Rais Samia Suluhu Hassan kuhudhuria Mkutano wa COP 26 Nchini Scotland

Acha kukurupuka, kuna sehemu nimesema mchakato wa pesa za IMF umeanza enzi za mwendazake?au nimesema mchakato wa pesa za IMF umeanza kabla ya bi mkubwa kwenda UN?...
Sasa umeandika nini? Ukweli unabaki kuwa mkopo wa IMF umewezekana baada ya Mama kuwa kwenye madaraka na correct perspective. Tusingerudi kwenye reli tusinge qualify.

Mama anaupiga mwingi tu, nyie mliyemtegemea yule SHETANI mlie tu
 
Hiyo pesa ya safari inatosha kujenga na kukamilisha mradi wa maji kwenye mji wa Namtumbo, tena na nyingine zinabaki za kujenga kituo cha afya na kuiondoa Namtumbo kwenye orodha ya kero za huduma za jamii.
Akili za "old stone age hizo", inawezekana wewe bado ni ile jamii inayoishi kwenye mapango ambayo haina uelewa wa yanayoendelea nje ya pango. Baki na mtazamo na akili hizo, KAZI INAENDELE, NA UKIZINGUA UTAZINGULIWA
 
Walio karibu nae lazima wafurahi, maana wanapata posho Kama zote, ila safari ya rais MOJA ni gharama kubwa Sana , zipo safari anaweza tuma wa kumwakilisha,
Mfano tangu amechukua kiti ameenda Nchi ngapi? na mwa haujaisha, vipi Mpaka 2025?
Shughuli za kiserikali usifananishe na shughuli zako binafsi.
 
Mkuu sisi bado tunaiitaji dunia kusonga mbele, uwepo wake yeye kule ni mkubwa mno kuliko wawakilishi! Wewe ukiwa Rais wa nchi hii utajifungia ndani na kuzuia watu wote kusafiri kama Jiwe?
Mkuu binafsi sipingani na kisafiri , ila KWa safari zenye tija , japo kila safari ina umuhim wake, ila zipo zingine Rais anaweza kuzipima kulingana na uzito wake kwamba lazima awepo yeye binafsi ,au anaweza wakilishwa, Ndo maana anawasaidizi kibao, waziri mkuu, makamo wake , n.k
 
Je Mzee wa Msoga yupo? Maana wanazusha eti New York alikwenda naye. Na Sasa Kuna uvumi wa Scotland
 
Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan anatarajiwa kuondoka Nchini Oktoba 30, 2021 kuelekea Glasgow, Scotland kuhudhuria Mkutano wa 26 wa Umoja wa Mataifa utakaojadili athari za Mabadiliko ya Tabianchi (COP 26).

Anatarajiwa kuhutubia siku ya pili ya Mkutano huo (Novemba 02, 2021) na pia atakutana kuzungumza na baadhi Wakuu wa Nchi, Wakuu wa Mashirika ya Kimataifa, Wakuu wa Taasisi mbalimbali na Wafanyabiashara wakubwa.

View attachment 1990991
Big move
Positive move
 
Back
Top Bottom