Nyendo
JF-Expert Member
- Jun 4, 2017
- 1,191
- 4,104
Rais Samia Suluhu ameiagiza Wizara ya Habari kuvifungulia vyombo vya habari vilivyofungiwa, na kuhakikisha vinafuata sheria. Aidha, ameagiza sheria kanuni na adhabu ziwe wazi, ifahamike kosa fulani adhabu yake ni fulani, ili isionekane kuwa serikali inaminya uhuru wa habari.
Rais Samia amesema haya...
Wizara ya habari, mnapaswa kusimamia vyombo vya habari, nasikia kuna vyombo vya habari mmevifungia, vifungulieni lakini vifuate sheria na kanuni. Tusiwape mdomo mdomo wa kusema tunabinya uhuru wa habari na nataka kanuni ziwe wazi. Tusifungie tu kibabe
Rais Samia amesema haya...
Wizara ya habari, mnapaswa kusimamia vyombo vya habari, nasikia kuna vyombo vya habari mmevifungia, vifungulieni lakini vifuate sheria na kanuni. Tusiwape mdomo mdomo wa kusema tunabinya uhuru wa habari na nataka kanuni ziwe wazi. Tusifungie tu kibabe