Rais Samia: Rais haruhusiwi kukaa mkoa mmoja kwa zaidi ya siku tatu

Paukwaa Pakawaaa!
Hapo zamani za kale kuna mtawala mmoja wa Tanzania alikuwa matata na Hamnazo kweli kweli! Mara nyingi alikuwa anakaa na kufanya kazi za kiserikali nyumbani kwao kule ndani ndani kulee kwa zaidi ya miezi kadhaa bila kujali hili wala lile...

Kwa ushamba wa asili; Hamnazo aliwaapisha watendaji wake na kuwapokea wageni mashuhuri kwenye mazingira ya kienyeji enyeji sana kule kwao! Alikuwa mjivuni na mdhalilishaji! Alipenda showoffs na media attentions. Alipenda yeye tu ndo aonekane akiwa fontipeji! Kila uzinduzi yeye! Mabango barabarani yeye peke yake!

Alitamani wananchi wawe wanyonge wa kudumu.
Watendaji wake walijifanya kumkubali. Wapo wafuasi waliojua udhaifu wake wa kupenda kuabudiwa. Mithili ya sinema za kijambazi; wafuasi wa Hamnazo walipora mali, waliua na kunyanyasa wote waliokuwa na mawazo mbadala.

Licha ya ulinzi wa kutosha aliojiwekea (unaoonekana na usioonekana) Hamnazo alifanikiwa kwenda zake kuzimu. Wengi walijitokeza kutaka kujiridhisha kama kweli Hamnazo kaenda zake. Maelezo yakawa mengi tofauti tofauti! Kwa kipindi kama mwezi hivi pengine zaidi baada ya shujaa Hamnazo kwenda zake kuzimu wafuasi wake bado hawakuamini kama kweli yule mtawala matata; shujaa wao angelienda zake kirahisi vile. Lakini ndo hivyo ilivyokuwa. Cha ajabu kuanzia aende zake hakuna tena aliyetaka kufuata nyendo zake ovu!
Hamnazo alisahaulika mapema sana.
Baada ya kuona hata mzimu wake nao haukuwa na jipya basi wateule wake wengi walipata mwanya wa kujivua u-hamnazo, kutua misalaba yao na kutema nyongo huku wakikiri wazi wazi kwamba Tanzania ilielekezwa njia ya kuzimu na yule mtukufu Hamnazo, shujaa wao.
Hadithi yangu imeishia hapo.

FUNDISHO: Tujenge taasisi imara na si miungu-watu. Akina Hamnazo hawajaisha! Asanteni
Da! mkuu mbona unachafua hali ya hewa kiasi hiki. Wacha niende zangu alafu nirudi tutaelewana tu humu ndani
 
Acheni kumchuria Nyerere. Nyerere ni kusikia jina lake tu?

Nani unalinganisha na Nyerere wewe? Huyu anayerukwa kimanga na wateule wake, kina Gambo?

Nyerere akae nyumbani wapi?

Nyumba hizi alizojengewa na JWTZ baada mno ya kustaafu?
Kama hujui bora unyamaze. Mwalimu Nyerere alikaa kwenye nyumba yake Msasani muda mwingi wa uraisi wake.
 
Alimuacha huku akiwaasa wanaadam kwamba huo ndo mtihani aliowapa aidha wamfuate ibilisi ama Mungu.

daily news july1-august 31,1977 page 5,monday, august 1,1977.jpg
 
Kama aliyosema mama leo ndiyo ukweli wenyewe basi pongezi sana mama Samia kwa kuzingatia maadili, taratibu na sheria.
Jambo jema ila siku ikatokea akakaa sehemu zaidi ya siku hizo asisahau kusema sababu ya kuzidisha siku, turejee ya wale wanasiasa wawili, mmoja alisema mwaka 2015 kama sijakosea sana "Kama uchaguzi utakuwa huru na wa haki, basi CCM ijiandae kuachia Ikulu" mwingine akasema "nafasi niliyopewa ni kubwa sana nikipewa nyingine sitokubali kabisa". na wote wawili walikula viapo
 
Na nyumba hiyo alijenga kwa mkopo toka serikalini

..niliwahi kusikia toka kwa watu wa serikali kwamba nyumba ya mwalimu ya msasani ilichukuliwa na serikali kabla mwalimu hajamaliza kulipa mkopo.
 
..niliwahi kusikia toka kwa watu wa serikali kwamba nyumba ya mwalimu ya msasani ilichukuliwa na serikali kabla mwalimu hajamaliza kulipa mkopo.
Kuna video yeye Mwenyewe Mwl Nyerere alisema alishindwa kulipa deni akaamua kuirudisha nyumba serikalini, lakini baadaye serikali ikamsamehe deni lake
 
Dodoma kuna Ikulu, Dar kuna Ikulu
Mikoa yote ina ikulu mkuu, Na Rais kama Mkuu wa Nchi anaweza kutekeleza Majukumu yake popote pale ndani ya nchi, Hapo hao watu wa Mwanza wamenangwa,

Sababu za Rais kutokukaa sehemu kwa Zaidi ya Siku tatu nje ya Ofisi zake labda ziwe kiusalama tu mana hio Area inakuwa haiko well protected on daily basis kama state house Chamwino ambapo measures nyingi ziko imposed na restrictions kwa vitu kama Anga tayari vinakuwa placed
 
Mikoa yote ina ikulu mkuu, Na Rais kama Mkuu wa Nchi anaweza kutekeleza Majukumu yake popote pale ndani ya nchi, Hapo hao watu wa Mwanza wamenangwa,

Sababu za Rais kutokukaa sehemu kwa Zaidi ya Siku tatu nje ya Ofisi zake labda ziwe kiusalama tu mana hio Area inakuwa haiko well protected on daily basis kama state house Chamwino ambapo measures nyingi ziko imposed na restrictions kwa vitu kama Anga tayari vinakuwa placed

Ulipata wasaa wa kumsikiliza au umeona uandike mawazo yako tu?
 
Back
Top Bottom