Patriot
JF-Expert Member
- Feb 11, 2008
- 5,698
- 4,693
Anachokifanya Rais Samia ni kuharibu amani ya nchi hii. Tumeishi bila ukabila lakini polepole tunarudishwa kwenye mtafaruku bila sababu. Tunalazimisha kutambua machifu bila sababu.
Yaani viongozi wa kiukoo, kikabila Watu hawa wanastahili kuachiwa kabisa nje ya mfumo kama ambavyo imekuwa miaka yote ya uhuru. Kuna nini hadi Rais anawatafute kwa nguvu zote hizo?
Museveni aliwadekeza Baganda, matokeo yake hadi leo ndani ya Kampala anaonekana ni mpangaji asiyetakiwa. Kule Kasese mwaka 2016 hadi mauaji yalitokea kwa sababu ya kudekezwa. Hatuhitaji tawala za kichifu/kikoo ktk nchi hii.
Yaani viongozi wa kiukoo, kikabila Watu hawa wanastahili kuachiwa kabisa nje ya mfumo kama ambavyo imekuwa miaka yote ya uhuru. Kuna nini hadi Rais anawatafute kwa nguvu zote hizo?
Museveni aliwadekeza Baganda, matokeo yake hadi leo ndani ya Kampala anaonekana ni mpangaji asiyetakiwa. Kule Kasese mwaka 2016 hadi mauaji yalitokea kwa sababu ya kudekezwa. Hatuhitaji tawala za kichifu/kikoo ktk nchi hii.