Rais Samia, naomba unisaidie ajira mwanao

Kop0

Member
Oct 6, 2021
71
96
Shikamoo Mheshimiwa Raisi Mama Samia!

Mimi ni kijana muhitimu wa Elimu ya chuo Kikuu nikiwa na Degree ya Uchumi pamoja na Diploma ya Uchumi. Nimehitimu chuo mwaka 2012 hapa hapa Tanzania ila kwa bahati mbaya sikupata ajira sehemu yeyote hadi leo hii.

Nilikuwa na biashara yangu ya duka ambayo ilikuwa ni tegemezi kwa familia yangu ila kwa sasa biashara hiyo imekata mtaji kabisa baada ya wezi kuvunja na kuchukua vitu vyote na kubaki nikiwa mtupu. Naomba nisaidie mama nipate ajira yeyote nakuaahidi kutokukuangusha Mama yangu nisaidie mwanao ambae kwa kweli maisha magumu sana kwangu.

Okoa Familia yangu ambayo ambayo ipo mbioni kubomoka kutokana na ugumu wa maisha yangu kwa kukosa ajira na kutokuwa na mtaji wowote kwa sasa. Natanguliza shukrani za dhati upatapo ujumbe huu.
 
duuuh NJOO INBOX
JamiiForums1758375822.jpg
 
Shikamoo Mheshimiwa Raisi Mama Samia!

Mimi ni kijana muhitimu wa Elimu ya chuo Kikuu nikiwa na Degree ya Uchumi pamoja na Diploma ya Uchumi. Nimehitimu chuo mwaka 2012 hapa hapa Tanzania ila kwa bahati mbaya sikupata ajira sehemu yeyote hadi leo hii.

Nilikuwa na biashara yangu ya duka ambayo ilikuwa ni tegemezi kwa familia yangu ila kwa sasa biashara hiyo imekata mtaji kabisa baada ya wezi kuvunja na kuchukua vitu vyote na kubaki nikiwa mtupu. Naomba nisaidie mama nipate ajira yeyote nakuaahidi kutokukuangusha Mama yangu nisaidie mwanao ambae kwa kweli maisha magumu sana kwangu.

Okoa Familia yangu ambayo ambayo ipo mbioni kubomoka kutokana na ugumu wa maisha yangu kwa kukosa ajira na kutokuwa na mtaji wowote kwa sasa. Natanguliza shukrani za dhati upatapo ujumbe huu.
Ewe mtaalamu wa uchumi, kwenye uchumi kuna kitu kinaitwa "diversification of capital" hii concept uliitumia vipi wakati duka likiwa kwenye hali nzuri?
 
Ewe mtaalamu wa uchumi, kwenye uchumi kuna kitu kinaitwa "diversification of capital" hii concept uliitumia vipi wakati duka likiwa kwenye hali nzuri?
Mkuu nipo hapa kuomba msaada na nashida we elewa ivyo inatosha.
 
Mkuu yaani umeandaa karamu ya milioni kumi ukasahau kununua tooth stick za buku,

Bandiko zuri umesahau kuandika namba yako ya simu, sasa mama takupataje?? Akufuate inbox leo!!?? Weka namba yako Basi na baade utupe mrejesho.
 
8 Reactions
Reply
Back
Top Bottom