Nebuchadinezzer
JF-Expert Member
- Oct 1, 2018
- 1,403
- 2,545
Nchi ya Tanzania ina watu takribani milioni 60, kila mtu ana vipaumbele vyake, hivyo huwezi kumridhisha kila mtu mama.
Asilimia 90 ya watanzania ni maskini: hawahitaji magari ya benzi wala nyumba za kishi baada ya kustaafu kushika chaki na kazi zingine za umma.
Wanahitaji maji safi na salama, huduma bora za afya, elimu bora na huduma zingine za kijamii.
Ukitaka kuwafurahisha baadhi ya watu kwenye asilimia 15 iliyobakia utapotea! Utabaki kukumbukwa kwa kuharibu nchi na hatma yake utakutana na mkono wa Allah aliyekupa nafsi hiyo.
Mama Samia, hutapendwa kwa kwenda kinyume na mtangulizi wako kwenye mambo yenye maslahi ya nchi. Mwenzako kamaliza zamu yake. Nadhani umeshuhudia namna umma wa watanzania ulivyompokea licha ya madhaifu yake kama binadamu.
Kikubwa timiza wajibu wako ukiingozwa na katiba na uzalendo wa hali ya juu.
Tumia nguvu uliyopewa, usipende kufanyiwa maamuzi na watu. Wengine baadhi ya washirika wako sio wema.
Wapinzani ni wapinzani tu, lengo lao kuchukua nchi hivyo kuwa nao makini.
Usiingie mkenge kwa kivuli cha kujenga umoja wa kitaifa. Nchi hii ni moja na hakuna mpasuko wowote labda mitandaoni ila uraiani tupo wamoja sana. Na hayati Magufuli ametupa nguvu sana kiasi kwamba tunajua kipi kizuri na kipi kibaya.
Mwisho nakutakia kila la kheri.
Happy Mothers' Day!
Asilimia 90 ya watanzania ni maskini: hawahitaji magari ya benzi wala nyumba za kishi baada ya kustaafu kushika chaki na kazi zingine za umma.
Wanahitaji maji safi na salama, huduma bora za afya, elimu bora na huduma zingine za kijamii.
Ukitaka kuwafurahisha baadhi ya watu kwenye asilimia 15 iliyobakia utapotea! Utabaki kukumbukwa kwa kuharibu nchi na hatma yake utakutana na mkono wa Allah aliyekupa nafsi hiyo.
Mama Samia, hutapendwa kwa kwenda kinyume na mtangulizi wako kwenye mambo yenye maslahi ya nchi. Mwenzako kamaliza zamu yake. Nadhani umeshuhudia namna umma wa watanzania ulivyompokea licha ya madhaifu yake kama binadamu.
Kikubwa timiza wajibu wako ukiingozwa na katiba na uzalendo wa hali ya juu.
Tumia nguvu uliyopewa, usipende kufanyiwa maamuzi na watu. Wengine baadhi ya washirika wako sio wema.
Wapinzani ni wapinzani tu, lengo lao kuchukua nchi hivyo kuwa nao makini.
Usiingie mkenge kwa kivuli cha kujenga umoja wa kitaifa. Nchi hii ni moja na hakuna mpasuko wowote labda mitandaoni ila uraiani tupo wamoja sana. Na hayati Magufuli ametupa nguvu sana kiasi kwamba tunajua kipi kizuri na kipi kibaya.
Mwisho nakutakia kila la kheri.
Happy Mothers' Day!