System failure again.Kuna tetesi na minong'ono huko kwenye korido za wachoraji katuni kuwa ifikapo 2025 watashiriki kampeni ya kutoiunga mkono CCM hasa nafasi ya Urais kwa sababu ya madhila makubwa wanayoyapitia chini ya serikali ya awamu ya 6
Baada ya kumkamata msanii Opptitus John Fwema, polisi wameendelea na kamata kamata ya kimya kimya kwani hivi jana usiku wamemkamata mchoraji wa tattoo aitwaye Ronny. Yupo kituo cha polisi Kawe wakimhusisha na kundi linaloikosoa serikali.
Wasanii wachoraji Vibonzo wanaelewa namna wanavyowindwa na wameamua kujipanga kuachana na kuiunga mkono CCM 2025.
Kwa taarifa kutoka kwa wakili ws Opptertus, tayari ameshapata dhamana leo mahakama ya Kinondoni.
Hivyo, badala ya amri za kuwakamata na kuwaminya kimya kimya, itakuwa busara kuharamisha uchoraji wa katuni za kisiasa.
Uzi tayariView attachment 1968090