MINOCYCLINE
JF-Expert Member
- Apr 2, 2015
- 8,011
- 16,748
Watanzania mnanishangaza sana hasa nikiwasikia Vijiweni na mnavyodanganywa na Waziri Mkuu Majaliwa na Katibu Mkuu Wizara ya Michezo Dk. Abbas kuwa Tanzania kupitia Taifa Stars itafuzu Kombe la Dunia kwa Alhamisi kumfunga Congo DR na Jumapili kumfunga Madagascar.
Kama Wachezaji wao Wawili tu wanaotamba Tanzania na kila Siku tunawaimba akina Yanick Bangala na Fiston Mayele hawajulikani Kikosini na hata Namba hawana hamjiulizi tu hao waliopo ( walioitwa ) ndiyo balaa zaidi na wanaenda Kutuumbua kwa Kutufunga Alhamisi pamoja na kwamba tumetenga Tsh 1.4 Bilioni ( ambapo humo humo ) hata ya Kumhonga Mwamuzi / Refa na Wasaidizi wake imetengwa?
Tanzania mpaka hivi sasa tunajivunia Wachezaji wanaocheza Soka la Kulipwa Nje Watatu tu Mbwana Samatta, Simon Msuva na Novatus Dismas wakati Congo DR ina Wachezaji zaidi ya 83 wanaocheza Soka la Kulipwa na 99.9% wapo katika Msafara wa kuja Kututia Adabu Tanzania kupitia Taifa Stars yetu Keshokutwa Alhamisi katika Uwanja wa Benjamin Mkapa.
Ninachojua Ushindi wa Tanzania na Taifa Stars yetu Keshokutwa ( Alhamisi ) ni Sare ya Pacha ( ya Magoli ) au Sare ya Suluhu ( isiyo na Magoli ) ila kwa 85% KEROZENE kwa ninavyowajua Wakongo, Uwezo wao, Mbinu na Mikakati yao ya ndani na nje ya Uwanja wanaenda Kutufunga hapa hapa katika Ardhi yetu.
Ng'ombe hanenepeshwi Siku ya Mnada.
Kama Wachezaji wao Wawili tu wanaotamba Tanzania na kila Siku tunawaimba akina Yanick Bangala na Fiston Mayele hawajulikani Kikosini na hata Namba hawana hamjiulizi tu hao waliopo ( walioitwa ) ndiyo balaa zaidi na wanaenda Kutuumbua kwa Kutufunga Alhamisi pamoja na kwamba tumetenga Tsh 1.4 Bilioni ( ambapo humo humo ) hata ya Kumhonga Mwamuzi / Refa na Wasaidizi wake imetengwa?
Tanzania mpaka hivi sasa tunajivunia Wachezaji wanaocheza Soka la Kulipwa Nje Watatu tu Mbwana Samatta, Simon Msuva na Novatus Dismas wakati Congo DR ina Wachezaji zaidi ya 83 wanaocheza Soka la Kulipwa na 99.9% wapo katika Msafara wa kuja Kututia Adabu Tanzania kupitia Taifa Stars yetu Keshokutwa Alhamisi katika Uwanja wa Benjamin Mkapa.
Ninachojua Ushindi wa Tanzania na Taifa Stars yetu Keshokutwa ( Alhamisi ) ni Sare ya Pacha ( ya Magoli ) au Sare ya Suluhu ( isiyo na Magoli ) ila kwa 85% KEROZENE kwa ninavyowajua Wakongo, Uwezo wao, Mbinu na Mikakati yao ya ndani na nje ya Uwanja wanaenda Kutufunga hapa hapa katika Ardhi yetu.
Ng'ombe hanenepeshwi Siku ya Mnada.