Naanto Mushi
JF-Expert Member
- Oct 16, 2015
- 6,236
- 15,602
Binafsi nilikuwa na mashaka na namna atavolimiliki jukwaa mbele ya viongozi wabobezi na malegandary wa siasa za kusini mwa Afrika. Ila ukweli kabisa nimeridhika, kwa hotuba ya leo nampa maksi 97% hizo maksi 3% nilizomnyima ni makosa madogo madogo ambayo nadhani yanachangiwa na ugeni na ukifananisha pia kwamba amekula kiapo cha urais siku tano zilizopita, ila kwa ujumla ametoa hotuba ambayo naweza sema kwa ubora imewazidi watangulizi wake na kupitia hotuba hii, nimenusa kwa mbali mwelekeo wa itikadi wa serikali ya Madam President na nimeridhika kwamba utaweza kufanikiwa sana kwenye baadhi ya maeneo ambayo utawala wa Hayati JPM uliboronga.
Kwa ufupi, mambo makubwa niliyoyaona kutoka kwenye hotuba ya leo ni haya
1. Uhusiano na nchi majirani - Haukua mzuri, na hususani uhusiano na jirani yetu Kenya ambaye tuna muingiliano mkubwa sana wa kibiashara na kijamii kuliko majirani wetu wote. Ila kwa namna ya namna alivotoa hotuba yake, nna imani sana kwamba ataboresha na kuponya haya mahusiano na majirani. Na sio Kenya tu, hata wale ambao walibatizwa kwamba ni 'mebeberu' nadhani Madam President ni kama amefungua mkono kupitia hotuba yake kitu ambacho ni kizuri.
2. Umoja wa kitaifa - amegusia pia kwenye hotuba yake na nadhani ni jambo jema, maana taifa tulishafika mahali pabaya sana
3. Moyo wa kuendeleza yale mazuri ya mtangulizi wake Hayati JPM - Hapa pia nimefurahi kuona kwamba amerithi mtizamo wa JPM kuhusu kuendeleza miundo mbinu, Hili ni jambo bora pia, kwa sababu naamini kwamba Magufuli kuna mahali alifanya vizuri na panastahili kuendelezwa, na nimefurahi kwa yeye kututhibitishia hilo.
4. Kusikiliza ushauri wa viongozi waliomtangulia - hii point nyngine ambayo naona imempa credit kubwa sana, maana technically viongozi waliopita wanaifahamu hii nchi vema na sio mbaya kuchukua ushauri kwao, japokuwa ninaamini itabidi kwanza awe ana mtizamo wake kwanza kabla ya kupokea ushauri ili asiingie kwenye hatari ya kuonekana ni kiongozi asiyeamua kwa akili yake.
Binafsi haya ni machache niliyoona kwenye hotuba ya leo, na kwa kweli nimeyafurahia kwa Madam President, na hili ni angalizo natoa. Madam President anaweza kufanya wonders kama atasimamia alichohutubia leo, na niseme tu wazi, anaweza kutawala mpaka 2030!...
Kwa hotuba ya leo, hata wale waliokuwa wanapiga ramli za ndoto za urais 2025, watakuwa wamaogopa sana. Angalia body language ya Mwinyi wakati Madam President anamaliza hotuba yake, hakika utaona kabisa ametiwa uwoga fulani. Ni kama leo viongozi wengi hawakutegemea kama Madam President angetoa speech ambayo ipo authoritative kiasi hicho.
Cha mwisho ni kumshauri tu, aache mara moja kuinamisha kichwa kwa heshima, Rais unatakiwa u express Authority kila dakika, so sijapendezwa na akisalimiwa kila saa anainamisha kichwa, awe straight kila saa hata akisalimiwa.
Nawasilisha
N.Mushi
Kwa ufupi, mambo makubwa niliyoyaona kutoka kwenye hotuba ya leo ni haya
1. Uhusiano na nchi majirani - Haukua mzuri, na hususani uhusiano na jirani yetu Kenya ambaye tuna muingiliano mkubwa sana wa kibiashara na kijamii kuliko majirani wetu wote. Ila kwa namna ya namna alivotoa hotuba yake, nna imani sana kwamba ataboresha na kuponya haya mahusiano na majirani. Na sio Kenya tu, hata wale ambao walibatizwa kwamba ni 'mebeberu' nadhani Madam President ni kama amefungua mkono kupitia hotuba yake kitu ambacho ni kizuri.
2. Umoja wa kitaifa - amegusia pia kwenye hotuba yake na nadhani ni jambo jema, maana taifa tulishafika mahali pabaya sana
3. Moyo wa kuendeleza yale mazuri ya mtangulizi wake Hayati JPM - Hapa pia nimefurahi kuona kwamba amerithi mtizamo wa JPM kuhusu kuendeleza miundo mbinu, Hili ni jambo bora pia, kwa sababu naamini kwamba Magufuli kuna mahali alifanya vizuri na panastahili kuendelezwa, na nimefurahi kwa yeye kututhibitishia hilo.
4. Kusikiliza ushauri wa viongozi waliomtangulia - hii point nyngine ambayo naona imempa credit kubwa sana, maana technically viongozi waliopita wanaifahamu hii nchi vema na sio mbaya kuchukua ushauri kwao, japokuwa ninaamini itabidi kwanza awe ana mtizamo wake kwanza kabla ya kupokea ushauri ili asiingie kwenye hatari ya kuonekana ni kiongozi asiyeamua kwa akili yake.
Binafsi haya ni machache niliyoona kwenye hotuba ya leo, na kwa kweli nimeyafurahia kwa Madam President, na hili ni angalizo natoa. Madam President anaweza kufanya wonders kama atasimamia alichohutubia leo, na niseme tu wazi, anaweza kutawala mpaka 2030!...
Kwa hotuba ya leo, hata wale waliokuwa wanapiga ramli za ndoto za urais 2025, watakuwa wamaogopa sana. Angalia body language ya Mwinyi wakati Madam President anamaliza hotuba yake, hakika utaona kabisa ametiwa uwoga fulani. Ni kama leo viongozi wengi hawakutegemea kama Madam President angetoa speech ambayo ipo authoritative kiasi hicho.
Cha mwisho ni kumshauri tu, aache mara moja kuinamisha kichwa kwa heshima, Rais unatakiwa u express Authority kila dakika, so sijapendezwa na akisalimiwa kila saa anainamisha kichwa, awe straight kila saa hata akisalimiwa.
Nawasilisha
N.Mushi