Rais Samia Suluhu akifanya kosa hili uongozi wake utakua mgumu sana

Kulingana na katiba ya JMT(1977) inaelekeza kuwa ikitokea Rais aliepo madarakani akapatwa na tatizo ambalo litamfanya kua nje ya ofisi ikiwepo na kifo basi Makamu ataapishwa kua Rais wa JMT.

Hapa basi nafasi ya makamu itakua wazi na kwa taratibu Pia katiba inamuelekeza Rais achague Makamu wake HAPA NDIPO LENGO LANGU LIPO.

Mama Samia ijulikane anachukua majukumu makubwa ya kuongoza nchi tena ambayo haijawahi kuongozwa na Mwanamke.

Kitu ambacho Mheshimiwa Rais anatakiwa afikiri zaidi ni kuhusu makamu wake akifanya kosa hapo nahisi ataona miaka4 kama10,anatakiwa achague mtu ambae ndani ya chama ana influence pia anakubalika na wazee wa chama, hapo atakua anapumua vizuri na atakua na mzigo mmoja tu wa upinzani ila akichagua ambae hakubaliki ndani ya chama ajiandae kupata wakati mgumu kwenye chama pia kutoka kwa upinzani kwa sababu upinzani wenyewe ni known hata kama akifanya hivi watakosoa tu hio ndio kazi yao.

Kwa hio Mheshimiwa akipuyanga hapa kwisha habari yake°

#ALUTA CONTINUA
Muna maneno mengi mno.Yaani hadi leo ukifuattilia kila mtu alilomwambia yaani utafikiri Rais hana akili kabisaaaa.Duuuh nyie ndo mlikuwaga wasumbufu kwa Mamonita darasani nyie aaaàah.

Sent from my Infinix X627 using JamiiForums mobile app
 
Unamaanisha Prof. Manya? Hana influence kwenye chama, lakini ana uwezo mkubwa na ana utulivu mkubwa wa akili, siyo kama Kabudi.

Geologist Manya, akiwa Makamu wa Rais, nina hakika ataendana vizuri Mama Samia.

Samia asifanye kosa kumteua Makamu wa Rais, ambaye kwa namna fulani anajiona au walikuwa wanalingana kimadaraka au alijiona ni mtu wa karibu sana kwa Rais. Lazima ampate mtu ambaye atakuwa na utii kwake wa dhamira, na siyo unafiki.
Huyo atakuwa Wzr wa MDN
 
Anachagua makamu wake mtu ambae watasaidiana majukumu ya kujenga nchi na kuifikisha

nchi sehemu tunayotamani,maswala ya kumshauri achague mtu anaekubalika na wazee wa chama

mtu anaekubalika ndani ya CCM,na sababu zingne za namna hiyo ni Makosa ambayo naamini MAMA akiyafanya

atakuja jutia,Hachagui Katibu wa CCM wala hachagui Mjumbe wa CCM anachagua Makamu wake anae fit ktk hiyo nafasi

kiutendaji na wala si Mtu wa kupendwa na wana CCM,hii mambo ya kufanya vitu ili upendwe ndio yale yaleee kurudishana

Misri.Mimi natamani kuona MAMA ana select kichwa moja ya MOTO sana ambayo huko CCM wanamuogopa ila wanamuheshimu

Mama akisema tu achague mtu ili wazee wa ccm wafurahi,Kabugi na Yatamshinda,Hii nchi ukitaka iende usiipeleke ki ccm ccm sana.

#maamuzimagumuyanahitajikaeneohili
 
Hata Suleimani ali abudu miungu ya wake na masuria 1000 na kuitengeneza madhabahu. Na bado kwa kupitia Daudi Baba yake Yesu alitwa mwana Wadaudi. Itoshe tu kuwa JPM alimkiri Bwana Yesu na Mungu wa Mbinguni hadharani na ulimwengu wote ukalishuhudia hilo.
Ukristo ni imani yako na yangu. JPM anaongoza hadi waabudu ng'ombe na wanalipa kodi na kuajiri. Nchi inaongozwa na sheria. Ushawahi sikia mahakama inahukumu mhalifu kwa kutumia kifungu cha biblia? Embu tuachane na hii discussion tu.
 
Ukristo ni imani yako na yangu. JPM anaongoza hadi waabudu ng'ombe na wanalipa kodi na kuajiri. Nchi inaongozwa na sheria. Ushawahi sikia mahakama inahukumu mhalifu kwa kutumia kifungu cha biblia? Embu tuachane na hii discussion tu.

Kwani hayo maamuzi mengine yalifanyika kimahakama ama kwa mamlaka ya Urais wake? Unafikiri sheria imeandika kila kilicho na kufanywa katika mamlaka ya Taasisi ya Urais! Mamlaka wa Urais ina mpaka watu wanaojipendekeza kwake na mambo yao yalitekelezwa na kufanyiwa kazi mengine yakawa ni yamanufaa mengine maumivu.

Hata Bwana Yesu, Emanuel Mungu pamoja nasi wanadamu aliongoza na kuwahubiria hao ulio wataja. Hakuna jipya hapa.
 
Kwani hayo maamuzi mengine yalifanyika kimahakama ama kwa mamlaka ya Urais wake? Unafikiri sheria imeandika kila kilicho na kufanywa katika mamlaka ya Taasisi ya Urais! Mamlaka wa Urais ina mpaka watu wanaojipendekeza kwake na mambo yao yalitekelezwa na kufanyiwa kazi mengine yakawa ni yamanufaa mengine maumivu.
Maamuzi ya nchi yanatakiwa yafanyike kwa kufuata sheria na katiba na si jambo lingine lolote. Kama linalotakiwa kufanyiwa maamuzi halipo ktk sheria au lina ukakasi mswada unapelekwa bungeni kwa wawakilishi wa wananchi.
 
Maamuzi ya nchi yanatakiwa yafanyike kwa kufuata sheria na katiba na si jambo lingine lolote. Kama linalotakiwa kufanyiwa maamuzi halipo ktk sheria au lina ukakasi mswada unapelekwa bungeni kwa wawakilishi wa wananchi.

Endelea kujidanganya hitatokea hiyo mpaka kiama.
 
Tego ni hili.., kama ana mpango wa kurudi 2025 atahitaji achague VP ambaye anahisi ata mu overshadow ....yaaani asitembelee kivuli chake ili yeye apige kazi aonekane zaidi,,,,na atakayechaguliwa trust me atakuja na haiba ya kikazi ya JPM ili ajenge legacy na mazingirira aminishwa ya 2025....yaani miaka hii minne ni training ground battle.

sasa either atampendekeza wa hivi hivi tu au chama kitataka mtu wa majaribio ili waone kama 2025 atawafaa ingawa sio utamaduni na haijawahi kutokea makamu akawa rais ila mambo hubadilika
 
Endelea kujidanganya hitatokea hiyo mpaka kiama.
Viongozi waliopita wamejitahidi kufuata katiba na sheria japo kuna changamoto nyingi katika uongozi. Walifanya vizuri na TZ bado ipo salama mpaka sasa. Hayo mengine yote ni porojo.
 
Viongozi waliopita wamejitahidi kufuata katiba na sheria japo kuna changamoto nyingi katika uongozi. Walifanya vizuri na TZ bado ipo salama mpaka sasa. Hayo mengine yote ni porojo.

Wale Majizi na Mafisadi na Waliochezea nchi hii kwaa kuingia mikataba bofu bofu ambao Marehemu JPM aka "Mmachinga One" hakusita kuwasema najukwaani aliwalenga kina nani?
 
Lukuvi HAFAI, angalia clip zake hivi karibuni akiwa Mwanza kwenye migogoro ya ardhi.Hasikilizi watu na anajitia mjuaji sana wakati ni zero brain! Elimu yake pia imejaa ujanja ujanja.
Mama Samia msimpangie yeye anajua wa kufanya naye kazi. VP asiwe hawa vijana wenye tamaa ya Urais.
 
Wale Majizi na Mafisadi na Waliochezea nchi hii kwaa kuingia mikataba bofu bofu ambao Marehemu JPM aka "Mmachinga One" hakusita kuwasema najukwaani aliwalenga kina nani?
Hii hoja yako ingekuwa na nguvu kama hao watu wangekuwa wamepelekwa mahakamani, kinyume na hapo naweza sema ni siasa tu. JPM ni mwanasiasa pia.
 
Hii hoja yako ingekuwa na nguvu kama hao watu wangekuwa wamepelekwa mahakamani, kinyume na hapo naweza sema ni siasa tu. JPM ni mwanasiasa pia.

Haina nguvu kwako ila ina nguvu na kunufaisha wengi ambao kiasi cha fedha zilizokuwa zimekwapulia na mafisadi zilirudidhwa na kutumika kuhudumia jamii. Ikiwemo barabara ambazo unasave fedha zako kwa kukuongezea muda wa kubadilisha shock absobers za gari lako.
 
Haina nguvu kwako ila ina nguvu na kunufaisha wengi ambao kiasi cha fedha zilizokuwa zimekwapulia na mafisadi zilirudidhwa na kutumika kuhudumia jamii. Ikiwemo barabara ambazo unasave fedha zako kwa kukuongezea muda wa kubadilisha shock absobers za gari lako.
Barabara zinajengwa kwa mujibu wa sheria.

Unajua porojo ni maneno yasiyo na ushahidi. Unasikia sikia tu kutoka vyanzo visivyo rasmi halafu unayaendeleza na kuyatumia kwenye hoja zako.

Embu nijibu hili swali:

Kiasi gani kilifisadiwa na kiasi gani kikarudishwa na zilirudi kwa utaratibu upi?
 
Barabara zinajengwa kwa mujibu wa sheria.

Unajua porojo ni maneno yasiyo na ushahidi. Unasikia sikia tu kutoka vyanzo visivyo rasmi halafu unayaendeleza na kuyatumia kwenye hoja zako.

Embu nijibu hili swali:

Kiasi gani kilifisadiwa na kiasi gani kikarudishwa na zilirudi kwa utaratibu upi?

Vilifanyika kwa usiri na tulichona ni matokeo ya miundo mbinu. Daraja halifichwi mfukoni kwa mfano.
 
Kulingana na katiba ya JMT(1977) inaelekeza kuwa ikitokea Rais aliepo madarakani akapatwa na tatizo ambalo litamfanya kua nje ya ofisi ikiwepo na kifo basi Makamu ataapishwa kua Rais wa JMT.

Hapa basi nafasi ya makamu itakua wazi na kwa taratibu Pia katiba inamuelekeza Rais achague Makamu wake HAPA NDIPO LENGO LANGU LIPO.

Mama Samia ijulikane anachukua majukumu makubwa ya kuongoza nchi tena ambayo haijawahi kuongozwa na Mwanamke.

Kitu ambacho Mheshimiwa Rais anatakiwa afikiri zaidi ni kuhusu makamu wake akifanya kosa hapo nahisi ataona miaka4 kama10,anatakiwa achague mtu ambae ndani ya chama ana influence pia anakubalika na wazee wa chama, hapo atakua anapumua vizuri na atakua na mzigo mmoja tu wa upinzani ila akichagua ambae hakubaliki ndani ya chama ajiandae kupata wakati mgumu kwenye chama pia kutoka kwa upinzani kwa sababu upinzani wenyewe ni known hata kama akifanya hivi watakosoa tu hio ndio kazi yao.

Kwa hio Mheshimiwa akipuyanga hapa kwisha habari yake°

#ALUTA CONTINUA
Muafaka wa kitaifa ni muhimu kama ilivyo huko Zenji, hivyo Lissu Antipas Tundu anahusika sana na nafasi hii.
 
Back
Top Bottom