inamankusweke
JF-Expert Member
- Apr 24, 2014
- 17,955
- 18,217
Kama ilivyo kwa mgombea urais ccm hachaguliwi na chama Bali Dola ndivyo ilivyo kwa mgombea mwenza hachaguliwi na mgombea Bali dolaNikusahihishe, karibu yote uliyoyasema ni ya kweli.
Isipokuwa Magufuli hakumchagua Samia, 2015 katika kikao cha CCM cha kumchagua mpeperusha bendera, Kikwete alikuja na jina la Magufuli mfukoni, na alipopitishwa . Naye Magufuli akamtaka Hussein Mwinyi awe mgombea wake mwenza, Kikwete akasema hebu tumpe Katibu mkuu wa chama fursa ya mawazo yake, Ndipo Comrade Abdulrahman kinana alipolileta jina la Mama Samia Suluh na kusema ni kiongozi bora kutoka kisiwani, na ni wakati muafaka kuwa na Mgombea mwenza wa kike.
Katika uchaguzi wa 2020 Magufuli alitaka kumbadilisha lakini akashauriwa kuwa akifanya hivyo kitakigharimu chama vibaya sana na Dunia itamshangaa.