Binafsi mimi ni kijana mdogo sana. Naomba nisema Mh. Rais Samia shikamoo.
Mh. Rais nasikitishwa na mateso anayopitia mzee Mbowe kwa baraka za utawala wako, sikudhani wewe ungekuja kuongeza mikanganyiko ya kisiasa nchini.
Naomba ujiulize maswali yafuatayo kisha ufanye yakupendezayo mama angu.
1. Unadhani kikombe/mateso anayopitia mzee Mbowe unaweza kuyapitia wewe binafsi?
2. Unadhani kumsingizia mtu kutaiponya nafsi yako mama angu mpendwa?
3. Unadhani familia ya mzee Mbowe haimuhitaji kama ambavyo ya kwako inakuhitaji?
4. Kama kweli wewe mzalendo kwanini unaogopa katiba mpya?
5. Kama kweli mbingu ipo unahisi utairithi kwa kufumbia macho mateso ya wenzio?
6. Je, Wewe nafsi yako inakwambiaje kuhusu kesi ya mzee mbowe?
Hili nalo lichukue mama.
Hivi unajua kinachoendelea kwenye vifaa vya ujenzi? kama unajua, je, Unadhani maisha ya Watanzania umeyaboresha ili kuweza kumudu mfumuko wa bei ambao haujawahi kutokea kwa miaka 20?
Hii si yako.
IGP sirro kila nikitaka kuandika juu yako nashindwa mzee wangu, hivi Mzee Mbowe alikula nini chako umma ujue? Mbona chuki yako dhidi yake inakuwa kubwa sana?
Mbona ulivyopewa maelekezo kumkamata Gwajima uligoma? Nahisi ulisimamia taaluma yako, lakini inapokuja swala la Mbowe hujiulizi mara mbili bali unamshushia kikombe cha mateso haraka sana kuna nini kati yako na Mbowe? Mungu asikupungukie Mzee wangu Sirro ila unachokitenda sidhani kama kitakupa faraja.
Mh. Rais nasikitishwa na mateso anayopitia mzee Mbowe kwa baraka za utawala wako, sikudhani wewe ungekuja kuongeza mikanganyiko ya kisiasa nchini.
Naomba ujiulize maswali yafuatayo kisha ufanye yakupendezayo mama angu.
1. Unadhani kikombe/mateso anayopitia mzee Mbowe unaweza kuyapitia wewe binafsi?
2. Unadhani kumsingizia mtu kutaiponya nafsi yako mama angu mpendwa?
3. Unadhani familia ya mzee Mbowe haimuhitaji kama ambavyo ya kwako inakuhitaji?
4. Kama kweli wewe mzalendo kwanini unaogopa katiba mpya?
5. Kama kweli mbingu ipo unahisi utairithi kwa kufumbia macho mateso ya wenzio?
6. Je, Wewe nafsi yako inakwambiaje kuhusu kesi ya mzee mbowe?
Hili nalo lichukue mama.
Hivi unajua kinachoendelea kwenye vifaa vya ujenzi? kama unajua, je, Unadhani maisha ya Watanzania umeyaboresha ili kuweza kumudu mfumuko wa bei ambao haujawahi kutokea kwa miaka 20?
Hii si yako.
IGP sirro kila nikitaka kuandika juu yako nashindwa mzee wangu, hivi Mzee Mbowe alikula nini chako umma ujue? Mbona chuki yako dhidi yake inakuwa kubwa sana?
Mbona ulivyopewa maelekezo kumkamata Gwajima uligoma? Nahisi ulisimamia taaluma yako, lakini inapokuja swala la Mbowe hujiulizi mara mbili bali unamshushia kikombe cha mateso haraka sana kuna nini kati yako na Mbowe? Mungu asikupungukie Mzee wangu Sirro ila unachokitenda sidhani kama kitakupa faraja.