Rais Samia Suluhu alazimika kufuta post yake ya Twitter aliyotoa taarifa ya kuwasili Dar. Ni baada ya malalamiko kuhusu mabando kuzidi kwa wachangiaji

G Sam

JF-Expert Member
Apr 20, 2013
11,555
35,880
Makabwela ambao wametoa malalamiko lukuki ya malipo ya bando jipya wamemlazimisha Rais Samia Suluhu kufutilia mbali post yake ya Twitter aliyoitoa ambapo alitoa taarifa rasmi ya kuwasili Dar leo.

Hii inakuwa post yake ya kwanza kuifutilia mbali tangia awe Rais rasmi wa Jamhuri ya muungano ambapo wengi wa wachangiaji wake wamemuomba kutengua uteuzi wa waziri wa teknolojia ya habari ndugu Faustine Ndugulile na mkurugenzi mkuu wa TCRA kutokana na kutokuchukulia maanani uzito wa malalamiko yao kuhusu malipo ya bando la mitandao yote ya mawasiliano nchini.

Tusubiri tuone!
 
Bongo raha sanaaaa

Screenshot_20210403-191342.jpg

Sihami bongo haki
 
Ile akaunti sijaielewa kabisa...hao wanaoiendesha wapunguze ushamba kidogo

Akaunti ya Mkuu wa Nchi huwa haipost mambo hovyo hovyo....wafuatilie akaunti za viongozi wenzake wajifunze mambo yalivyo

Au hata kwa Mtangulizi wake Hayati JPM..

May be anayeiendesha ile akaunti ya Mama yetu Rais inawezekana mwanamke mwenzie..... kwa sababu wanawake kwa vijipost post hawajambo wanadhani bado ni VP......

Kiufupi yule tayari ni Mkuu wa Nchi..Dunia nzima inamfuatilia 24hrs
 
Kwa akili zako unaamini wote walio mchukia mtukufu wako hayati walikuwq ni Bavicha! Watumishi wa umma wote walio dhulumiwa haki zao ni Bavicha, Wastaafu wanaodai mafao yao ni Bavicha, wale wakukima wa korosho walio sumbuliwa kipindi kile mi Bavicha!

ok!! Basi sawa.
Hao ni 2% tu ya raia wote hapa nchini.

Hakuna mtu anapendwa na kuchukiwa na wote, hakuna duniani.

Kama unabisha nioneshe mmoja wapo?

Kwenye familia yako tu mitoto yako kuna baadhi haikuopendi sembuse nchi ya watu milioni 60?

Hata Rais wangu Samia hawezi kuingia kwenye mtego wa kijinga kwamba eti atapendwa na kila mtu
 
Back
Top Bottom