Rais Samia, mbona kila unaloagiza watendaji wakuu wanakugomea?

Ndugu zetu viongozi waislamu wakishika madaraka ya nchi wanabezwa na kuzarauliwa sana lakini wenyewe uwa wanajifanya waungwana hilo ndio tatizo, Kikwete katukanwa sana na Pengo na wenzake leo anajitokeza kibaka wa sadaka mwenyewe anajiita askofu naye anaanza chokochoko lakini anayetukanwa katulia kama hakuna kilichotokea siamini kama wakati wa Magufuli ingetokea sheikh fulani anademka angebaki salama.
 
Kauli za viongozi kama Mwigulu, Ndugai na Mbunge Gwajima ziko wazi kabisa hawakubaliani na wewe katika yale unayo agiza.

Sio hayo ya miamala na chanjo za corona pekee, lakini kuna jingine kubwa mno ambalo Watumishi waathirika na zoezi la vyeti wanakutazama kwa mshangao.

Ulitoa agizo kuwa watumishi walio ondolewa kazini kwa matatizo ya majina na vyeti ambao walikuwa wanakatwa fedha kupelekwa kwenye mifuko ya jamii walipwe pesa zao kwani ni jasho lao na serikali sio ya kudhulumu haki za watu.

Ulisisitiza hilo ni AGIZO. Lakini watendaji kama kawaida yao Wamedharau na hawajawalipa na wakihoji wanakejeliwa.

Kwa nini wanakudharau namna hii?

Au kwa vile serikali iliyopo hukuiunda wewe bali umeipinduapindua tu?

This is 2021, na hadi 2025 ni mbali mno na utaona ugumu wa kubaki na hawa watu wa mwendazake!
Hata la retention fee naona wamegoma kabisa kulifuta
 
Ulimsikia Ndugai? Hebu tafuta clip yake ya juzi kuhusu miamala kisha linganisha na agizo la SSH.

Ni kama anamuambia ATAKE ASITAKE wameshapitisha

Yeye mwenyewe Rais aliridhia muswada unaohusika ndipo ukawa sheria! Baada ya hapo, sheria haibadilishwi kwa agizo lake tu. Amending or repealing a law follows almost the same process that was followed to enact it!
 
Jiwe alipiga marufuku mikutano ya siasa ya vyama kinyume na Katiba ya nchi kabisa sio hata sheria ya bunge.
Sheria haibadilishwi kwa agizo la Rais. Amending or repealing a law follows almost the same process that was followed to enact it!
 
Kupandisha madaraja ya watumishi kuna maafisa utumishi waliozoea rushwa wamemgomea Mama kuwapandisha watumishi madaraja yao....!
 
Jiwe alipiga marufuku mikutano ya siasa ya vyama kinyume na Katiba ya nchi kabisa sio hata sheria ya bunge.

Mikutano ya kisiasa sio mandatory. Kuruhusiwa au kutokuruhusiwa kwake kufanyika ni function ya circumstances!
 
kuongoza nchi si kazi rahisi.

anapofanya mwenzio ni rahisi sana na kuona kasoro ni rahisi pia.

Mtanikumbuka-JPM
 
Ndio maana nakuambia wewe ni mjinga kila siku.
Once a president, you are not belongs to anybody but Republic uliyoiapia maana huna mtu wa kukupangia la kufanya zaidi ya katiba ya nchi.
Hicho kiingereza kimekaaje?
Ndugu yangu si ungeandika kiswahili tu kuliko kuvunjavunja lugha ya watu.
 
Kauli za viongozi kama Mwigulu, Ndugai na Mbunge Gwajima ziko wazi kabisa hawakubaliani na wewe katika yale unayo agiza.

Sio hayo ya miamala na chanjo za corona pekee, lakini kuna jingine kubwa mno ambalo Watumishi waathirika na zoezi la vyeti wanakutazama kwa mshangao.

Ulitoa agizo kuwa watumishi walio ondolewa kazini kwa matatizo ya majina na vyeti ambao walikuwa wanakatwa fedha kupelekwa kwenye mifuko ya jamii walipwe pesa zao kwani ni jasho lao na serikali sio ya kudhulumu haki za watu.

Ulisisitiza hilo ni AGIZO. Lakini watendaji kama kawaida yao Wamedharau na hawajawalipa na wakihoji wanakejeliwa.

Kwa nini wanakudharau namna hii?

Au kwa vile serikali iliyopo hukuiunda wewe bali umeipinduapindua tu?

This is 2021, na hadi 2025 ni mbali mno na utaona ugumu wa kubaki na hawa watu wa mwendazake!
Sio kila button kwenye remote ni active, zingine sensors zime collapse.
 
26 Reactions
Reply
Back
Top Bottom