figganigga
JF-Expert Member
- Oct 17, 2010
- 25,491
- 54,884
Najua Polisi wa Tanzania wamejipa jukumu la kuhakikisha rais unatawala Milele. Waambie wakutetee lakini roho zetu watuachie. Watanzania wote ni ndugu uwe Polisi Mgambo au Mpiga debe
Soma Ujumbe kaandikiwq baba Askofu
=====
POLISI WAFANYA MAUAJI YA KUTISHA KIJIJI CHA IKWAMBI, KATA YA MOFU, MLIMBA KATIKA WILAYA YA KILOMBERO, MOROGORO!
Mpendwa Baba Askofu Mwamakula!
Huku kwetu katika Kijiji cha Ikwambi, Kata ya Mofu, katika Halmashauri ya Mlimba (Jimbo la Uchaguzi la Mlimba) Wilaya ya Kilombero katika Mkoa wa Morogoro kumetokea mauaji ya kutisha ya raia wawili yaliyofanywa na Jeshi la Polisi kutoka Ifakara Mkoani Morogoro.
Chanzo cha mauji hayo ni migogoro ya muda mrefu kati ya wakulima na wafugaji. Wakulima wamekuwa wakilalamika kwa uongozi wa Kijiji na Kata kuhusu kuharibiwa mazao yao pamoja na kupigwa na wafugaji kila mara wanakienda mashambani kulima. Tatizo hilo halijawahi kupatiwa ufumbuzi. Kuna hisia kuwa wafugaji huwahonga viongozi. Baada ya kuchoshwa na matukio hayo, wakulima waliamua kundamana leo asubuhi tarehe 23 Oktoba 2022 kwenda katika Ofisi za Kijiji. Wakawakamata Wenyeviti wa Vitongoji, Mwenyekiti wa Kijiji, Diwani pamoja na Polisi Kata, wakawaweka chini ya ulinzi na kuwafungia ndani ya Ofisi
Baada ya hapo, Polisi kutoka Mlimba walifika eneo la tukio na baadaye wakaongezewa nguvu na Polisi kutoka Ifakara. Baada ya majadiliano kati ya Polisi na wananchi kuwa magumu, Polisi walianza kupiga mabomu ya machozi na baada ya mabomu kuwaishia wakaanza kutumia silaha za moto na kuua watu wawili kwa kuwapiga risasa za kifuani na kuwajeruhi wengine kadhaa.
Baada ya mauaji hayo, Polisi wakaondoka na kukimbia na viongozi wa viongozi, Kijijini, Polisi Kata na Diwani na kuondoka nao na kuacha miili ya marehemu mahali pale ikiwa inazagaa!
Tunaomba Baba Askofu tusaidie ujumbe huu ufike hata Kwa wakubwa maana huku kwetu mawasiliano ni hafifu na mambo kama haya ni rahisi kunyamaziwa.
Ni Mimi ...
Mwanachi wa Kijiji cha Ikwambi,
Kata ya Mofu, Mlimba,
Wilaya ya Kilombero, Morogoro
23 Oktoba 2022.
Soma Ujumbe kaandikiwq baba Askofu
=====
POLISI WAFANYA MAUAJI YA KUTISHA KIJIJI CHA IKWAMBI, KATA YA MOFU, MLIMBA KATIKA WILAYA YA KILOMBERO, MOROGORO!
Mpendwa Baba Askofu Mwamakula!
Huku kwetu katika Kijiji cha Ikwambi, Kata ya Mofu, katika Halmashauri ya Mlimba (Jimbo la Uchaguzi la Mlimba) Wilaya ya Kilombero katika Mkoa wa Morogoro kumetokea mauaji ya kutisha ya raia wawili yaliyofanywa na Jeshi la Polisi kutoka Ifakara Mkoani Morogoro.
Chanzo cha mauji hayo ni migogoro ya muda mrefu kati ya wakulima na wafugaji. Wakulima wamekuwa wakilalamika kwa uongozi wa Kijiji na Kata kuhusu kuharibiwa mazao yao pamoja na kupigwa na wafugaji kila mara wanakienda mashambani kulima. Tatizo hilo halijawahi kupatiwa ufumbuzi. Kuna hisia kuwa wafugaji huwahonga viongozi. Baada ya kuchoshwa na matukio hayo, wakulima waliamua kundamana leo asubuhi tarehe 23 Oktoba 2022 kwenda katika Ofisi za Kijiji. Wakawakamata Wenyeviti wa Vitongoji, Mwenyekiti wa Kijiji, Diwani pamoja na Polisi Kata, wakawaweka chini ya ulinzi na kuwafungia ndani ya Ofisi
Baada ya hapo, Polisi kutoka Mlimba walifika eneo la tukio na baadaye wakaongezewa nguvu na Polisi kutoka Ifakara. Baada ya majadiliano kati ya Polisi na wananchi kuwa magumu, Polisi walianza kupiga mabomu ya machozi na baada ya mabomu kuwaishia wakaanza kutumia silaha za moto na kuua watu wawili kwa kuwapiga risasa za kifuani na kuwajeruhi wengine kadhaa.
Baada ya mauaji hayo, Polisi wakaondoka na kukimbia na viongozi wa viongozi, Kijijini, Polisi Kata na Diwani na kuondoka nao na kuacha miili ya marehemu mahali pale ikiwa inazagaa!
Tunaomba Baba Askofu tusaidie ujumbe huu ufike hata Kwa wakubwa maana huku kwetu mawasiliano ni hafifu na mambo kama haya ni rahisi kunyamaziwa.
Ni Mimi ...
Mwanachi wa Kijiji cha Ikwambi,
Kata ya Mofu, Mlimba,
Wilaya ya Kilombero, Morogoro
23 Oktoba 2022.