Rais Samia Suluhu Hassan akutana na kufanya mazungumzo na Rais Mstaafu Ally Hassan Mwinyi

Uzalendo wa Kitanzania

JF-Expert Member
Mar 8, 2020
2,192
4,659
Taarifa kamili ya mazungumzo ya Viongozi hao imeambatanishwa hapo chini

Ikulu.jpg

Mny1.jpg
Mny2.jpg


 
Mzee Mwinyi anatakiwa asamehewe bure popote atakapoteleza, kwa umri aliokua nao wazee wengi huwa akili zinaruka kidogo na kurudi utotoni.

Mungu amlinde na amuongoze. Taifa hili wasingekuwepo Mzee Mwinyi na Mzee Mkapa, nchi ingegawanywa na MATAGA katika vikao vyao vya CCM (Wee Bashilu, chukua mkoa wa bukoba utakuwa wako, na wee nanii, nanii, eenh Hapi chukua mkoa wa ilinga utakua shamba lako - Mtaandika maombi ya kuomba hati muyalete ofisini kwa Lukuvi, mimi ndio laisi wa nchi, ntawapa. Nasema ntawapa.)
 
Hamna Mtanzania asiye taka kumuunga mkono Mh Rais, tatizo ni pale anaposhindwa kujipambanunua kuwa alikuwa msaidizi namba moja wa mwendazake. Wakati mwendazake ana chakufuliwa kakaa kimya kama hayuko na hasikii au anafurahia kimoyomoyo?! Ukweli ni kuwa Magufuli hawezi kuchafuliwa na walio tumikia naye wakafikiri watabaki salama.

Spika anaona atabaki salama kwa kusema mwendazake alishauriwa vibaya ana sahau anayo skandali ya mabilioni ya matibabu ambayo ilikuwa ina hang somewhere ni suala la muda tu.

Wakimaliza hii biashara yao kichaa ya kumpaka oil chafu mwendazake watamgeukia hili halihitaji akili kubwa kulijua. Alishauriwa na nani zaidi ya nyie mlio kuwa mnamzunguka na kufanyakazi pamoja naye?

Mbona Judge Mkuu hatumsikii akiendekeza haya mambo ya kusikitisha na kutahayarisha yanayo endelea kwa sasa hapa Tanzania. Huyu amekuwa kiongozi mweledi siku zote. Hotuba aliyoitoa siku ya maziko pale Chato ni kielelezo tosha cha kiongozi mwenye hekima.

Wazee wamshauri huyu ahamie mhimili wa Excutive ifikapo 2025 atawafaa sana Watanzania/Tanganyika.
 
Back
Top Bottom