Rais Samia tusaidie, Uteuzi wa DCI Kingai, Watanzania tunaenda kuzikwa wazima wazima

dubu

JF-Expert Member
Oct 18, 2011
3,496
3,461
20220721_055148.jpg

Shikamoo Rais Samia

Huyu Kingai anaenda kutumaliza, visasi vingi na atahakikisha wabaye wake wanakipata cha mtemakuni.

Kingai haijui hata PGO, atakuwaje Mkurugenzi wa Upelelezi? Twafwa.

Kesi dhidi ya Mbowe ya Ugaidi, nilitegemea imfumbue macho Rais ili ajue waliomzunguka. Naamini rais kashauriwa Vibaya. Tusimlaumu sana sababu bado anayo nafasi ya kubadilisha.

Huu ndo Ushauri Lukuvi anampa rais wetu? Kingai? Huyu wa Kinondoni au yupo Kingai mwingine Jeshini?

Kama Afande Kingai angesoma PGO vizuri, angegundua kuwa SHTAKA linafunguliwa BAADA ya mtuhumiwa KUHOJIWA! Ikibainika "maelezo ya onyo" yanafichua KOSA, ndipo Jalada la Mashtaka HUANDALIWA. Kingai alipoulizwa na Wakili wa Serikali kwanini aliwatoa watuhumiwa Moshi kuwaleta DSM,

alijibu, "huko ndiko mashtaka yao yalipofunguliwa!" Sasa, ilikuwaje ukafungua mashtaka ya hawa Vijana wakati bado hawajakamatwa, na wala KUHOJIWA!

PGO isomwe jamani, tena isomwe vizuri! Mnadhalilisha hili Jeshi.

Kingai alimnyima dhamana mtu aliyehoji kutaka kujua kama Hayati Magufuli anaumwa. Eti hakupasa kuhoji akakamatwa akapigwa na kunyimwa dhamana.

Aloshiriki kumdanganya rais Samia ili amteue Kingai, achukuliwe hatua.

20220721_053606.jpg

Screenshot_20220721-055110.png
 
Polisi hawafungui mashtaka. Mashtaka yanafunguliwa na DPP.

Polisi wanapokea malalamiko na wakiona ni malalamiko ya jinai wanayaandika kwenye daftari la taarifa na kukupa namba ya taarifa (RB). Malalamiko yanazaa tuhuma. Tuhuma ndo zinakufanya ukamatwe na Polisi kwa ajili ya mahojiano.

Mahojiano yatafanyika kule ambako malalamiko yalipokelewa.

Kwa hiyo hapo inatakiwa ujiongeze uelewe kwamba hayo ambayo huyo afisa wa polisi aliyaita "mashtaka" alikuwa anaaminisha malalamiko. Kama kukosea ni amekosa lugha tu, ila sio utendaji.

Kama malalamiko yalipokelewa Dar, na mlalamikiwa yuko Moshi atakamatwa na kupelekwa Dar akahojiwe.
 
Watawala wanaoingia madarakani kwa wizi wa kura, huchagua viongozi wa vyombo vya dola wanaowatii bila kuhoji maagizo yao, na wala hawachagui viongozi kutokana na uwezo wa kazi husika. Kwa bahati mbaya kwenye taasisi zote za umma, uteuzi hufanyika kwa utashi wa mteuzi na sio ubora wa mteuliwa.
 
Huwa siwaelewi mnavyoandika kila siku Rais anadanganywa, au Rais anashauriwa vibaya, kama vile Rais ni mtoto mdogo asiyejua chochote.

Iko hivi, kwenye huu uteuzi wa Kingai, na wengine wote wa sampuli yake, mamlaka ya uteuzi ilijua vizuri nini inachofanya.

Ili wakupe "shavu" lazima uwathibitishie wewe ni mwenzao, na unatii amri zao, hasa zile mbaya [utekaji na utesaji]. Hapa Kingai alisha "graduate" kwa vitendo [refer Adamoo, Kasekwa, na Lijenje].

Wakishajiridhisha hapo ndio unapewa cheo, suala la kuangalia public interest/opinion, au knowledge [PGO] kwao halipo, kwani huyo Kingai haendi kuifanyia kazi public, anaifanyia kazi mamlaka iliyomteua.
 
CCM ina laana,badala ya kuteua watu wenye weledi kama hawa, unateua Mapaka!🐒🐒🐒
 
Watawala wanaoingia madarakani kwa wizi wa kura, huchagua viongozi wa vyombo vya dola wanaowatii bila kuhoji maagizo yao, na wala hawachagui viongozi kutokana na uwezo wa kazi husika. Kwa bahati mbaya kwenye taasisi zote za umma, uteuzi hufanyika kwa utashi wa mteuzi na sio ubora wa mteuliwa.
Nafurahi sana kwamba machadema mnateseka!

Kingai mi 5 tena!

By the way.. Mbaya wenu si alishakufa na sasa mnapumua?
 
Back
Top Bottom