Rais Samia: Sipendi kubadili viongozi mara kwa mara lakini nalazimika kukwepa fedheha

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Apr 18, 2017
2,797
11,959
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan akifungua Mkutano wa Faragha (Retreat) wa Mawaziri, Naibu Mawaziri, Makatibu Wakuu na Naibu Makatibu Wakuu katika Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa Arusha (AICC) jijini Arusha leo tarehe 02 Machi, 2023




Samiaa.jpg

RAIS SAMIA
“Kutofanyika kwa mikutano yenye lengo la kutoa maelekezo ya kiuongozi kumesababisha athari katika utendaji kazi wa Serikalini.

“Hii ni moja ya sababu ya kubadilishwa kwa viongozi mara kwa mara ili kuiepusha Serikali na fedheha ya kuwa na viongozi wanazifanya Wizara kuwa sehemu za marumbano na migawanyiko isiyo na tija.

“Nafahamu madhara ya kubadilisha viongozi mara kwa mara na huwa sipendi kufanya hivyo kwa kuwa kunawafanya watu wafanye kazi kwa hofu na viongozi kutokuwa na mipango ya muda mrefu kwa kuhofia teuzi zao kutenguliwa.

“Kiongozi anapoondoshwa kazini ni fedheha kwa familia yake, watoto na vijana ambao walikuwa wanamuona kama mtu wa mfano, kwangu pia si lengo langu kubadilisha viongozi kwa kuwa inachukua muda mrefu kuwajenga lakini wakati mwingine nafanya hivyo kuepusha madhara Serikalini na kwa Wananchi.”
 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan akifungua Mkutano wa Faragha (Retreat) wa Mawaziri, Naibu Mawaziri, Makatibu Wakuu na Naibu Makatibu Wakuu katika Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa Arusha (AICC) jijini Arusha leo tarehe 02 Machi, 2023



Yote ni kupoteza muda, hapo wapo miili tu, lakini kwenye roho zao, in the innermost chambers of their hearts, wamepata nafasi ya kujinufaisha wao na wanaowazunguka wa karibu nao...ndugu zao! Hiyo yote ni kupoteza fedha za umma
 
Justfication ya kutumbua pesa za walipa kodi,hapo perdiem ni zaidi ya mshahara wa mwalimu,kiufupi hatuna rais mwenye maono ila mtumbuaji wa kodi za wananchi.
 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan akifungua Mkutano wa Faragha (Retreat) wa Mawaziri, Naibu Mawaziri, Makatibu Wakuu na Naibu Makatibu Wakuu katika Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa Arusha (AICC) jijini Arusha leo tarehe 02 Machi, 2023



Hebu zuumu vizuri hiyo nguo ya kijani na nyeusi kushoto, sidhani hilo buumu ni la mchina naona kama urijino.
 
Justfication ya kutumbua pesa za walipa kodi,hapo perdiem ni zaidi ya mshahara wa mwalimu,kiufupi hatuna rais mwenye maono ila mtumbuaji wa kodi za wananchi.
Huu mtindo ulifanywa na Kikwete pia ila yeye aliwapeleka kwenye hoteli ya kitalii iliyonona kuliko zote.
 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan akifungua Mkutano wa Faragha (Retreat) wa Mawaziri, Naibu Mawaziri, Makatibu Wakuu na Naibu Makatibu Wakuu katika Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa Arusha (AICC) jijini Arusha leo tarehe 02 Machi, 2023





RAIS SAMIA
“Kutofanyika kwa mikutano yenye lengo la kutoa maelekezo ya kiuongozi kumesababisha athari katika utendaji kazi wa Serikalini.

“Hii ni moja ya sababu ya kubadilishwa kwa viongozi mara kwa mara ili kuiepusha Serikali na fedheha ya kuwa na viongozi wanazifanya Wizara kuwa sehemu za marumbano na migawanyiko isiyo na tija.

“Nafahamu madhara ya kubadilisha viongozi mara kwa mara na huwa sipendi kufanya hivyo kwa kuwa kunawafanya watu wafanye kazi kwa hofu na viongozi kutokuwa na mipango ya muda mrefu kwa kuhofia teuzi zao kutenguliwa.

“Kiongozi anapoondoshwa kazini ni fedheha kwa familia yake, watoto na vijana ambao walikuwa wanamuona kama mtu wa mfano, kwangu pia si lengo langu kubadilisha viongozi kwa kuwa inachukua muda mrefu kuwajenga lakini wakati mwingine nafanya hivyo kuepusha madhara Serikalini na kwa Wananchi.”

Ameongeza ukweli lakini Kwa nini Chuo Cha diplomasia Kurasini au Uongozi Institute au Kile Cha Kibaha visiwe vyuo vya kuwafundisha viongozi maadili mara Kwa mara badala ya kuitana huku kwenye kumbi na hoteli?

Utaratibu huu usiwe unaishia Kwa viongozi wa Juu pekee ufike Hadi Kwa viongozi ngazi ya Wilaya.
 
Kwa namna hizi Seminar zinavyofanyika kwa kasi awamu hii, kweli hela kupitia biashara ya hotel na Lodges lazima ilipe.

Imagine una Lodge ya vyumba kama 20 hivi vya 30,000 hadi 35,000 hujawalaza Madereva na Wasaidizi wote kweli?

Kweli Mama Anafungua Nchi 🥂
 
Huu mtindo ulifanywa na Kikwete pia ila yeye aliwapeleka kwenye hoteli ya kitalii iliyonona kuliko zote.
Watumie utaratibu wa vyuo badala ya hoteli na kumbi

Chuo Cha Diplomasia
Uongozi Institute,
ESSAMI,
Chuo Cha CCM Kibaha(kitolewe Kwa Umma)
 
Mama usisite kuwatimua pindi wanapoboronga, laa sivyo tutaambulia mabua.

Lakini usimuonee mtu.
 
Back
Top Bottom