Roving Journalist
JF Roving Journalist
- Apr 18, 2017
- 2,807
- 11,969
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwaapisha Majaji 6 na Mwenyekiti wa Baraza la Maadili leo Mei 23, 2023, Ikulu ya Chamwino mkoani Dodoma.
Walioapishwa ni;
A. Majaji
Mhe. Jaji (MST) Rose Aggrey Teemba, Kuwa Mwenyekiti wa Baraza la Maadili.
Jaji Mkuu wa Tanzania Prof. Ibrahim Hamisi Juma amemshukuru Rais kwa kuongeza idadi ya Majaji wa Mahakama ya Rufani ambapo aliwakuta wapo chini ya 16 na sasa wamefika 31.
Majaji hawa 6 walioongezwa watasaidia kuboresha ufanisi wa Mahakama ya Rufani kutoka vikao 7 hadi 9 na kupunguza mzigo kwa kila jopo la Majaji.
Amesema kwa sasa kuna zaidi ya mashauri 200 yanayohusu fedha za kibenki, mashauri zaidi ya 52 kuhusu kodi na mashauri mengi ya mirathi hivyo kufanya pesa nyingi zisiwepo kwenye mzunguko. Amewataka Majaji wapya wafikirie mbinu mpya za kutatua migogoro hii na sio kwenda kwa mazoea kama walivyo wanyama nyumbu.
Pamoja na hayo, Jaji Mkuu amewaasa kushughulikia Kesi watakazopewa kwa haraka ndani ya siku 90 kadri ya mwongozo wao ili kutokuingia kwenye mtego wa kuondolewa kwenye nafasi zao, pia wanapaswa kuwa na tabia njema wawapo kazini. Kazi zao zitaanza rasmi July 3, 2023 baada ya kukabidhi ofisi zao na kupata Semina fupi.
Akizungumza kwenye hafla hiyo, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan amempongeza Jaji Mkuu kwa kupata timu mpya na ameahidi kuendelea kuteua wanawake kila atakapofanya uteuzi ili kufikia 50/50.
"Kila nikitengeneza jopo nitakuletea na wanawake ili nifikie 50/50 jambo ambalo hatukulizoea huko nyuma. Lakini sasa kwa sababu wapo na wana qualify, na nina hakika majaji wanawake ni wazuri zaidi, huwa wanaogopa dhambi zaidi...." Amesema Rais Samia.
Amewataka kwenda kufanya kazi bila chuki, huba na upendeleo. Amesema ngazi ya Chini ya Mahakama bado kuna shida na uangalizi mkali unapaswa kufanywa ili haki kwa wananchi wa kawaida itendeke.
Kuhusu Baraza la Maadili, amemtaka Mwenyekiti wa Baraza hilo kusimamia maadili hasa ya watendaji wa Serikali na amesema yupo tayari kubadili watendaji wa baraza hilo ikiwa atapokea mapendekezo kama waliopo hawawezi kutekeleza vyema majukumu yao.
Awali, Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Tulia Ackson amesema Mhimili wa Mahakama nao hufanya kazi ya kumsaidia Rais. "Wakati mwingine mkitumia hili neno kumsaidia (Rais), kuna watu huwa hawaelewi kama Mhimili wa Mahakama nao hufanya kazi ya kumsaidia Rais lakini naamini sote tunasoma vitabu vyetu vya dini. Kazi zote huwa za Mfalme, wengine tunamsaidia Mfalme kuhakikisha Nchi inakaa sawa sawa"
Amempongeza Rais kwa kuendelea kuwaamini wanawake ambapo kwenye uapisho wa leo wanawake walikuwa 4 na wanaume 3, zaidi ya 50% ya walioapishwa leo.
Kama muwakilishi wa Bunge la wananchi, amewashauri Majaji kutoa haki kwa wakati na kutenda haki bila kuifukia.
Walioapishwa ni;
A. Majaji
- Mhe. Jaji Zainab Goronya Muruke, Kuwa Jaji wa Mahakama ya Rufaa
- Mhe. Jaji Leila Edith Mgonya, Kuwa Jaji wa Mahakama ya Rufaa
- Mhe. Jaji Amour Said Khamis, Kuwa Jaji wa Mahakama ya Rufaa
- Mhe. Jaji Dkt. Benhaji Shaaban Masoud, Kuwa Jaji wa Mahakama ya Rufaa
- Mhe. Jaji Gerson John Mdemu, Kuwa Jaji wa Mahakama ya Rufaa
- Mhe. Jaji Agnes Zephania Mgeyekwa, kuwa Jaji wa Mahakama ya Rufaa
Mhe. Jaji (MST) Rose Aggrey Teemba, Kuwa Mwenyekiti wa Baraza la Maadili.
===
Jaji Mkuu wa Tanzania Prof. Ibrahim Hamisi Juma amemshukuru Rais kwa kuongeza idadi ya Majaji wa Mahakama ya Rufani ambapo aliwakuta wapo chini ya 16 na sasa wamefika 31.
Majaji hawa 6 walioongezwa watasaidia kuboresha ufanisi wa Mahakama ya Rufani kutoka vikao 7 hadi 9 na kupunguza mzigo kwa kila jopo la Majaji.
Amesema kwa sasa kuna zaidi ya mashauri 200 yanayohusu fedha za kibenki, mashauri zaidi ya 52 kuhusu kodi na mashauri mengi ya mirathi hivyo kufanya pesa nyingi zisiwepo kwenye mzunguko. Amewataka Majaji wapya wafikirie mbinu mpya za kutatua migogoro hii na sio kwenda kwa mazoea kama walivyo wanyama nyumbu.
Pamoja na hayo, Jaji Mkuu amewaasa kushughulikia Kesi watakazopewa kwa haraka ndani ya siku 90 kadri ya mwongozo wao ili kutokuingia kwenye mtego wa kuondolewa kwenye nafasi zao, pia wanapaswa kuwa na tabia njema wawapo kazini. Kazi zao zitaanza rasmi July 3, 2023 baada ya kukabidhi ofisi zao na kupata Semina fupi.
Akizungumza kwenye hafla hiyo, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan amempongeza Jaji Mkuu kwa kupata timu mpya na ameahidi kuendelea kuteua wanawake kila atakapofanya uteuzi ili kufikia 50/50.
"Kila nikitengeneza jopo nitakuletea na wanawake ili nifikie 50/50 jambo ambalo hatukulizoea huko nyuma. Lakini sasa kwa sababu wapo na wana qualify, na nina hakika majaji wanawake ni wazuri zaidi, huwa wanaogopa dhambi zaidi...." Amesema Rais Samia.
Amewataka kwenda kufanya kazi bila chuki, huba na upendeleo. Amesema ngazi ya Chini ya Mahakama bado kuna shida na uangalizi mkali unapaswa kufanywa ili haki kwa wananchi wa kawaida itendeke.
Kuhusu Baraza la Maadili, amemtaka Mwenyekiti wa Baraza hilo kusimamia maadili hasa ya watendaji wa Serikali na amesema yupo tayari kubadili watendaji wa baraza hilo ikiwa atapokea mapendekezo kama waliopo hawawezi kutekeleza vyema majukumu yao.
Awali, Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Tulia Ackson amesema Mhimili wa Mahakama nao hufanya kazi ya kumsaidia Rais. "Wakati mwingine mkitumia hili neno kumsaidia (Rais), kuna watu huwa hawaelewi kama Mhimili wa Mahakama nao hufanya kazi ya kumsaidia Rais lakini naamini sote tunasoma vitabu vyetu vya dini. Kazi zote huwa za Mfalme, wengine tunamsaidia Mfalme kuhakikisha Nchi inakaa sawa sawa"
Amempongeza Rais kwa kuendelea kuwaamini wanawake ambapo kwenye uapisho wa leo wanawake walikuwa 4 na wanaume 3, zaidi ya 50% ya walioapishwa leo.
Kama muwakilishi wa Bunge la wananchi, amewashauri Majaji kutoa haki kwa wakati na kutenda haki bila kuifukia.