Rais Samia mtazame Hannelore Manyanga aliye ndani akihusishwa kwenye sakata la kuingiza stika feki za viza nchini

SautiYaMnyonge

JF-Expert Member
May 13, 2018
439
742
Mhe Rais Samia Suluhu Hassan hongera na pole kwa kazi kubwa na nzuri unayoifanya katika kufungua nchi yetu, kuhakikisha nchi yetu utawala wa sheria na uadilifu katika kila sekta nchini na wananchi kwa ujumla unashamiri huku ukihimiza utatuzi wa kero za wananchi na uwekaji wa mazingira wezeshi kwa uwekezaji nchini. Sisi tunakuelewa na tunakuombea heri ufanikiwe zaidi.

Mhe Rais Mama yetu anaitwa Hannelore Morgan Manyanga alikuwa mkuu wa kitengo cha sheria idara ya uhamiaji akitumikia cheo cha kamishna ila alihusishwa kwenye sakata la kuingiza stika feki za viza nchini zikitokea Afrika Kusini na tangu akamatwe na kuwekwa gereza la Segerea ni zaidi ya mwaka mmoja sasa huku watuhumiwa wenye mzigo wa stika hizo wakiwa waliachiwa huru na mahakama.

Kwa heshima kabisa tunaomba ofisi yako tukufu itusaidie kulitazama faili lake ili haki itendeke kwani mama yetu aliandaa kesi ya hao walengwa ambao baadae waliachiwa kwa mujibu wa sheria. Kwa heshima Mhe Rais tunaomba msaada wako utusaidie mama yetu.

Tunakutakia afya njema.

#KaziIendelee #ZegeHalilali

Screenshot_20210512-192924_1620837035654.jpg
Screenshot_20210512-192935_1620837066038.jpg
 
Pole sana mkuu. Bila shaka atakuwa ni mtu wa maana sana kwako (probably ni ndugu yako) ndio maana ukaja kuandika humu.

Lakini tukisikia na upande wa pili wa walalamikaji (bila shaka ni jamuhuri) ndio tunaweza kujua ni nani yupo sahihi zaidi.

Siku zote katika maisha sio sahihi kufanya maamuzi kwa kusikiliza tuhuma/malalamiko ya upande mmoja tu. inawezekana huyo mama ana hatia au hana hatia.
 
Pole mno na ni mada nzuri hasa zinazomgusa binadamu mwenzetu ambaye anateseka bure maana upo innocent hadi court of law ikutie kwenye hatia, ndio maana nchi inahitaji TAASISI imara zenye kujitegemea sio mpangaji wa paleMagogoni, hope's wahusika watapitia mada yako na kuifanyia kazi let's pray.
 
Pole sana mkuu. Bila shaka atakuwa ni mtu wa maana sana kwako (probably ni ndugu yako) ndio maana ukaja kuandika humu...
Common mkuu hii sio rocket science suala la undugu hapa halina mshiko,huyu ni binadamu mwenzetu mwenye familia kama mimi na wewe,why wamweke jela for a year bila kufikishwa mahakamani na kupata haki yake ya bail?

Ni Mahakama pekee yenye mamlaka ya kumfunga sio vinginevyo
 
Mambo mengine ya Uhamiaji ni kichefu chefu sana. Kamishna kuhusihwa na stika za visa feki siyo jambo dogo ati, una haraka ya nini?
Acheni sheria ifuate mkondo wake ati , UHAMIAJI ni moja ya idara nyeti sana nchini na inayoingiza fedha za kigeni nyingi kwa taifa.

Wizi ukabila na fitina kwenye idara hii umetamalaki sana, mfano idara for the first time kwenye uongozi wa nchi imetoa vijana machachari kwenye nafasi za uwaziri, Dc , DASs na DEDs lakini uhamiaji wamewafukuzilia mbali na kuzuia malipo yao na stahiki zao za uaskali ilikhali wakiwapandisha vyeo vya kijeshi pamoja na nafasi walizonazo.

Kuna watu wanamshauri Kamishna wa uhamiaji vibaya kufuta posho za uaskali za waliopandishwa vyeo na kuwa seconded kwenye idara nyingine za serikali.

Kamishna jitambue na elewa hawa wakirusishwa any time hiyo budget hujaitenga na ni watu wako pia wanaokutangaza wewe na idara nchini.

Wezio police na jeshi wanaendelea na nafasi na stahili zao jeshini. Andengenye ni kamishna wa polisi akitokea kuwa kamishna mkuu wa zima moto nchini. Wewe MAKAKALA jiulize kama zimamoto police na JWTZ wamezuia vyeo, stahili za askali wao. Halafu kuna mtu anataka Mh Rais aingilie watuhumiwa walio jela kuachiwa badala ya kushughulikia masuala ya msingi.
 
Common mkuu hii sio rocket science suala la undugu hapa halina mshiko,huyu ni binadamu mwenzetu mwenye familia kama mimi na wewe,why wamweke jela for a year bila kufikishwa mahakamani na kupata haki yake ya bail?ni Mahakama pekee yenye mamlaka ya kumfunga sio vinginevyo
Sawa mkuu
 
Mambo mengine ya Uhamiaji ni kichefu chefu sana.Kamishna kuhusihwa na stika za visa feki siyo jambo dogo ati, una haraka ya nini?
Acheni sheria ifuate mkondo wake ati , UHAMIAJI ni moja ya idara nyeti sana nchini na inayoingiza fedha za kigeni nyingi kwa taifa...
Kazini/sehemu ya kutafutia rizki kuna changamoto nyingi sana mkuu
 
Kumbe Hadi wateule wa Mhe. Rais aliyepita walikuwa mahabusu kimyakimya! Kamishna kuwekwa ndani Ni Jambo kubwa sana.

Kwa namna mambo yanvyokwenda yaonekana JPM aliwaweka watu wengi ndani ila tulikuwa hatujui.

Lakini kibaya kinachoonekana waliowekwa ndani amri ya mkuu wa nchi wakitoka au wakitetewa hakuna anayekubali kumtaja aliyewaweka ndani Bali tumekuwa tunarusha maneno kwa waliopewa maelekezo.

Semeni adharani kwamba tatizo halikuwa watendaji Bali tatizo lilikuwa ofisi kuu.

Huyu kamishna wa sheria usishangae kukuta yupo ndani si kwa kuhujumu uchumi Bali yupo ndani kwa sababu alipinga maelekezo ya mzee

Pole Kamishna hope mama Samia katika kuliponya Taifa atakuona pia.
 
Kama kuna idara ya kipuuzi na kipumbavu, Uhamiaji ni miongoni mwa hizo idara. Huwa wanajiona wao ni miungu watu. Wanaweza kumvua mtu uraia au kumnyima mtu passport kwa sababu zao za kipumbavu.
 
Back
Top Bottom