ya kubuni isiyo na ukweli wowote. Ikiwekwa mtandaoni habari nyingine itasomwa na watu milioni moja. Kati ya hao watakaoiamini wanaweza kuwa ni laki tisa na ile laki moja ikaweza kuitilia mashaka. Wale laki tisa ni wengi kiasi cha kuamini uzushi kuwa ni habari ya ukweli.

Rais SSH aitumie nafasi hii kulishughulikia hili tatizo kabla halijawa sugu na kukwamisha ufanisi wa kile anachokifanya ambacho kwa kiasi kikubwa na umaliziaji wa miradi iliyoachwa na hayati JPM. Akiwa hai JPM aliweza kuishughulikia mitandao inayosambaza fake news na akaogopwa kwani msimamo wake ulieleweka kwa kila mtu.

Rais SSH kwa upole na uungwana wake ataivumilia hii hali lakini itakwenda ikiharibu kile anachotaka kukifanya. Wanaopotoshwa na fake news ni wengi, na uwezo wetu wa kupima ukweli na mantiki ya kile kinachoandikwa na kusambazwa mtandaoni siku zote unatofautiana.

Wanaopaka matope ufanisi wa serikali hufanya hivyo kwa kivuli cha demokrasia hata kama wanawafanyia kazi watu wenye nia ovu dhidi ya serikali na mipango yake. Ni hali ya kuishughulikia kwa kutumia busara na umakini wa hali ya juu.
Eti unasema SAMIA anaupole umemuuliza Ndugai wewe au Umemuuliza Chalamaila wewe? Nenda kamuulize SABAYA upole wa Samia ndugu yang.
 
Urais wa Samia Suluhu Hassan umeanza na upole. Umeanza na uungwana wa kuwa tayari kupoteza baadhi ya marafiki ili mradi tu taswira yake kimataifa iweze kubakia na heshima. Akaenda Ubelgiji akaonana na Tundu Lissu wakati ambao wapo wana CCM wengi tu wasingependa kumuona akijishusha (kwa mujibu wa fikra zao) namna ile.

Akamfungulia Mbowe na kumualika ikulu kufanya nae mazungumzo. Baada ya kukisia kilio cha muda mrefu cha maaskofu na wanaharakati wenye kutoa maoni yao kwa vyombo vya habari. Ameonyesha uwezo wa kujishusha na kufanya mijadala ya kimaongezi. Amejitahidi kuliishi jina lake 'suluhu' kwa vitendo.

Lakini anao maadui kwani huwezi kuongoza nchi ukakubalika kwa kila raia unayemuongoza, haijawi kutokea hali ya aina hiyo mahali popote haswa kwenye nchi zilizo katika michakato ya ukuzaji wa demokrasia ya kivitendo kama Tanzania. Binafsi nimemuelewa sana Rais Samia.

Wapo wale wenye mawazo ambayo kwa kingereza wanaitwa ni conservative. Wapo wale wenye hulka kwamba Mwanamke hana hadhi ya kuwaongoza wanaume, wapo wale waliomkubali mno hayati JPM na kile alichokuwa akikihubiri majukwaani na kukiishi kila siku. Wapo wale ambao ni 'waafrika' kweli kweli wenye mawazo yale yale ya mzungu kuvalishwa mtumba baada ya mwafrika kutengeneza nguo akaivaa na kisha akaisafirisha kuipelekea Ulaya.

Hawa wanaona siku zote kuwa viatu vya hayati JPM ni vikubwa mno kwa Samia kuweza kuvivaa na vikamtosha, tatizo lao lipo akilini zaidi. Ndani ya ufikiriaji mzima (mindset) walionao. Ni ngumu kuweza kuwabadilisha kile wanachofikiria. Hawakuweza kuijua mipango ya Mungu walidhani maadam JPM alishaapa na kuingia ikulu basi angeendelea mpaka 2025. Kipindi kile cha msiba, hawa ni miongoni mwa waliolia hadharani na kwa uchungu mkubwa.

Ni kama wana hasira fulani japokuwa wakiulizwa wanakana kwamba hawana kinyongo au ghadhabu inayowasumbua. Hawa ni maadui wanaokua katika suala zima la mbinu za kuupinga uongozi wa awamu ya sita. Walimpenda JPM lakini wanashindwa kuelewa ni kwamba Samia alikuwa msaidizi muhimu wa JPM. Wanamnyanyapaa kwa sasa wakiwa mbali ya kamera lakini enzi za uhai wa JPM walifanya hivi hadharani kabisa, hawakuijua mipango ya Muumba ni ipi.

Ninapenda kumkumbusha Rais SSH kwamba upole wa awamu yake unaweza huko mbeleni kuleta ugumu wa kuelezea haya anayoyafanya kwa sasa, kama yameyagusa maisha ya mtu mmoja mmoja. Kwa maana kwamba hawa wanaojichekesha mbele ya macho yake wanaitumia mitandao kwa mapana ili aonekane hana anachokifanya.

Hawa jamaa wa JPM wamegeuka kuwa ni mabingwa wa utengenezaji wa hizi fake news zinazozagaa mitandaoni. Tatizo ni kwamba habari inaweza kuwafikia watanzania 10000 na kati yao watakaoamini ni 9500 na pakawepo watu makini 500 wenye kuweza kuielewa hiyo propaganda kwa kina.

Lakini tayari wapo wale 9500 waliokwisha kuaminishwa na kile kinachokuwemo katika habari ya kubuni isiyo na ukweli wowote. Ikiwekwa mtandaoni habari nyingine itasomwa na watu milioni moja. Kati ya hao watakaoiamini wanaweza kuwa ni laki tisa na ile laki moja ikaweza kuitilia mashaka. Wale laki tisa ni wengi kiasi cha kuamini uzushi kuwa ni habari ya ukweli.

Rais SSH aitumie nafasi hii kulishughulikia hili tatizo kabla halijawa sugu na kukwamisha ufanisi wa kile anachokifanya ambacho kwa kiasi kikubwa na umaliziaji wa miradi iliyoachwa na hayati JPM. Akiwa hai JPM aliweza kuishughulikia mitandao inayosambaza fake news na akaogopwa kwani msimamo wake ulieleweka kwa kila mtu.

Rais SSH kwa upole na uungwana wake ataivumilia hii hali lakini itakwenda ikiharibu kile anachotaka kukifanya. Wanaopotoshwa na fake news ni wengi, na uwezo wetu wa kupima ukweli na mantiki ya kile kinachoandikwa na kusambazwa mtandaoni siku zote unatofautiana.

Wanaopaka matope ufanisi wa serikali hufanya hivyo kwa kivuli cha demokrasia hata kama wanawafanyia kazi watu wenye nia ovu dhidi ya serikali na mipango yake. Ni hali ya kuishughulikia kwa kutumia busara na umakini wa hali ya juu.
Samia hawezi kuongoza nchi kwa ukatili Kama alivyokuwa anaongoza magufuli,na alishasema kuhusu hilo,

Magufuli na ukatili wake na Bado watu waliiba Sana,
Uzalendo wa bwana yule labda hile kumuweka mpwae pale HAzina (p.general)
 
Kama unakiri kwenye andiko lako kuwa Rais SSH hawezi kupendwa na raia wote, kwa nn unashauri awe mkali wasijempanda mabegani?
Nadhali hili neno DEMOKRASIA kwake linajipambanua kiasi flani kulinganisha na mtangulizi wake.
Lakini pia inaonyesha Rais SSH alikuwa mnafiki kwa nafasi aliyokuwa nayo ya umakamu wa rais.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom