Rais Samia Suluhu kuwa Gorbachev na De Clerk wa Tanzania

Hamatan

JF-Expert Member
Nov 10, 2020
3,183
7,645
Failure of the organisation is failure of the management. Failure of a nation is failure of the leadership, and vice versa.

Kama nchi itaendelea kuwepo kwenye mkwamo wa sasa, au ikaenda kwenye hali mbaya zaidi kuliko ilivyo sasa, tutambue kuwa atakayekuwa amesababisha ni Mh. Rais Samia. Lakini pia, kama Taifa hili litabadilika kutoka kwenye hali mbaya ya sasa na kwenda kwenye ustawi wa kweli, atakayekuwa amesababisha ni Mh. Rais Samia. Siyo wasaidizi wake, maana wasaidizi huteuliwa na yeye. Uteuzi wa wasaidizi nayo ni kipimo cha uwezo wa uongozi.

Kiongozi mwenye upeo mkubwa, uelewa na hekima, anajua amteue na na asimteue nani kama anataka kufikia malengo aliyoyapanga.

Wakati wa Mwungano wa Urusi, USSR, watu kwenye mataifa yaliyotengeneza huo mwungano, waliishi kwenye udikteta wa ajabu, watu walifungwa, waliwekwa vizuizini, wenginebwaliuawa kama kuku walipotaka kuuruka ukuta wa Berlin ili kuyatafuta maisha mazuri Ujerumani Magharibi. Hayo yalitokea na kuendelea kwa miaka mingi na kwa vipindi mbalimbali vya viongozi wa Urusi. Hakuna kiongozi aliyejaribu kuibarilisha hali hiyo.

Ni mtu mmoja tu aliyesababisha watu wote kwenye mataifa yaliyokuwa yanaunda mwungano wa USSR kuwa na uhakika wa kuishi, kuwa na uhuru wa kusafiri, kuwa na uhuru wa kumiliki mali, n.k. Mtu huyo ni Rais MIKHAIL GORBACHEV. Huyu aliamua kwenda kinyume na wenzake ndani ya chama cha kikomunisti.

Kule Afrika Kusini, kwa miaka mingi, watu weusi walibaguliwa, wakllifungwa, waliuawa. Lakini hata wazungu walishambuliwa na kuuawa na watu weusi. Kwa ujumla, ni kuwa hakuna aliyekuwa na amani kamili na uhuru kamili. Mtu mmoja tu aliyeitwa FREDERICK DE CLERK, ndiye aliyebadili kila kitu, na kuleta tumaini la maisha ya furaha, amani na upendo nchini Afrika Kusini na mataifa jirani, Tanzania ikiwa mojawapo. Huyu aliamua kwenda kinyume na katakwa ya kundi lake lililoasisi na kuneemeka na siasa za ubaguzi wa rangi

Katika rejea zote mbili, USSR na Afrika Kusini, walioleta mabadiliko ni watawala ambao walitoka kwenye mfumo wa utawala gandamizi, yaani kutoka kwenye kundi la utawala lililokuwa likineemeka kwa gharama ya mateso na upotevu wa maisha ya makundi mengine.

JE, SAMIA ATAKUWA MIKHAIL GORBACHEV NA FREDERICK DE KLERK WA TANZANIA?
 
Kwa huyu, bora ukasahau tu! Maana hana hizo dalili. Muda si mrefu na yeye madaraka yakimlevya, ataifuata tu njia ya mtangulizi wake.

Hao akina Mikhail Gorbachev walikubali yote! Kutukanwa na hata kuchukiwa na Wahafidhina wa huo Ujamaa! Kwa huyu mama, sitarajii hilo kutokea. Kama kweli angekuwa na hizo sifa, asingejisifia mara kwa mara kufungamana na mtangulizi wake kwa kila kitu.
 
Kwa huyu, bora ukasahau tu! Maana hana hizo dalili. Muda si mrefu na yeye madaraka yakimlevya, ataifuata tu njia ya mtangulizi wake.

Hao akina Mikhail Gorbachev walikubali yote! Kutukanwa na hata kuchukiwa na Wahafidhina wa huo Ujamaa! Kwa huyu mama, sitarajii hilo kutokea. Kama kweli angekuwa na hizo sifa, asingejisifia mara kwa mara kufungamana na mtangulizi wake kwa kila kitu.
Nadhani Rais Samia tumpe miezi 6. Kisha tutajua kama ni mleta mabadiliko, mnogeshaji wa masikio, mfurahishaji macho, ni ndumilakuwili, n.k.

Mambo makubwa ambayo kwayo Mh. Samia astahili kupimwa nayo ili kuweza kujua kama kweli ni mtu wa kuleta mabadiliko chanya:

1) upatikanaji katiba mpya

2) uondoaji wa sheria gandamizi - sheria ya mitanadao, sheria ya vyama vya siasa, sheria ya takwimu, sheria ya uhujumu uchumi, sheria ya utakatishaji fedha, sheria ya ugaidi na sheria ya uchaguzi.

3) uimarishaji na usafishaji wa taasisi mbalimbali ambazo kwa kipindi kirefu zimekuwa hazifanyi kazi kwa maslahi ya Taifa bali kwa maslahi ya chama - Jeshi la Polisi, TISS na NEC

4) Kufuta kinga ya Rais, Spika na Jaji Mkuu kutoshtakiwa

Kama hatayagusa maeneo hayo matatu, hakika itakuwa ni kupoteza muda na kujipa faraja zisizo na mizizi kuamini kuwa Samia ataleta mabadiliko yatakayoweka misingi mipya, imara na iliyo bora ya uongozi, inayoweza kulibadilisha Taifa hili ambalo Rais hutawala kama mfalme bila ya kulazimishwa kufanywa chochote ambacho umma unataka.
 
Failure of the organisation is failure of the management. Failure of a nation is failure of the leadership, and vice versa.

Kama nchi itaendelea kuwepo kwenye mkwamo wa sasa, au ikaenda kwenye hali mbaya zaidi kuliko ilivyo sasa, tutambue kuwa atakayekuwa amesababisha ni Mh. Rais Samia. Lakini pia, kama Taifa hili litabadilika kutoka kwenye hali mbaya ya sasa na kwenda kwenye ustawi wa kweli, atakayekuwa amesababisha ni Mh. Rais Samia. Siyo wasaidizi wake, maana wasaidizi huteuliwa na yeye. Uteuzi wa wasaidizi nayo ni kipimo cha uwezo wa uongozi.

Kiongozi mwenye upeo mkubwa, uelewa na hekima, anajua amteue na na asimteue nani kama anataka kufikia malengo aliyoyapanga.

Wakati wa Mwungano wa Urusi, USSR, watu kwenye mataifa yaliyotengeneza huo mwungano, waliishi kwenye udikteta wa ajabu, watu walifungwa, waliwekwa vizuizini, wenginebwaliuawa kama kuku walipotaka kuuruka ukuta wa Berlin ili kuyatafuta maisha mazuri Ujerumani Magharibi. Hayo yalitokea na kuendelea kwa miaka mingi na kwa vipindi mbalimbali vya viongozi wa Urusi. Hakuna kiongozi aliyejaribu kuibarilisha hali hiyo.

Ni mtu mmoja tu aliyesababisha watu wote kwenye mataifa yaliyokuwa yanaunda mwungano wa USSR kuwa na uhakika wa kuishi, kuwa na uhuru wa kusafiri, kuwa na uhuru wa kumiliki mali, n.k. Mtu huyo ni Rais MIKHAIL GORBACHEV. Huyu aliamua kwenda kinyume na wenzake ndani ya chama cha kikomunisti.

Kule Afrika Kusini, kwa miaka mingi, watu weusi walibaguliwa, wakllifungwa, waliuawa. Lakini hata wazungu walishambuliwa na kuuawa na watu weusi. Kwa ujumla, ni kuwa hakuna aliyekuwa na amani kamili na uhuru kamili. Mtu mmoja tu aliyeitwa FREDERICK DE CLERK, ndiye aliyebadili kila kitu, na kuleta tumaini la maisha ya furaha, amani na upendo nchini Afrika Kusini na mataifa jirani, Tanzania ikiwa mojawapo. Huyu aliamua kwenda kinyume na katakwa ya kundi lake lililoasisi na kuneemeka na siasa za ubaguzi wa rangi

Katika rejea zote mbili, USSR na Afrika Kusini, walioleta mabadiliko ni watawala ambao walitoka kwenye mfumo wa utawala gandamizi, yaani kutoka kwenye kundi la utawala lililokuwa likineemeka kwa gharama ya mateso na upotevu wa maisha ya makundi mengine.

JE, SAMIA ATAKUWA MIKHAIL GORBACHEV NA FREDERICK DE KLERK WA TANZANIA?
Je? mama akichukua maamuzi magumu Boris Yetsin atakuwa nani.Mzee Malichela ana Kumbukumbu nzuri na saga ya G 55
 
Back
Top Bottom