Rais Samia, ulitaka kutuhutubia au kuzungumza nasi?

Binafsi nlijiandaa sana kuja kuongea na Mh. Rais nimweleze changamoto na masuluhisho kadhaa kwa baadhi ya changamoto tulizo nazo vijana mitaani.

Achana na mawaziri hawa wahajui changamoto zetu sababu hawajavaa viatu vyetu. Mimi sikuja na chama chochote. Nlikuja na hoja na naona ntaondoka nazo kama nlivyokuja nazo.

Nliamini tunakuja zungumza na Rais wetu. Kumbe tunakuja elezewa mambo kadhaa na watu kadhaa
Aisee pole sana. Hiyo ndo inaitwa kutumika kisiasa... Imeishia hiyooo
 
Yaani nyie vijana nilifikiri mnaenda kuzungumza na Rais... afadhali hata wazee wa Dar walipata nafasi ya kutoa ya moyoni.... hotuba za viongozi na wabunge ziliwapotezea nafasi adhimu.... poleni sana.
Kwa ccm kiongozi kuhutubia watu huwa wanaita ni kuongea na watu.
 
Haya mambo ya kiongozi mkuu kuongea na wananchi mara nyingi ni Public Relations na kupiga Kampeni. Mfumo mzuri na sustainable na wenye tija ni kero zote kupitia kwa wawakilishi ambao wapo kila ngazi, na sababu Rais ni Taasisi nina uhakika hata akitaka kujua kama bei ya nyanya imepanda pale barabara ya saba chini ya mwembe mkoani Tanga hashindwi.

Hivyo basi nguvu nyingi itumike kwenye kurekebisha kero (sio kujifanya tunasikiliza kero ambazo nina uhakika hata miaka 15 iliyopita zilikuwa ni hizi hizi tu)

Ule ni usanii kama usanii mwingine. Na kama kweli ile ndio namna ya kiongozi kuongea na watu ili kujua matatizo yao, basi ni njia ya kijima kweli kweli.
 
Kwa ccm kiongozi kuhutubia watu huwa wanaita ni kuongea na watu.
Mkuu 'tindo',
Huyu mama alidhani huu mtindo wa kukutana na makundi mbalimbali kutampambanua katika uongozi wake.

Kwa bahati mbaya, hakujiandaa vyema kuitumia hii mikutano kwa lolote; si mlejesho wala lengo maalum analolenga kufanikisha kupitia kwenye mikutano hii.

Mimi simlaumu, huenda amejifunza na ataanza kuitumia kwa malengo maalum anayotaka kuyafikia. Vinginevyo matokeo yake yatakuwa ni kama ulalamishi tunaouona hapa.
 
Mkuu 'tindo',
Huyu mama alidhani huu mtindo wa kukutana na makundi mbalimbali kutampambanua katika uongozi wake.

Kwa bahati mbaya, hakujiandaa vyema kuitumia hii mikutano kwa lolote; si mlejesho wala lengo maalum analolenga kufanikisha kupitia kwenye mikutano hii.

Mimi simlaumu, huenda amejifunza na ataanza kuitumia kwa malengo maalum anayotaka kuyafikia. Vinginevyo matokeo yake yatakuwa ni kama ulalamishi tunaouona hapa.

Ninachokiona kwa huyo mama, ni kama ameamua kuiga style ya Magufuli kwenye kile kinachoitwa kukutana na makundi ya wananchi na kujua kero zao. Nadhani wale washauri Magufuli ndio bado wanamshauri na yeye, hivyo wanampa mbinu za kusaka umaarufu, na sio kutatua matatizo ya watu kwa mantiki ya kutatua. Hivi ni kweli rais hajui matatizo ya vijana mpaka akakutane nao hapo aishie kuwahutubia na wala sio hata mjadala?
 
Alijua sana yale mliyotaka kuongea that's why hakuona sababu ya kutembeza mic kwa vijana wote 50.
Wewe binafsi, una jambo gani jipya kwa mfano?
Kwahiyo wewe unamsemea Mama leo sio!?
Yani umeisoma mind yake!?
 
Hama nchi
Huu ni ujinga wa hali ya juu sana ... Na utaendelea kuwagharimu..
Yani vile wewe ni TAGA ....!! unajitoa akili kabisa.

Lakini msije sema hatukuwakumbusha.

Mamlaka ni za Mungu...aliye juu.. The Almighty GOD.
 
KUDEMKA ni hulka yake huyo.
Binafsi nlijiandaa sana kuja kuongea na Mh. Rais nimweleze changamoto na masuluhisho kadhaa kwa baadhi ya changamoto tulizo nazo vijana mitaani.

Achana na mawaziri hawa wahajui changamoto zetu sababu hawajavaa viatu vyetu. Mimi sikuja na chama chochote. Nlikuja na hoja na naona ntaondoka nazo kama nlivyokuja nazo.

Nliamini tunakuja zungumza na Rais wetu. Kumbe tunakuja elezewa mambo kadhaa na watu kadhaa
 
11 Reactions
Reply
Back
Top Bottom