Rais Samia, nakuomba angalia upya Mradi wa BRT Dar

Niende moja kwa moja kwenye mada yangu ya leo ninayotaka kuizungumzia.

Mama Samia Suluhu Hassan, Rais wetu, nakuomba chonde chonde kuuangalia upya mradi wa BRT unao endelea kujengwa jijini Dar es salaam. Kwa uzoefu mkubwa nilio nao na analysis yangu ndogo niliyo ifanya naona kuwa huu mradi hautakuwa na impact yoyote kubwa kwenye maisha ya wakazi wa jiji la Dar es salaam katika;

1. Kumpunguza tatizo la usafiri jijini
2. Kutoa ajira nyingi kwa vijana
3. Kuleta transformation yoyote ile ya kiteknolojia ambayo itawawezesha vijana kupanua bongo zao na
4. Uharibifu wa mazingira kwa nishati inayotokana na matumizi ya mafuta mengi ya diesel

Mama nafikiri umeshatembelea nchi nyingi za ulimwengu na kuona miji yake yenye wakazi wengi. Kwenye hizo nchi nafikiri umeona pia jinsi gani wenzetu walivyo jitahidi kuondoa tatizo la usafiri wa abiria wanao kwenda kazini asubuhi na kurudi majumbani kwao baada ya kazi. Sambamba na usafiri wa mabasi ya public, commuter trains au niseme under ground na street trains au trams zimetamalaki sana.

Sisemi tujenge underground trains ila tu ningependa kusisitiza kuwa sambamba na mabasi ya mwendo kasi, commuter trains nazo zingepewa kipau mbele kikubwa katika kukabiliana na tatizo la usafiri wa abiria katika mji unao kua kwa kasi sana kama Dar es salaam. Mabasi ya mwendo kasi peke yake kwa jiji letu sitegemei kama yatakidhi mahitaji yanayo takiwa huko mbeleni.

Ni jambo ambalo sote tunajua kuwa Tanzania na hasa mji wa Dar es salaam unakabiliwa na uhaba mkubwa sana wa ajira kwa vijana wetu wanao maliza shulr na vyuo. Na serikali naona haina mbinu kubwa ya kutatua tatizo hili mbali na kutegemea wawekezaji wa sekta binafsi kutoka nje na ambao sio wengi wanaomiminika nchini.

Nafikiri tumeshuhudia wenyewe jinsi treni ya umeme ilivyopokelewa kwa miyo mkubjufu na watanzania na kusisitiza kumalizika kwa SGR ili watanzania waone matokeo yake.

Commuter trains na karakana zake zitasaidia kupunguza uhaba wa ajira kwa vijana na vile vile ni chachu ya vijana kuweza kupanua uwezo wao wa kufikiri kuhusina na teknolojia hii mpya kwao.

Connections kati ya miji kama Bagamoyo , Kibaha, Mkuranga na Kisarawe na Station yetu ya Tanzanite na Magufuli Bus Terminal, ingekuwa ni rahisi sana. Lakini kwa vile tuna waziri wa ujenzi na watu wa mipango miji ambao hawana vision, inakuwa shida sana kwa nchi kama Tanzania kupiga hatua kubwa na za haraka kiteknolojia.

Nashindwa kuelewa Mama Samia mipango ya serikali ya kusafirisha abiria jijini pindi SGR yetu ya Mwanza, Kigoma na nchi jirani itakapo kuwa imemalizika. Mji utakuwa haupitiki kwa foleni za magari na msongamano wa watu watakao pata nafasi ya kuja Dar haraka kufanya biashara kutoka mikoani na nchi jirani.

Jiji halina budi kujipanga sasa jinsi ya kukabiliana na changamoto la baadae. Tuna watu wa aina gani Mama ambao hata ile fikra ya kutambua nini matokeo ya baadae?

Mama sisi tunakutegemea wewe sana, kwani tunaimani ya kuwa una ile spirit ya kipenzi chetu Hayati Rais Magufuli. Haya mambo usipoyafanya wewe sidhani kama kuna mwingine atakaye kuwa na spirit yako na Hayati Rais Magufuli.

Swala jingine kubwa linalo tufanya tujenge usafiri wa commuter trains kwa haraka ni uharibifu wa mazingira. Kwa vile usafiri wa mabasi unachochea sana kwenye uharibifu wa mazingira kwa nishati inayotumia ya diesel haina budi kutafuta njia mbadala wa kuondokana na tatizo la uchafuzi wa hali ya hewa jijini.

Hivi haya mabasi yetu ya mwendo kasi yana partickel Filter na catalylizer ili kupunguza air polution?
Tatizo viongozi wetu hawasafiri, huyo “kipenzi chetu “ Magufuli aliishia Burundi tu, na hata wakisafiri hawatembei! Mtu mwenye uzoefu wa kuishi nje ya nchi hasa za Ulaya na America kwa muda mrefu ndio anaweza kuleta mawazo mazuri sio hawa viongozi wetu wa Dar-Dodoma.
 
Tatizo viongozi wetu hawasafiri, huyo “kipenzi chetu “ Magufuli aliishia Burundi tu, na hata wakisafiri hawatembei! Mtu mwenye uzoefu wa kuishi nje ya nchi hasa za Ulaya na America kwa muda mrefu ndio anaweza kuleta mawazo mazuri sio hawa viongozi wetu wa Dar-Dodoma.
Naunga mkono hoja
 
Tatizo viongozi wetu hawasafiri, huyo “kipenzi chetu “ Magufuli aliishia Burundi tu, na hata wakisafiri hawatembei! Mtu mwenye uzoefu wa kuishi nje ya nchi hasa za Ulaya na America kwa muda mrefu ndio anaweza kuleta mawazo mazuri sio hawa viongozi wetu wa Dar-Dodoma.
Hapana wanasafiri sana ila sisi hatuwezi jua. Mara nyingi wanafanya safari za kitalii. Hapo ndipo wana kuwa na uwezo wa kutembelea sehemu nyingi private na.kujionea mambo mengi jinsi yalivyo kwenye nchi za wwnzetu.

Tatizo kubwa ninalo liona ni kuwa wanakosa maarifa mapana kama ya Hayati Rais Magufuli. Lile jamaa liliipenda Tanzania na watanzania kwa ujumla. Alikuwa yuko tayari kufa kuliko kuona wananchi wenzake na nchi yake inateseka.

Tanzania tunakosa wanasayansi wanao jiamini. Katika nchi zenye mfumo kama huu wa kwetu ni Rais tu peke yake mwenye uwezo wa kubadilisha hali ya maisha ya nchi. Kama Rais hana vision na uwezo wa ku impliment yale anayo yataka na kuyaona, hiyo sahau.

Viongozi wengine wote hawawezi kufanya mambo wanayotaka bila Rais kutia idhini yake ya kutoa pesa za ku finance mambo hayo wanayo taka yafanyike.

Kitu kikubwa kinacho tuharibu ni kule kukosa spirit ya uwajibikaji wa watendaji wizarani na kwenye taasisi zinazohusika na utekelezaji wa malengo na maazimio ya serikali. Watumishi wanaopewa madaraka mara nyingi huwa hawatendi yale mambo kama ilivyo kusudiwa.

Hizo hela za miradi kutoka serikali kuu na halmashauri watumishi na watendaji always wanazipigia mahesabu jinsi gani wao binafsi wataweza faidika na hela hizo za miradi ya maendeleo. Hapo haijalishi kama hana barabara ya kupita na gari lake au la. Anacho taka ni hela mfukoni ili aonekane kwa watu kuwa yeye ni tajiri na kuzifanyia hizo hela matumizi ya mambo ya hanatha.
 
Hongere mkuu nipe na mimi mchongo nije huko nioshe macho kidogo
Ningekushauri baki tu Tanzania na ijenge Tanzania yetu. Mbona Tanzania ni nchi nzuri sana! Europe ni stress pure! Ulaya kwa wewe mtu mweusi utakuwa mtumwa tu ndugu yangu bila kujitambua. Mimi nina miaka 35 Ulaya, lakini kwenye nchi ninayo ishi wananiona ni "Alien" tu. Hata nifanye nini ninabaki kuwa Alien kwao. Ni kitu ambacho kina ninyima raha sana. Ndiyo maana huwa nakuja ku Tank furaha Tanzania.
 
Niende moja kwa moja kwenye mada yangu ya leo ninayotaka kuizungumzia.

Mama Samia Suluhu Hassan, Rais wetu, nakuomba chonde chonde kuuangalia upya mradi wa BRT unao endelea kujengwa jijini Dar es salaam. Kwa uzoefu mkubwa nilio nao na analysis yangu ndogo niliyo ifanya naona kuwa huu mradi hautakuwa na impact yoyote kubwa kwenye maisha ya wakazi wa jiji la Dar es salaam katika;

1. Kumpunguza tatizo la usafiri jijini
2. Kutoa ajira nyingi kwa vijana
3. Kuleta transformation yoyote ile ya kiteknolojia ambayo itawawezesha vijana kupanua bongo zao na
4. Uharibifu wa mazingira kwa nishati inayotokana na matumizi ya mafuta mengi ya diesel

Mama nafikiri umeshatembelea nchi nyingi za ulimwengu na kuona miji yake yenye wakazi wengi. Kwenye hizo nchi nafikiri umeona pia jinsi gani wenzetu walivyo jitahidi kuondoa tatizo la usafiri wa abiria wanao kwenda kazini asubuhi na kurudi majumbani kwao baada ya kazi. Sambamba na usafiri wa mabasi ya public, commuter trains au niseme under ground na street trains au trams zimetamalaki sana.

Sisemi tujenge underground trains ila tu ningependa kusisitiza kuwa sambamba na mabasi ya mwendo kasi, commuter trains nazo zingepewa kipau mbele kikubwa katika kukabiliana na tatizo la usafiri wa abiria katika mji unao kua kwa kasi sana kama Dar es salaam. Mabasi ya mwendo kasi peke yake kwa jiji letu sitegemei kama yatakidhi mahitaji yanayo takiwa huko mbeleni.

Ni jambo ambalo sote tunajua kuwa Tanzania na hasa mji wa Dar es salaam unakabiliwa na uhaba mkubwa sana wa ajira kwa vijana wetu wanao maliza shulr na vyuo. Na serikali naona haina mbinu kubwa ya kutatua tatizo hili mbali na kutegemea wawekezaji wa sekta binafsi kutoka nje na ambao sio wengi wanaomiminika nchini.

Nafikiri tumeshuhudia wenyewe jinsi treni ya umeme ilivyopokelewa kwa miyo mkubjufu na watanzania na kusisitiza kumalizika kwa SGR ili watanzania waone matokeo yake.

Commuter trains na karakana zake zitasaidia kupunguza uhaba wa ajira kwa vijana na vile vile ni chachu ya vijana kuweza kupanua uwezo wao wa kufikiri kuhusina na teknolojia hii mpya kwao.

Connections kati ya miji kama Bagamoyo , Kibaha, Mkuranga na Kisarawe na Station yetu ya Tanzanite na Magufuli Bus Terminal, ingekuwa ni rahisi sana. Lakini kwa vile tuna waziri wa ujenzi na watu wa mipango miji ambao hawana vision, inakuwa shida sana kwa nchi kama Tanzania kupiga hatua kubwa na za haraka kiteknolojia.

Nashindwa kuelewa Mama Samia mipango ya serikali ya kusafirisha abiria jijini pindi SGR yetu ya Mwanza, Kigoma na nchi jirani itakapo kuwa imemalizika. Mji utakuwa haupitiki kwa foleni za magari na msongamano wa watu watakao pata nafasi ya kuja Dar haraka kufanya biashara kutoka mikoani na nchi jirani.

Jiji halina budi kujipanga sasa jinsi ya kukabiliana na changamoto la baadae. Tuna watu wa aina gani Mama ambao hata ile fikra ya kutambua nini matokeo ya baadae?

Mama sisi tunakutegemea wewe sana, kwani tunaimani ya kuwa una ile spirit ya kipenzi chetu Hayati Rais Magufuli. Haya mambo usipoyafanya wewe sidhani kama kuna mwingine atakaye kuwa na spirit yako na Hayati Rais Magufuli.

Swala jingine kubwa linalo tufanya tujenge usafiri wa commuter trains kwa haraka ni uharibifu wa mazingira. Kwa vile usafiri wa mabasi unachochea sana kwenye uharibifu wa mazingira kwa nishati inayotumia ya diesel haina budi kutafuta njia mbadala wa kuondokana na tatizo la uchafuzi wa hali ya hewa jijini.

Hivi haya mabasi yetu ya mwendo kasi yana partickel Filter na catalylizer ili kupunguza air polution?
Commutter trains (London) na tramways (Warsaw) na mwendokasi (Dar, Dubei, Bogota na Bangkok) ni kitu hichohicho kimoja: concept ni kwamba yawe na exclusive right of way kwenye njia yake, yasiwe na foleni. Hayo matatizo au fursa unazosema ni hizohizo across the board. Latest research indicates that "BRT" ya buses au trams au trains zote ni mwendokasi. Ipi uchague ni gharama ya magari (light metals, aluminium) na train/tram ambazo ni chuma tupu

Kuhusu pollution, dawa yake na CNG, compressed natural gas, sasa hii most motor vehicles are converting to CNG while some manufacturers (Honda, Volvo, Samsung, Ikarus) are already manufacturing for CNG fuel.

Cha kufanya ni tuwape support mwendokasi wasambae mji mzima, then wahamie Zanzibar, Mwanza, Mbeya, kote.

Tatizo kubwa linalotajwa ni mtaji, kwa private sector, au bajeti ya serkali. Hili nalo tayari lilishatuliwa - tutatumia soko la hisa DSE kupata collective investors. Mwendojasi itaunganishwa na terminals kuwa na shopping malls kama za Dubai na Thailand. Kwa kutumia kitu huitwa REITS (real estate investment trusts) tutabadilisha kabisa mfumo mzima wa infrastructure funding na mfumo wetu wa fedha.
 
Ningekushauri baki tu Tanzania na ijenge Tanzania yetu. Mbona Tanzania ni nchi nzuri sana! Europe ni stress pure! Ulaya kwa wewe mtu mweusi utakuwa mtumwa tu ndugu yangu bila kujitambua. Mimi nina miaka 35 Ulaya, lakini kwenye nchi ninayo ishi wananiona ni "Alien" tu. Hata nifanye nini ninabaki kuwa Alien kwao. Ni kitu ambacho kina ninyima raha sana. Ndiyo maana huwa nakuja ku Tank furaha Tanzania.
Mkuu mimi nachotaka ni pesa, issue ya heshima hiyo kwangu haina nafasi, hata wanione kinyesi poa tu.
 
UDART panakosekana uongozi na utaalam wa kuendesha shirika la usafirishaji kisasa. Serikali ingerudisha Public Private Partnership(PPP) ili UDART ijiendeshe kama entity ya kibiashara. Kuanzia maintenance ya mabasi, maintenance ya mifumo iliyofungwa, usimamizi wa vituo, usimaizi wa route, kukusanya nauli/mapato ni vitu vinaweza kuvunjwa vikafanywa na private entities ziwe na SLA za kuwawajibisha. UDART abaki kufanya supervision, kulipa mishahara na kuangalia maslahi ya serikali na shareholders wengine.

Phase 1 hii cha mtoto, nasubiri kuona Phase 2 huko mbagala ile nyomi kwa style hii ya ubabaishaji watafanyaje.
 
Mkuu mimi nachotaka ni pesa, issue ya heshima hiyo kwangu haina nafasi, hata wanione kinyesi poa tu.
Duh! Sawa kwa msimamo wako thabiti! Lakini elewa kuwa hata ukipata nafasi ya kwenda kufanya kazi na kuishi Ulaya utataka kuwa na familia ambayo hiyo ndiyo itapata shida sana baadae na manyanyaso ya wazungu.

Kumbuka pia kuwa wewe sio ndiyo uliyeanza kuwa na fikra hizo, hata sisi tulipokuwa tuko Bongo kabla ya kwenda Ulaya tulikuwa na mawazo hayo hayo, lakini ukisha isha nao kwa mda mrefu na umri ukikuingia kidogo ndiyo hapo unaona "majuto ni mjukuu." Unaanza kuona athari ulizozipata mpaka kwenye familia yako.

Inaumoza sana. Na inavunja moyo. Nikutakia mafanikio makubwa katika jitihada zako za kqenda kutafuta hela Ulaya au Amerika..
 
Daladala zirejeshwe tu njia ya ferry, Posta, fire,magomeni, manzense, ubungo,kimara na mbezi ndio ujinga wa kuendesha Mwendokasi kupumbavu utakoma kujaza gani kule
 
Back
Top Bottom