Mag3
Platinum Member
- May 31, 2008
- 13,064
- 22,757
Rais wetu Mh. Samia Suluhu Hassan, ada ya mja hunena, mwungwana ni kitendo na siku njema huonekana asubuhi.
Wewe ni Rais wetu kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania uliyoapa kuiheshimu, kuilinda na kuitetea.
Kupitia hiyo Katiba sisi wananchi tuliamua rasmi na kwa dhati kujenga jamii inayozingatia misingi ya uhuru, haki, udugu na amani.
Mh. Rais, tarehe 29 Machi, 2021 uliapishwa kuliongoza Taifa la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika hafla iliyofanyika Ikulu Jijini Dar-es-Salaam.
Leo tarehe 9 Mei, 2021 ni siku ya arobaini toka ulipoapishwa na kuwa Kiongozi Mkuu wa taifa hili lenye watu karibia milioni sitini (60,000,000!)
Kama kiongozi matendo yako ni lazima yalete faraja na matumaini kwa Watanzania wote na kuhamasisha zaidi ushiriki wao katika hatma ya taifa.
Pamoja na kuapa kuiheshimu, kuilinda na kuitetea Katiba, epukana kabisa na matendo yanayoweza kutafsiriwa kwamba yanapingana na Katiba.
Mh. Rais kumbuka kauli huumba hivyo epukana pia na zile kauli ambazo zinaweza kutafsiriwa na wasaidizi wako kama ruhusa ya kuvunja Katiba.
Hali hii inahusu hasa yale maagizo yanayotolewa papo kwa papo bila kupima yatakavyopokelewa na watendaji wakuu wa vyombo vya dola.
Mh. Rais tuko wengi ambao kuapishwa kwako kulitupa japo faraja kutokana na mizengwe ya awali iliyokuwa ikifanywa na mahafidhina.
Amini usiamini asilimia kubwa ya wananchi bila kujali tofauti zao walipokea mabadiliko ya uongozi wa juu kabisa wa nchi kwa matumaini.
Yawezekana walisukumwa na sababu mbali mbali lakini lililowaunganisha ni uhitaji wa hewa safi kupitia dirisha ambalo ujio wako ungewafungulia.
Ni hilo dirisha lingewezesha kiapo chako kiwe na maana kwa kuturudisha kwenye utawala wa sheria unaoheshimu, kulinda na kutetea Katiba
Ingawa wengi tulikupokea bila kujali unatoka miongoni mwa watu wale wale na chama kile kile, tuliguna kidogo uliposema kazi iendelee.
Kiongozi bora hafuati tu nyayo za aliyemtangulia, hapana, huyo si kiongozi bora, ni mfuasi, kiongozi bora huvumbua njia salama wapite anaowaongoza.
Tafadhali Mh. Rais, acha kupaka ukuta rangi nyumba ipendeze huku msingi una nyufa; shughulikia kwanza msingi nyumba iwe imara na salama.
Tunayo Katiba ya mwaka 1977 lakini cha ajabu ni kuwa hata hii, pamoja na mapungufu yake, tunashindwa kuiheshimu, kuilinda na kuitetea!
Tunayo Rasimu ya Warioba lakini kwako Mh. Samia Suluhu Hassan, hata kuitaja tu imekuwa shida, shida ni nini? Je kuku wetu anataga kwenye miba?
Mwanga uliojitokeza unaanza kufifia ghafla huku safari hatujafika hata nusu, je kulikoni? Chukua hatua na katika kuidai Katiba mpya sahau suluhu.
Shughulikia sheria zote ambazo zinaisigina Katiba kwa namna moja au nyingine kwani tuna kiu kubwa ya utawala unaozingatia haki na usawa.
Ngoja Ngoja yaumiza matumbo na linalowezekana leo lisingojee kesho; kwa kweli baada ya miaka minne ya giza uvumilivu uko mashakani.
Wewe ni Rais wetu kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania uliyoapa kuiheshimu, kuilinda na kuitetea.
Kupitia hiyo Katiba sisi wananchi tuliamua rasmi na kwa dhati kujenga jamii inayozingatia misingi ya uhuru, haki, udugu na amani.
Mh. Rais, tarehe 29 Machi, 2021 uliapishwa kuliongoza Taifa la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika hafla iliyofanyika Ikulu Jijini Dar-es-Salaam.
Leo tarehe 9 Mei, 2021 ni siku ya arobaini toka ulipoapishwa na kuwa Kiongozi Mkuu wa taifa hili lenye watu karibia milioni sitini (60,000,000!)
Kama kiongozi matendo yako ni lazima yalete faraja na matumaini kwa Watanzania wote na kuhamasisha zaidi ushiriki wao katika hatma ya taifa.
Pamoja na kuapa kuiheshimu, kuilinda na kuitetea Katiba, epukana kabisa na matendo yanayoweza kutafsiriwa kwamba yanapingana na Katiba.
Mh. Rais kumbuka kauli huumba hivyo epukana pia na zile kauli ambazo zinaweza kutafsiriwa na wasaidizi wako kama ruhusa ya kuvunja Katiba.
Hali hii inahusu hasa yale maagizo yanayotolewa papo kwa papo bila kupima yatakavyopokelewa na watendaji wakuu wa vyombo vya dola.
Mh. Rais tuko wengi ambao kuapishwa kwako kulitupa japo faraja kutokana na mizengwe ya awali iliyokuwa ikifanywa na mahafidhina.
Amini usiamini asilimia kubwa ya wananchi bila kujali tofauti zao walipokea mabadiliko ya uongozi wa juu kabisa wa nchi kwa matumaini.
Yawezekana walisukumwa na sababu mbali mbali lakini lililowaunganisha ni uhitaji wa hewa safi kupitia dirisha ambalo ujio wako ungewafungulia.
Ni hilo dirisha lingewezesha kiapo chako kiwe na maana kwa kuturudisha kwenye utawala wa sheria unaoheshimu, kulinda na kutetea Katiba
Ingawa wengi tulikupokea bila kujali unatoka miongoni mwa watu wale wale na chama kile kile, tuliguna kidogo uliposema kazi iendelee.
Kiongozi bora hafuati tu nyayo za aliyemtangulia, hapana, huyo si kiongozi bora, ni mfuasi, kiongozi bora huvumbua njia salama wapite anaowaongoza.
Tafadhali Mh. Rais, acha kupaka ukuta rangi nyumba ipendeze huku msingi una nyufa; shughulikia kwanza msingi nyumba iwe imara na salama.
Tunayo Katiba ya mwaka 1977 lakini cha ajabu ni kuwa hata hii, pamoja na mapungufu yake, tunashindwa kuiheshimu, kuilinda na kuitetea!
Tunayo Rasimu ya Warioba lakini kwako Mh. Samia Suluhu Hassan, hata kuitaja tu imekuwa shida, shida ni nini? Je kuku wetu anataga kwenye miba?
Mwanga uliojitokeza unaanza kufifia ghafla huku safari hatujafika hata nusu, je kulikoni? Chukua hatua na katika kuidai Katiba mpya sahau suluhu.
Shughulikia sheria zote ambazo zinaisigina Katiba kwa namna moja au nyingine kwani tuna kiu kubwa ya utawala unaozingatia haki na usawa.
Ngoja Ngoja yaumiza matumbo na linalowezekana leo lisingojee kesho; kwa kweli baada ya miaka minne ya giza uvumilivu uko mashakani.