Rais Samia: Mifumo imeanza kuchezewa na kuonesha makasha yamelipiwa na kuruhusiwa kutolewa Bandarini

Yaani huyu bibi daaah, yaani hapo aliposema hapo kwenye hiyo hazara ndo amemaliza !!,hakuna hatua yeyote atakayochukua!!. ukweli ni kwamba ,tunayemuona kwa macho sie ,Ila aliyefichama ndiye!!
 
"...ninazo taarifa za hivi karibuni wafanyakazi wasio waaminifu wamechezea mifumo na kuonyesha mizigo imelipiwa Bandarini na kuruhusiwa kuondolewa ilhali malipo hayajafanyika." Amesema Rais Samia.

My take;

Je, ni rasmi upigaji umerejea kwa kasi namna ile?!

Je, wenye dhamana za uongozi katika taasisi husika hawapaswi kuwajibishwa kwalo?!

Watendaji walio chini ya mkurugenzi wa Bandari wanachezea mifumo na yeye yupo ofisini wa kazi gani?!

Kamishina wa TRA bado yupo ofisini kwa sifa zipi kama ubadhirifu wa kuchezewa mifumo namna ile unafanywa na vijana wake?

Rais analalamikia ilhali yeye ndiye mwenye uwezo wa kuchukua hatua je mimi mlima pareto huku polini nifanyeje?

Inafikirisha!
Suala muhimu ni kuchukua hatua stahiki. Wahusika ama watuhumiwa wanapaswa kusimamishwa kazi ili kupisha uchunguzi. Wizi wa namna hiyo siku zote huwa ni wa kimfumo kwa kuwa unahusisha watu wengi wenye mamlaka ya kuridhia na kuidhinisha hatua moja ifanyike kabla ya kwenda kwenye nyingine inayofuata.

Kwa mantiki hiyo ni kuondoa ama kubalisha vituo wote waliohusika katika hatua mbalimbali za kuyatoa hayo makasha yenye kashfa bandarini. Serikali ni lazima I ya kwamba; "Ukicheka na utavuna mabua"

Badala ya serikali kuhangaika na kutumia vyombo vya dola kuthibiti viongozi wa vyama vya upinzani kwa hofu ya kung'olewa madarakani, itumie vyombo hivyo kuthibiti wizi uliokubuhu serikali.
 
Back
Top Bottom