#COVID19 Rais Samia: Tanzania tuna wagonjwa wa Wimbi la Tatu la Corona

Shujaa Mwendazake

JF-Expert Member
Jul 11, 2015
3,735
6,292
“Tanzania tuna wagonjwa wa wimbi la Tatu la Corona. Hili jambo bado lipo, tuchukue hadhari zote na tunawaomba viongozi wa dini mseme hili kwa sauti kubwa"

Rais Samia Suluhu Hassan wakati akizungumza na baraza la maaskofu katoliki (TEC) #Tanzania #COVID19

=========

Rais Samia Suluhu: Wahashamu, baba Maaskofu kama mnavyofahamu, dunia kwasasa inakabiliwa na mlipuko wa Covid-19 na nafahamu kanisa tangu mwanzo limekuwa na msimamo Thabit katika kupambana na ugonjwa huu hivyo basi niwaombe sana Maaskofu msisahau kuwakumbusha waumini kuhusu wa kujikinga na kuchukua Tahadhari zote zinazoelekewa na wataalam wa Afya dhidi ya ugonjwa wa Corona.

Kwakuwa Kinga ni Bora kuliko Tiba, tusiache kutumia kila kitakachotukinga na maradhi haya ili kuepesha vifo vya makundi.

Kama tunavyojua, duniani sasa hivi kuna wimbi la tatu la Corona, tumetoka kwenye wimbi la kwanza Tanzania tumeingia, limekwenda limepungua kidogo, tumeingia Wimbi la Pili tumekwenda nalo na sasa kuna Wimbi la Tatu.

Ishara ndani ya nchi tayari zinaonekana, tayari tuna wagonjwa ambao wameshaonekana katika kwenye wimbi hili la Tatu. Kama mnakumbuka siku nilitembelea hospitali ya Mwananyamala, kuna wodi daktari mfawidhi alikuwa ananiingiza akaniambia humu kuna wagonjwa wenye matatizo ya kupumua, nikamwambia hebu kuwa muwazi, ni covid, akaniambia ndio Covid wakati wapiga picha wangu tayari wameshatangulia, nikawaambia nyie tokeni haraka huko.

Kwahiyo ni kusema kwamba hili jambo bado lipo, tusijiche, bado lipo tuchukue hadhari zote na tunawaomba sana viongozi wa Dini mliseme hili kwa sauti kubwa, kwa waumini wetu ili tujiepushe na vile vifo vya makundi.

Pamoja na yote hato, ni vyema pia tumuombe Mungu kwa kiasi kikubwa aendelee kutuepusha na kutupa hifadhi yake kutokana na maradhi hasa Janga hili la Corona kwakuwa yeye ndio Muweza wa Yote.

 
Hilo wimbi la tatu liko kwenye magazeti na televisheni, lakini huku mtaani hakuna cha wimbi wala bibi yake na wimbi.

Hizo fedha za wazungu mlizokula hakika mtazitapika majizi nyinyi. Maana hamuishi kuweweseka na makorona kama visungura tope.

Huku Buzza kwanza hatujui hata maana ya corona. Tunaisikiaga tu kwenye mitandao na majarida.

Kwendeni huko na mabarakoa yenu uchwara!

Matapeli wakubwa!
 
Sawa mama SSH. Siyo kama yule alikuwa anawafokea mpk viongozi wa dini waliovaa barakoa. Alikuwa akiwananga kwamba hawana Imani kwa Mungu wanayemtumikia. Yule yule mtu yule!!!

Kongole mama.
Na ni bora aliwafokea hao maaskofu uchwara.

Hakuna dini inayofundisha kutapeli watu kwa magonjwa ya kuigiza.

Nyinyi madalali na vibaraka wa wazungu kiama chenu hakipo mbali.

Hatuwezi kuruhusu mliangamize taifa kwa machanjo yenye sumu.
 
25 June 2021

MKUTANO WA RAIS SAMIA SULUHU NA BARAZA LA MAASKOFU KATOLIKI TANZANIA TEC



Ishara zinaonekana Covid-19 tayari ipo Tanzania, katika ziara yangu ya hivi karibuni hospital ya Mwananyamala jijini Dar es Salaam, niliambiwa kuwa hii ni wodi ya wagonjwa wenye changamoto ya kupumua nikamuliza mganga mfawidhi kuwa muwazi ni nini hicho (changamoto ya kupumua), akanithibitishia ni Covid -19. Hivyo nikahepa kuingia ktk wodi hiyo ingawa wapiga picha wangu na wengine ktk msafara wangu walishakuwa wameingia mimi na wengine tukaamua kuacha kuingia ktk wodi hiyo. Hivyo tuendelee kuchukua tahadhari.
 
Bimkubwa kwenye hili la Corona ni kama kuna Taasisi za nje anataka kuzifurahisha. Ila tulio wengi tumeshakataa kwamba Corona haipo TZ na ndio maana tunashonana kwenye mwendokasi na masokoni bila barakoa na hautuoni hospitali kuwekewa Oxygen.

Bongo korona hakuna, Period!
 
Back
Top Bottom