Roving Journalist
JF Roving Journalist
- Apr 18, 2017
- 3,807
- 13,577
Rais Dkt. Samia ametoa agizo hilo Kilosa Mjini leo Agosti 03, 2024 katika hafla ya ufunguzi wa wa barabara Rudewa - Kilosa (km 24) iliyokamilika kujengwa kwa kiwango cha lami Mkoani Morogoro.
Aidha, Dkt. Samia ameeleza kuwa Morogoro ni mkoa wa kimkakati kwa maendeleo ya miundombinu ambapo kwa kipindi cha miaka mitatu Serikali kupitia TANROADS imeupatia Mkoa huo kiasi cha Shilingi Bilioni 78.7 kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya barabara na madaraja.
Dkt. Samia ameeleza kuwa Serikali inakwenda kukamilisha ujenzi wa barabara katika kipande kilichobakia cha kuunganisha Wilaya ya Kilosa na Mikumi katika barabara ya Dumila – Kilosa – Ulaya – Mikumi (km 142) kwa kiwango cha lami katika mradi huo.
Vilevile, Dkt. Samia ameipongeza Wizara ya Ujenzi, TANROADS na Wakandarasi Wazawa waliotekeleza na kukamilisha ujenzi wa barabara ya Rudewa - Kilosa (km 24) kwa kiwango cha lami kwa gharama ya Shilingi Bilioni 45.6.
Kwa upande wake, Waziri wa Ujenzi Innocent Bashungwa ameeleza kuwa barabara ya Rudewa - Kilosa (km 24) ni sehemu ya barabara muhimu kwa kuwa inaunganisha Mkoa wa Tanga, Morogoro na Nyanda za Juu Kusini ambapo inaanzia Bandari ya Tanga - Handeni - Mziha - Turiani - Dumila - Kilosa - Mikumi - Ifakara - Mlimba - Lupembe hadi Mkoani Njombe.
Bashungwa ameeleza kuwa Wizara ya Ujenzi imetengewa zaidi ya Bilioni 800 kwa ajili ya kuanza utekelezaji wa ujenzi wa miundombinu ya barabara iliyoathirika kutokana na mvua za El-Nino katika mikoa yote nchini kipindi hiki cha kiangazi ambapo hivi sasa kazi za manunuzi zimeanza kwa ajili ya utekelezaji na Mkoa wa Morogoro ukiwemo.
Awali akitoa taarifa ya mradi, Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS), Mhandisi Mohamed Besta ameeleza barabara ya Dumila – Kilosa – Ulaya - Mikumi (km 142) ni barabara ya Mkoa inayounganisha barabara kuu ya Morogoro – Dodoma katika eneo la Dumila na barabara kuu ya TANZAM katika eneo la Mikumi.
Besta ameeleza ujenzi wa barabara ya Rudewa - Kilosa umetekelezwa na kampuni ya wazawa ya M/s Umoja Kilosa JV yenye muunganiko wa Makandarasi saba (7) Wazawa na Mhandisi Mshauri kampuni ya PIDAEL JV Consulting Engineers ya Tanzania kwa gharama ya Shilingi Bilioni 45.6 zikihusisha gharama za fidia, ujenzi na usimamizi.