Salary Slip
JF-Expert Member
- Apr 3, 2012
- 46,888
- 143,985
Katika hali ya kawaida, Rais Samia atapaswa kuwa mnyenyekevu na mpole kwa wajumbe wa Mkutano Mkuu wa CCM unaotaraijiwa kufanyika April 30 mwaka huu(nimesoma mahala), mkutano utakaokuwa na jukumu la kumchagua mwenyekiti wa CCM Taifa huku mama Samia akitarajiwa kuwa ni mgombea pekee.
Kwa mantiki hiyo, sioni uwezekano wa Rais Samia kuwa huru na kufunguka mbele ya wabunge wa CCM atapohotubia Bunge hiyo kesho zaidi ya kulazimika kuwa mpole mbele ya wapiga kura wake iwapo ni kweli haridhishwi na mwenendo wa wabunge licha ya kuwa hapaswi kuingilia Bunge kama mhimili unaojitegemea.
Hata hivyo, hali inaweza kuwa tofauti iwapo Mama Samia anataka kutumia sehemu ya hotuba yake Bungeni kujiipigia kampeni na hili tutaligundua kutokana na aina ya hotuba atayoitoa hiyo kesho.
Uwezekano wa Rais Samia kuchaguliwa upo na ni mkubwa tu, ila pia upo uwezekano wa yeye kuweka rekodi ya kupata ushindi mdogo kulinganisha na watangulizi wake. Hii inatokana na hali iivyo hivi sasa ndani ya CCM na kama inavyojidhihirisha hata ndani ya Bunge.
Hivyo, kama Mama Rais Samia anataka kufunguka ndani ya Bunge, ni bora asubiri uchaguzi upite, ila kama yuko kwenye kampeni, basi ameona mbali na itabidi awe mpole tu mbele ya wabunge wa CCM (wajumbe wa mkutano mkuu).
Nawasilisha.
Kwa mantiki hiyo, sioni uwezekano wa Rais Samia kuwa huru na kufunguka mbele ya wabunge wa CCM atapohotubia Bunge hiyo kesho zaidi ya kulazimika kuwa mpole mbele ya wapiga kura wake iwapo ni kweli haridhishwi na mwenendo wa wabunge licha ya kuwa hapaswi kuingilia Bunge kama mhimili unaojitegemea.
Hata hivyo, hali inaweza kuwa tofauti iwapo Mama Samia anataka kutumia sehemu ya hotuba yake Bungeni kujiipigia kampeni na hili tutaligundua kutokana na aina ya hotuba atayoitoa hiyo kesho.
Uwezekano wa Rais Samia kuchaguliwa upo na ni mkubwa tu, ila pia upo uwezekano wa yeye kuweka rekodi ya kupata ushindi mdogo kulinganisha na watangulizi wake. Hii inatokana na hali iivyo hivi sasa ndani ya CCM na kama inavyojidhihirisha hata ndani ya Bunge.
Hivyo, kama Mama Rais Samia anataka kufunguka ndani ya Bunge, ni bora asubiri uchaguzi upite, ila kama yuko kwenye kampeni, basi ameona mbali na itabidi awe mpole tu mbele ya wabunge wa CCM (wajumbe wa mkutano mkuu).
Nawasilisha.