Rais Samia ni team waungwana adui hawamuumizi wala hawamtesi, wanamvuta karibu na kummonita

Superbug

JF-Expert Member
Jan 31, 2018
12,417
30,927
Mama ni muungwana na anafwata ushauri wa kikwete na jk alikuwa ni mtu muungwana.

MFANO WA MWANDOSYA
Wakati wa utawala wa jk MWANDOSYA alikuwa tishio sana na infact MWANDOSYA na JK walishazinguana miaka ya 90 wakati wa utawala wa mwinyi. Wakati huo JK alikuwa waziri wa nishati na MWANDOSYA alikuwa karibu mkuu. Ugomvi wao ulisuluhishwa na mzee mwinyi.

Japo bifu lilidumu na JK alipokuwa rais alimpa wizara MWANDOSYA lakini baadae ili amdhibiti vizuri akampa wizara isiyokuwa na jukumu lolote pale ikulu. Huu ni uungwana aliotumia jk kumvuta MWANDOSYA ili amdhibiti na vyombo vya udhibiti vya ikulu (tiss);

MFANO WA KABUDI NA LUKUVI
Team waungwana kama kawaida inafwata Mfumo wa jk kabudi na mwenzake lukuvi walishaonyesha kuwa threat kwa system ya mama kwahiyo kuitwa ikulu ni ile dhana ya kuwa karibu na adui ili udhibiti. Hata kapolepole kamepelekwa kule ili kadhibitiwe kumbuka vipepeo weusi hawana mipaka na jicho la mwewe halitambui mipaka ya kijografia.

Kinyume na team sukuma ile iliumiza watu na adui alifinywa barabara.
 
Kwa mwandosya Kuna kitu umekiruka kwa makusudi, mwandosya awamunya 4 alipewa sumu.

Lakini pia hata kwa Samia inategemea na mtu, nilivyoona wameshindwa kumsamehe ndugai nikaona huo uungwana hana.

Wanasiasa sio waungwana Kama unavyodhani, inategemea tu ww ni threat kwa kiasi gani kwao. Ukiwa na madhara kidogo ndio utaaona uungwana na ukiwa na madhara makubwa basi u will face consequences.

Hata mwendazake Kuna watu aliwafanyia uungwana pamoja na kuikosoa serikali akiwemo bashe, akampa uwaziri. tu pengine bashe hakuwa na madhara makubwa kwake.
 
Ni JK Na Mama tu?au kuna washauri wanasikilizwa?..

Inawezekana Mwendazake hakusikiliza washauri..
 
Ni JK Na Mama tu?au kuna washauri wanasikilizwa?..

Inawezekana Mwendazake hakusikiliza washauri..
Ni JK na Mkulu tu.....
Kuna kubwa ambalo waliopo kwenye kufurahia keki ya Taifa hawalioni...
Kuna jambo linakuja litaumiza wengi wapendao chama tawala na wapinzani..
Ni swala la muda tu....hii teua hamisha peleka rudisha
Swala la kule kwa Wamasai wanunuzi wanatengeneza wigo

Linda sana imani yako ..... Ni maandiko sio mimi
 
Back
Top Bottom