Rais Samia Suluhu tumsamehe Sabaya, inatosha

Neno la Mungu siku zote hupelekewa kwenye uovu. Neno la Mungu limeletwa ili kutumika katika uovu na kwa neno hilo waovu waponywe. Kama ulivyosena kuwa Paulo hakuna mhalifu kwa sababu aliua kwa kufuata Torati basi yatupasa kuamini kuwa Sabaya hakua mkosefu ila torati. Kama kusingalikua na wakosefu, waovu; basi neno la Mungu lingalikosa maana. Narudia, msamaha ni darasa lenye maana kuliko adhabu.
 
ManukaJr;

Kwa kuwa kidogo utetezi wako dhidi ya ndugu yetu huyu (Sabaya) umetumia Neno la Mungu huku reference ikiwa ni Mtume Paulo.
Basi kwa hili, imenibidi nami niandike kujibu..

IKO HIVI;

1. Mtu kusamehewa dhambi zake ni jambo moja na kwa mtu kuendelea kutibu majeraha ya dhambi hizo ni kitu kingine kabisa...

2. Sasa nikuulize swali hili; Je, Ole Lengai Sabaya kwa kinywa chake na kwa moyo wake amekiri kuwa ni mwenye dhambi mbele za Yehova ili apokee msamaha huo? Kama bado, mpelekee injili ya neema ya msamaha kwanza ktk Yesu Kristo kisha achukue maamuzi ya busara kutubu...

3. Akishatubu na kusamehewa hilo liende sambamba na kuwaomba msamaha wote na kuwarejeshea chochote kile alichochukua bila ridhaa yao wote aliowatendea ubaya....

Hii kanuni haimuhusu Sabaya tu bali inatuhusu sisi wanadamu wote...

4. Ndugu yangu kila jambo lina kusudi na wakati wake kutendeka. Huyu Sabaya kupitia hatua hizo ni kama njia tu ya kumfanya aje kuwa mtu bora zaidi ktk jamii. Hakuna anayemchukia. Hapo anacheza na matokeo ya matendo yake mabaya aliyoyatenda. Hilo haliepukiki ni lazima apite humo...

Unachokiomba wewe kwa Sabaya, ni sawa na kumshurutisha Mungu atende kwa mapenzi yako na si kama vile atakavyo yeye...

5. Umemtumia Mtume Paulo kama reference ktk kujenga hoja yako ya "msamaha wa Sabaya". Lakini usisahau kuwa, mpaka Paulo kuwa mtumishi na mtume aliyetenda kazi kubwa sana ktk kuuneza ufalme wa Mungu, alipitia mchakato Wa muda mrefu kidogo ktk kumtengeneza ili kufuta uchafu aliokuwa ameubeba...

Kama Sabaya ni " mteule wa Mungu", hahitaji kusemewa na mtu. Bwana atamtengeneza mwenyewe...

Mwambie hivi, aache kulaumu watu wengine kwa madhara (matokeo) ya matendo yake maovu...

Nawe vivyo hivyo, acha kutupia lawama watu wengine kwa matendo mabaya ya ndugu yetu huyu na matokeo yake. Kumbuka hili, kuwa kila mtu ataubeba msalaba wake mwenyewe..

Kila mtu anawajibika kubeba matokeo ya maamuzi yake mwenyewe. Kama alitenda ubaya kwa sababu aliagizwa kufanya vile na mtu mwingine, basi abebe matokeo ya ujinga huo. Asilaumu mtu mwingine...

Atengeneze na Mungu wake yeye mwenyewe. That's all..
 
Ndugu kati ya haya iliyoandika, lipo hata moja limesomwa mahakamani? Kama sivyo, wewe ndiye unayejifucha kwenye kivuli cha Magufuli ili umtete huyu swahiba wako Sabaya.
Shutuma za Sabaya mahakamani ziko dhahiri; rushwa ujambazi wa kutumia silaha na matumizi mabaya ya madaraka. Je haya yanakihusuje chama cha mapinduzi? Walimtuma? Je haya yanahusianaje na ubunge wa Hai na Mbowe? Je haya aliyoyafanya ndio yaliyofanikisha ushindi wa ccm Hai? Maswali ni mengi, ila itoshe kusema tuhuma za Sabaya ni personal na usitake kuihusisha na ccm.
Juu ya mwendazake, ni sahihi kuhusishwa naye kwani ukweli uko wazi. Haya mengi sabaya alifanya wakati wa uongozi wa mwendazake na hakukemewa licha ya kuchukuliwa hatua. Kuweri ni ukweli tu, haufichiki.
Hivyo ndivyo umenielewa. Wengine wamenielewa tofauti, kwa vyovyote kila mmoja aelewe anavyoweza isipokuwa wote tunakutana katika msamaha.
 
Mleta mada, wakati ukisoma michango ya wadau, kaa na vidonge vya kutuliza maumivu jirani.
Sio rahisi kupata maumivu katika maoni rahisi yaliyofunikwa na chuki, ubinafsi, hasira, visasi na ushabiki. Maoni yenye kupingana na msimamo wa maneno ya Mungu hayawezi kuumiza nafsi iliyoshiba msamaha. Ninaendelea kuwasamehe wote wenye kuona tunapaswa kulipa visasi katika maridhiano.
 
Hili jambo tuache Sheria ichukue mkondo wake ili haki itendeke maana hata wewe unakubali ya kuwa kuna makosa amefanya na kama hana makosa haki itendeke. Unachojaribu kukionyesha hapa ni ushabiki wa chama/kisiasa. What if makosa anayotuhumiwa yangekuwa yamefanywa na mtu kutoka upinzani? Sidhani kama ungekuja na haya maelezo yenye mlengo wa kisiasa na kutaka kuonesha huruma.
Nimechagua kupita njia hiyo kwa sababu wenzetu wametangulia. Kama sio kulifanya swala la Sabaya kuwa kisasi cha Ubunge wa Freeman hata mimi (sisi) tungaliacha mambo yaende inavyostahili. Kwa sababu wenzetu wameanza, sisi tumaomba tumalize. #HatutoiPointTatu.
 
Hapana. Hii ndio rasmi, ni bahati mbaya nilichelewa kujumuika katika jukwaa hili, mimi sio mwenyeweji humu. Matusi, kashfa na maoni yasiyozingatia utu vilinichelewesha lakini hata hivyo muda ulipofika sikua na chaguo. Kwa maneno hayo, hii ndio ID yangu rasmi.

Mkuu vipo vi ID vingi vipya vipya huwa vinachipuka chipuka kila upepo mbaya unapowavumia wale watoto wapendwa wa mwendazake au yeye mwenyewe.

Hiki cha kwako bacho kina beba alama zile zile za vidole kama zile za ID zingine.

Au nasema uongo ndugu zangu?
 
Huyo JPM wako ndio alikuwa dhalimu namba moja, na alikuwa hapiganii lolote kwenye nchi hii zaidi ya kutekeleza majukumu yake aliyoyapata kwa mabavu. Usitake kutetea udhalimu kwa kichaka cha kufia nchi. Huwezi kufia nchi huku ukimiliki kundi la wahalifu ili utawale kwa mabavu. Yule alikuwa kiongozi muovu na sio zaidi ya hapo.

Hilo la ubunge wa Hai mnalichomeka ili kucheza mind game. Kwa taarifa yenu ruduni shule mkajifunze propaganda kwani katika hili mmekwama. Sabaya alifanya ukatili wa wazi, huku akijificha kwenye kichaka cha kupambana na upinzani hasa Mbowe. Na aliweza kupata nguvu ya kutekeleza uovu wake, maana aliyemchagua alikuwa muovu mwenzake pia. Kwa maneno mengine hapa umeleta bandiko la kutetea muovu aliye kaburini na aliye jela. Kwenye kundi hilo la watu waovu bado Makonda, Mwigulu nk.
 
Back
Top Bottom