Rais Samia: Mikoa ya Kusini watu wanatokwa damu puani na kudondoka. Hatujui ni ugonjwa gani, uchunguzi unaendelea

Influenza

JF-Expert Member
Jul 1, 2018
1,445
3,402

Rais Samia Hassan amesema kuna maradhi ambayo hayakuwepo siku za nyuma lakini yanajitokeza siku za karibuni kwa kuwa uharibifu wa misitu unasababisha Viumbe wa Msituni wasambae kwa Wanadamu

Amesema “Nilikuwa nazungumza na Waziri Mkuu juzi, ametoka ziara Mikoa ya Kusini (Lindi), ameniambia ameona maradhi mapya yameingia. Watu wanatokwa na damu za pua na wanadondoka chini”

Rais anaongeza "Hatujui ni kitu gani, Wanasayansi wamehamia huko kwa uchunguzi zaidi kwa kuwa ni Watu wengi wanaougua kwa mfululuzo, na yote ni kwa sababu tunaharibu makazi ya viumbe kule walikowekwa na Mungu. Tunawasogeza kwetu wanatuletea maradhi”

Rais Samia amezungumza hayo leo, Julai 12, 2022 katika Maadhimisho ya Mkutano wa 20 wa Shirikisho la Mabaraza ya Maaskofu Katoliki ya Afrika Mashariki (AMECEA)
 
Siasa as usual. Ilitakiwa ripoti itoke kwa mabingwa wa afya
Kwaiyo unahisi suala watu kutokwa na damu puani na kuanguka, Ni suala Hadi mabingwa wa afya watoe report? Kwamba Rais hawezi kulisema? Na Rais hajasema Ni aina gani ya ugonjwa, ndiomaana kasema Kuna wataalamu wameenda kuchukua sampuli hili wajue Ni aina gani ya ugonjwa,

Wafuasi wa mwendazake mna chuki na Rais
 
Hujui ni ugonjwa gani, unasababishwa na nini, how it infect human, umeanzia kusini kwetu au imported; lakini tayari umehitimisha chanzo chake ni kuingilia biodiversity ya wanyama pori huna supporting evidence ya virus kuruka kutoka kwa wanyama kwenda kwa binadamu.
 
Watu wa kusini waambiwe ukweli tu kwakweli tuache kuzunguka mbuyu,mambo ya kula panya hapana,wengine wameanza kula hadi mende sasahivi,juzi nimeona kwenye tv kuna nzi wanaliwa
 
Back
Top Bottom