Rais Samia Suluhu Hassan, mteue Zitto Zuberi Kabwe awe Mbunge akaongeze chachu ya hoja Bungeni

Bunge letu linahitaji kuongezewa chachu ya aina fulani ili liweze kuichambua kikamilifu Miswada ya Serikali.

Vile vile Bunge letu linahitaji Sauti ya Upinzani yenye kukubalika mbele ya jamii yetu ya Kitanzania.

Kwa kuwa Kada wawili wa CCM wamekuwa Wabunge wa Kuteuliwa, Humphrey Polepole na Dkt. Bashiru Ally Kakurwa, basi ikimpendeza Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan, itapendeza sana Mhe. Zitto Zuberi Kabwe wa ACT-Wazalendo, akateuliwa kuwa Mbunge, katika zile nafasi za Rais.

Hali hii itaimarisha Muungano wetu kwa kuwa ACT-Wazalendo imekubali kushiriki katika Serikali ya Umoja wa Kitaifa Zanzibar.

CCM, kwa upande wa Tanzania Bara, itakuwa imeungana na Rais wa Zanzibar, Dkt. Hussein Ali Mwinyi katika kuonesha dhamira njema ya kushirikiana na makundi yote ndani ya Nchi yetu, katika kuijenga Nchi yetu.
Zitto alipigwa jimboni sasa anaombewa ubunge wa hisani
 
Hahaaaa mwami kama mwami sasa anaombewa Ubunge kwa Mama , hatari sana yaani mambo yanakwwenda kasi sana jamani
 
Sina hakika kama WanaKigoma wote watakubaliana na wewe.
Jamii zetu Tanzania zina kundi dogo la Wafiachama, ambalo kwalo Nchi inakuja baada ya Chama.
Kundi hilo dogo linafurahia Wabunge wote watoke CCM, Madiwani wote watoke CCM.
Kwa wale wengi wanaoipenda Nchi yao kuliko Vyama vyao, wanaamini kuwa SAUTI MBADALA Bungeni inaimarisha AFYA ya Taifa.
Sauti ya Zitto Bungeni ni Sauti Mbadala.
Wanakigoma mpaka sasa wanashangilia kugaragazwa kwa huyo jamaaa yenuuu. Kama zito anafaa siuombe aje awe mbunge wa jumbo lenu hapo ufipani??
 
Kila nikiliangalia Bunge letu la miaka hii minne iliyobaki, na kauli ya Mheshimiwa Mama Samia Suluhu Hassan kueleza bayana kuwa Serikali yake iko tayari kukosolewa, Mbunge aina ya Zitto Zuberi Kamwe, mwenye uwezo mkubwa wa kujenga hoja, ni faida sana kuwa nawe Bungeni.
kazi za mbunge ni.kujenga hoja kwa ajili ya watu wa jimboni.kwake bungeni .Zitto hoja zipi nzito alizowahi jenga kwa ajili ya jimbo lake? Lisu pia hoja zipi alizowahi jenga kwa ajili ya watu wa jimbo lake? tuanzie hapo
 
Katika miaka yake 15 bungeni ambayo alikuwa anafanya ukosoaji nini kimebadilika??
Kukosoa kwa staha, kwa lugha ya Kibunge, na hoja ikafanyanyiwa kazi na Serikali, kwa mujibu wa Katiba yetu, inabidi awe Bungeni.
Ndiyo, ni vizuri kukosoa ukiwa Bungeni.
 
Bunge letu linahitaji kuongezewa chachu ya aina fulani ili liweze kuichambua kikamilifu Miswada ya Serikali.

Vile vile Bunge letu linahitaji Sauti ya Upinzani yenye kukubalika mbele ya jamii yetu ya Kitanzania.

Kwa kuwa Kada wawili wa CCM wamekuwa Wabunge wa Kuteuliwa, Humphrey Polepole na Dkt. Bashiru Ally Kakurwa, basi ikimpendeza Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan, itapendeza sana Mhe. Zitto Zuberi Kabwe wa ACT-Wazalendo, akateuliwa kuwa Mbunge, katika zile nafasi za Rais.

Hali hii itaimarisha Muungano wetu kwa kuwa ACT-Wazalendo imekubali kushiriki katika Serikali ya Umoja wa Kitaifa Zanzibar.

CCM, kwa upande wa Tanzania Bara, itakuwa imeungana na Rais wa Zanzibar, Dkt. Hussein Ali Mwinyi katika kuonesha dhamira njema ya kushirikiana na makundi yote ndani ya Nchi yetu, katika kuijenga Nchi yetu.
TANZANIA INA WATU WENGI WENYE UWEZO SAWA NA ZITTO NA WAPO WALIOMZIDI, SEMA HAWAJAPATA FURSA ALIZOWAHI PATA ZITTO. NAFIKIRI ILI UPINZANI UJIIMARISHE NI VYEMA WASIWE WANAPEWA VYEO VYA HISANI KWANI VINALETA UKAKASI HUKO MBELENI JARIBU KUMUWAZA A.E. MREMA, NA MBATIA JE VYEO WALIVYPEWAGA VILISAIDIA JAMII YAO AU WATZ ZAIDIZAIDI VILIWASAIDIA WAO KWA MUDA FULANI MWISHOWE VIKATUONDOLEA IMANI KWAMBA WALE NI WAPINZANI HALISI, SISHAURI ZITTO AINGIE KWENYE MTENGO HUO KWANI BADO ANANAFASI YAKUFANYA HAYO UNAYOSEMA NA ZAIDI AKIWA NJE YA BUNGE CHA KUSHAURI NI PAWEPO NA TAASISI IMARA NA MADHUBUTI YENYE KUHESHIMU SHERIA NA HAKI YA RAIA WAKE, UHURU WA MAWAZO KINZANI HATA KAMA MUNATOKA CHAMA KIMOJA PASIWE NA WEWE NI MWENZETU USITUKOSOE. HATA NDANI YA CCM WAKIACHA U CCM WAKAJIPAMBANUA KUIJENGA TANZANIA KULIKO KUWAZA CHAMA WANAWEZA TUSAIDIA SANA.(REJEA BASHE KABLA YA KUPEWA UNAIBU WAZIRI PIA REJEA NAPE BAADA YAKUTUMBULIWA UWAZIRI WA HABARI) ALAFU HEBU TUWATIZAME KAMA JENERAL ULIMWENGU, ISSA SHIVYA , TUNDU LISU N.K WASIKUTANENA VIZUIZIVYOVYOTE PALE WANAPOTOA MAWAZO HURU NACHNYA AMBAYO NI MWARUBAINI WA SEREKALI
 
Ubunge wa viti maalum na kuteuliwa ufutwe.
Ni ufujaji tu wa pesa za walipa kodi wavuja jasho.
Unapendekeza nani aende huko badala ya Zitto?
Huko nyuma, Rais Kikwete aliwahi kumteua Mhe. Mbatia kuwa Mbunge.
 
Kamanda Mbowe ni kada mtiifu sana wa CCM kuliko Zitto
Vitu vingine ni siri, haswa zile siri unazozipata wakati wa mambo yetu yale, mtu anajikuta anasema kila kitu, hivyo sio vizuri kutoa nje siri za ndani hivyo!.
Hata wasiojua kuwa ulikuwa naniliu, wanajua!. Siri nyingine mezea!.
P
 
Back
Top Bottom