Rais Samia Suluhu Hassan, geuka nyuma uone anachofanya DED wa Temeke, aibu!

KooZito

JF-Expert Member
Dec 14, 2020
396
1,377
Enyi wana wema mliojirani na Rais Samia Suluhu Hassan mstueni bega ageuke nyuma aone kwa macho yake mawili, asikie kwa masikio yake mawili then atumie ile rula ya kupima mabega ya wateule alivyoahidi.

Mkurugenzi huyu amelewa chakari fedha za umma kana kwamba TAKUKURU wako likizo au wanamuogopa. Shule zote za umma Msingi/Sekondary Temeke, madarasa yamekuwa yakijengwa na wakandarasi wazawa kwa gharama ya Shilingi 20milioni kwa darasa moja.

Wakandarasi takriban 8 wazawa kwa miaka minne wamejenga madarasa wilayani humu kwa viwango standard lakini DED amegoma kuwalipa kisa wamegoma "kumhakikishia chochote" akiadhimisha malipo yao. Sasa ni "saga" Kati ya DED na Mchumi na Mamlaka za juu zisipoingilia wawili hawa wanaweza kuuana maana Mchumi amegoma kuchukua rushwa kutoka kwa kandarasi wazawa.

Ili kuonesha kuwa yeye kweli ni DED wa Hayati Magufuli asiyetishwa sasa ameamua kuchukua madarasa yote 116 za wilaya kutoka shule mbalimbali na kumpa kandarasi mmoja nje ya wale "wagumu" na kumpa "mkarimu" kwa sharti la kujenga madarasa hayo kwa Shilingi 23milioni kwa kila darasa. Piga hesabu hizo 3m mara 116. Kweli hela za umma zinachezewa. Hazina mwenyewe.

"Mimi ndiye bosi wa Temeke, kama unadhani Mchumi anaweza kuwalipa, sitoe hela hadi mjifikirie, sitishiki na utawala mpya" anamjibu kandarasi mwenye mkono wa birika.

My Take: Rais SSH, agiza vyombo vyako kumchunguza mabega ya DED huyu. Atakwamisha mwendo kasi uliyoanza nayo. Inawezekana wako wengi wa aina hii. Mbali na kiburi lakini ufisadi wa aina hii ni aibu.

#FreedomIsBack
 
Sawa chawa wa mchumi wamekusikia.
Kandarasi nina swali kwako darasa 1 milioni 20, linakuja na madawati kabisa??

Everyday is Saturday................................:cool:
 
Halmashauri za Bahi,temeke,moshi manispaa,arusha jiji, Geita mji na vijijini, chato,ikungi,meru, chunya, kilosa, Kahama, nyangwale,siha, biharamulo, kibaha,kongwa, mbulu, babati mjini, Tarime, karatu, ilala, wakurugenzi wake na wakuu wa idara ni mchwa.
 
Sawa chawa wa mchumi wamekusikia.
Kandarasi nina swali kwako darasa 1 milioni 20, linakuja na madawati kabisa??

Everyday is Saturday................................:cool:
Linakuja na A.c, ipad kwenye kila desk, self contained na vitanda vya kupumzikia wanafunzi wakichoka kusoma😂
hayo ya milioni 23 yatakuja na madada poa kabisa kwa ajili ya watoto kufanya practical ya topic ya reproduction.
 
Enyi wana wema mliojirani na Rais Samia Suluhu Hassan mstueni bega ageuke nyuma aone kwa macho yake mawili, asikie kwa masikio yake mawili then atumie ile rula ya kupima mabega ya wateule alivyoahidi...
Ulichoandika hapa kinaleta shaka kubwa.

Kwanza hakuna wakandarasi wanaojenga madarasa. Madarasa nchi nzima yanajengwa kwa force account. Pili MD hana mamlaka ya kuchagua fundi, kuna kamati za force account.

Kamati ya ujenzi, kamati ya manunuzi, kamati ya mapokezi. Mambo yote yanafanyika huko kwenye mashule siyo kwa MD/DED. Mi sipo Dsm, sipo Temeke jaribu kufikiri tena namna ya kumshambulia Mwakabibi.
 
Halmashauri za Bahi,temeke,moshi manispaa,arusha jiji, Geita mji na vijijini, chato,ikungi,meru, chunya, kilosa, Kahama, nyangwale,siha, biharamulo, kibaha,kongwa, mbulu, babati mjini, Tarime, karatu, ilala, wakurugenzi wake na wakuu wa idara ni mchwa.
Umejuaje kote huko?
 
Back
Top Bottom