Rais Samia: Nimeagiza tozo ya mafuta irudishwe, asema nauli na bei za bidhaa vitapanda. Sababu ni vita ya Urusi

Replica

JF-Expert Member
Aug 28, 2017
1,441
7,780
Leo Rais Samia amepokea ripoti ya CAG Ikulu Dodoma na kuongelea mambo kadhaa ikiwemo suala la mafuta. Rais Samia amesema waziri husika aliondoa tozo ya Tsh 100 kwenye lita ya mafuta bila kuangalia upana wake ikiwemo tayari ilikuwemo kwenye bajeti ambayo ilipitishwa na Bunge hivyo Rais ameagiza irejeshwe.

Rais Samia ametaka wananchi kuambiwa ukweli kwamba nauli zitapanda na usafirishaji wa bidhaa umepanda, gharama ambazo zitaingizwa kwenye bei za vitu.

Kuhusu bei ya mafuta ya kula ameomba tathmini ya tozo iliyowekwa kwenye mafuta yanayotoka nje ili kulinda viwanda vya ndani itazamwe tena kwani viwanda hivyo vya ndani havizalishi.

========

Rais Samia: Bei zimepanda kwa bidhaa nyingi tunazoagiza kutoka nje lakini kuna upandaji wa bei za mafuta, mafuta yamekuwa yakipanda nadhani kutoka mwaka jana katikati ya mwaka.

Tukachukua hatua ya kupunguza tozo ndani ya mafuta kwa mara ya kwanza ili kushusha bei ya mafuta kwa wananchi lakini mafuta yameendelea kupanda.

Kipindi hiki cha pili mafuta yamepanda kwa 156 kwa lita, waziri akaona nikitoa shilingi mia yapande kwa shilingi 56 nitaleta unafuu ndani ya nchi lakini kwa bahati mbaya hakuangalia kwa upana zaidi ile ilikuwa tayari iko kwenye bajeti iliyopitishwa na bunge kwahiyo kulikuwa na utata kidogo, tumekaa kama Serikali tumerekebisha.

Ile shilingi iliyotoka, nimeagiza irudishwe na tathmini tuliyofanya hata kama ile shilingi tungeitoa, kwa mwenendo wa upandaji wa mafuta duniani, bado isingekuwa na impact ila tungejikosesha kile ambacho tunakifanya, kwahiyo tumeamua shilingi irudishwe.

Wabunge wenye maeneo yenu, mawaziri mnaosimamia sekta waambieni wananchi ukweli, vita ya Russia na Ukraine imepandisha sana bei ya mafuta na mafuta yanapopanda ndio kila kitu kinapanda.

Nauli zitapanda, usafirishaji wa bidhaa zitapanda. Sasa hivi kutoa kontena China ya bidhaa kuleta Tanzania walikuwa wanalipa kontena ya ft 40 dola 1500, sasa hivi ni dola 8,000-9,000. Hii inaenda kuingia kwenye bidhaa anazozileta kwahiyo waambieni wananchi ukweli, wasikae tu kulaumu Serikali haisemi kitu.

MAFUTA YA KULA
Rais Samia:
Nakumbuka nilikuagiza waziri wa fedha kwamba katika bajeti yetu tunayoimaliza tuliingiza kitu katika mafuta ya kula nadhani na ya nyuma yake ili kulinda viwanda vya ndani nadhani kwenye uzalishaji lakini pamoja na kuongeza hiyo kitu kuzuia mafuta ya nje yasije, viwanda vya ndani ndio vimefungwa kabisa hata huo uzalishaji wenyewe, kwahiyo naomba litizameni tena.

Kama haitusaidii ondoeni ili mafuta ya nje yaingie angalau hata kama bei itakuwa kubwa lakini wananchi wana mafuta ya kutumia. Sasa mmezuia ya nje hayaingii, ndani hayazalishwi, wananchi wanapiga kelele bila shaka mafuta yatapanda bei kwa kiasi kikubwa, nendeni katazameni vipengele vitakavyoleta unafuu kwa wananchi.

=> Kwa mfano kwenye bei ya mafuta Afrika Mashariki na kati Tanzania ndio ina bei ya chini kabisa ya mafuta lakini wenye sekta hawasemi, wamekaa tu wanajifungia.

PIA, Soma=> Rais Samia aagiza tozo za mafuta kupunguzwa
 
Leo mama Samia amesema ile tozo ya mafuta iliyotangazwa kufutwa kwenye mafuta aliaamua kuirudisha.

Wengi walipongeza ile tozo kufutwa vyombo vya habari vikaandika na kama kawaida wale jamaa zetu wakasifu kuwa hii Ni hatua nzuri. Looh kumbe ilipotangazwa kufutwa, raisi aliamua kuirudisha.

Cha ajabu kabisa wale walioshangilia na kusifu tozo ile kufutwa, leo watasifu ile tozo kuendelea. Lakini walikua hawajui Kama inaendelea.

Nguvu iliyotumika kutoa taarifa ya kufutwa tozo ilipaswa pia itumike tozo iliporudishwa. Lakini kukaa kimya haikua sawa kabisa.

Lakini pia mama Samia hii Bei ya dunia ya mafuta iliyopo sasa iliwahi kuwepo 2012 lakini Bei huku haikua hii, au Kuna kitu kingine kimepandisha mafuta huku zaidi ya soko la dunia?
 
Baada ya report yake mwaka jana, CAG alifanya press conference na kuichambua report yake huku akieleza kinagaubaga mapungufu yote aliyoyaona.

Na mwaka huu itakuwepo? Ataifanya lini? Ataifanyia wapi? Atutangazie mapema ili tujipange kuhudhuria. Ule utaratibu ulikuwa mzuri sana. Tuendelee na uleule uwazi.

Kazi iendelee. 😂
 
Rais Samia: Bei zimepanda kwa bidhaa nyingi tunazoagiza kutoka nje lakini kuna upandaji wa bei za mafuta, mafuta yamekuwa yakipanda nadhani kutoka mwaka jana katikati ya mwaka.

Tukachukua hatua ya kupunguza tozo ndani ya mafuta kwa mara ya kwanza ili kushusha bei ya mafuta kwa wananchi lakini mafuta yameendelea kupanda.

Kipindi hiki cha pili mafuta yamepanda kwa 156 kwa lita, waziri akaona nikitoa shilingi mia yapande kwa shilingi 56 nitaleta unafuu ndani ya nchi lakini kwa bahati mbaya hakuangalia kwa upana zaidi ile ilikuwa tayari iko kwenye bajeti iliyopitishwa na bunge kwahiyo kulikuwa na utata kidogo, tumekaa kama Serikali tumerekebisha.

Ile shilingi iliyotoka, nimeagiza irudishwe na tathmini tuliyofanya hata kama ile shilingi tungeitoa, kwa mwenendo wa upandaji wa mafuta duniani, bado isingekuwa na impact ila tungejikosesha kile ambacho tunakifanya, kwahiyo tumeamua shilingi irudishwe.
Safi ndio maana namkubali mama, huwa hapepesi macho aki focus jambo lazima akomae nalo, mtukane, mnune au msengenye ndio kwanza anawapuuza.

Tukutane 2025, watu mtaumia wee lakini matokeo yatayoishi vizazi na vizazi yataendelea kuwepo.
 
Huyu bibi bora arudi Zanzibar hajui shs 100 ni kubwa sn kwenye mafuta na tunaoumia ni sisi yeye anapewa bure kila kitu ndiyo maana anaona siyo kitu, hafai kabisa kuwa kiongozi.
Kwa mujibu wako wewe timu mwenda zake, HUONI U.K, GERMAN, USA, INDIA WANANCHI WANALALAMA JUU YA BEI YA MAFUTA KWA GALON YAMEPANDA ALMOST MARA MBILI,/ PENDA KUJUA PIA MAMBO YA KIMATAIFA.
 
Back
Top Bottom