Benjamini Netanyahu
JF-Expert Member
- Aug 7, 2014
- 80,083
- 92,518
Hata ndugu zetu albono ni weupeUweupe wenyewe mkorogo
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Hata ndugu zetu albono ni weupeUweupe wenyewe mkorogo
Tena wa hatari arudi kwao ZanzibarHuyu mzanzibara sinitch
Kwani wewe hupo huru mkuu???Labda kwa vile yeye yupo huru anaona kila mtu yupo huru
Soma uelewe mkuu kwanzaKwani wewe hupo huru mkuu???
Wewe akili nyembamba umeona sasa unavyojitia ujuaji? Haya wame-edit vizuri heading umeelewa sasa maana ya maneno yako ya NADHANI na SIDHANI? next time usijifanye mjuajiHii ni maana yako wewe. Siyo ya kisheria kwa mujibu wa Katiba na mamlaka ya DPP. Jitahidi kusoma Katiba
Na bado mtanena sana kwa lugha!Kwahiyo mikutano ya hadhara aliyopiga marufuku ni fujo za kisiasa?!
Hili taifa lina watawala wa hovyo sana...
Yaani Dikteta Uchwara la Kiume linatoka, linaingia Dikteta Uchwara la Kike
Hizi ndio nyuzi za kufutwa daimaNahudhunika sana na suala la binadamu mwenye akili timamu kujitoa ufahamu wake waziwazi kulihusisha suala la mashtaka ya mbowe na masuala ya katiba mpya,maana yake kwa hapa watu wanashindwa kutofautisha jambo gani lilifanyika wakati gani, na jambo lipi lilifanyika wakati upi?so ningeliomba chadema na wapambe wao wao waache upotoshaji wa suala hili na tuzisubiri mahakama zetu tukufu zituonyeshe mlango sahihi maana ndivyo vyombo pekee vya umma vyenye kazi rasmi ya kuuthibitishia umma baada ya malumbano ya mawakili wa pande zote mbili kuumana vilivyo na kuja na jawabu moja yenye vithibitisho mahsusi.
Rais amezungumza vizuri kweli tena kwa uwazi ulio uwazi kwamba shauri hili sio la leo lilikuwepo na bw yule yule alikuwa analifahamu fika na baadhi ya wahusika wa jambo hili walikuwepo rumamnde kwa muda mrefu tu kabla bwana yule hajakamatwa isipokuwa bw yule ni intelegent wa kutisha sana ana akili nyingi sana akaona atafanyaje suala hile alipe mlango au mwonekano mwingine wa ki umma zaidi akaingilia kwa kasi ya katiba mpya bahati mbaya kondoo wake hawajui haya au intelegency aliyonayo kiongozi wao katika kuwatumia vyema koondoo wake, ''Rais amesaema mahakama itatupa majawabu sahihi baada ya mahakimu na wanasheria wa pande zote mbili kukabiliana kwa kina na kuja na jawabu moja tuvute subraaaaaKama kesi ya ugaidi dhidi ya Mbowe alikuwepo mahakamani tangu mwaka Jana kabla ya uchaguzi, Umoja wa Mataifa na watetezi wa haki za binadamu wanasubiri nini kuitangaza Tanzania kuwa nchi inayoongoza duniani kwa "Ustaarabu wa Kijinai?"
Maana hakuna nchi duniani ambayo ingeweza kumwacha anatamba mitaani mtuhumiwa mkuu wa votendo vya ugaidi na kuua viongozi. Yaani tuseme viongozi wa Tanzania walikuwa tayari wauawe na GAIDI huku wakichekelea lakini hawako tayari kuona Mtanzania akienda mahakamani kusikiliza kesi dhidi ya GAIDI huyo? Inachukua mwaka mzima kumkamata GAIDI lakini haiishi hata sekunde kumkamata mwananchi aliyekwenda Kisutu kusikiliza kesi dhidi ya GAIDI huyo?
UN, Amnesty nk mnaionea gere Tanzania, itangazeni mara moja kuwa nchi bora katika Ustaarabu wa kijinai.
Narudia...Na bado mtanena sana kwa lugha!
Si mlikuwa mnademka humu eti hoo sasa tunapumua, tuko huru, tulibanwa sana!
Wenye akili tuliwambia huo ni mfumo na si matakwa ya mtu binafsi, na bado
Anyway.. Mama anafungua nchi,
Mama anawakomesha mataga na sukuma gang
Mama anarudisha hela mtaani ili sisi mibavicha tuwe tunaziokota
Uchumi uko juu, mafuta bei chini, bidhaa muhimu bei sawa na bure.
Bashiru na Polepole wanakiona cha moto
Duh! Unamtuhumu mtu kwa ugaidi tokea mwaka jana na unamuachia achanje mbuga!!!!!Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan amesema hawezi kuzungumzia kesi ya kiongozi wa chama kikuu cha upinzani- Chadema- Freeman Mbowe ambaye anakabiliwa na mashtaka ya ugaidi.
Katika mahojiano maalum na mwandishi wa BBC Salim Kikeke, Rais Samia amesema ana imani sheria itachukua mkondo wake.
Wafuasi wa Bwana Mbowe wanadai kuwa mashtaka haya yamechochewa kisiasa.
Aidha katika suala la demokrasia na uhuru wa kujieleza Rais Samia Suluhu Hassan amesema watu wana uhuru wa kutosha.
BBC
---
UHURU WA KUJIELEZA
Kikeke: Tanzania unayoingoza sasa hivi ina Uhuru wa Kujieleza na Demokrasia ya kutosha?
Rais Samia: Ahaaha! Wewe ni mwandishi wa habari toka umefika umesikia vyombo vya habari vimelalamika? Hakuna chombo kimelalamika kuna uhuru wa kutosha wanajieleza, na wanajieleza mpaka wanavuka mipaka saa nyingine. Lakini kwasababu viongozi inabidi mvae ngozi ngumu muangalie.
Lakini wakati mwingine kusema kwao bora umpe nafasi mtu a-offload alichonacho atoe umsikie kama kiongozi useme kumbe kinalalamikiwa hiki, basi unakifanyia kazi kuliko ukiwabana hawasemi, hujui wanafukuta na nini ndani, ile! Sasa Tanzania kuna uhuru wa kutosha, vyombo vyote vya habari viko huru, anayefuata sheria, anayefuata maadili ya kazi yao wako wanafanya kazi yao.
DEMOKRASIA
Kikeke: Demokrasia ya Kisiasa?
Rais Samia: Demokrasia ya Kisiasa, Yes ipo. Na hapa naomba nitofautishe baina ya Demokrasia ya Kisiasa na fujo za kisiasa.
Demokrasia ya Kisiasa ni nini? - Demokrasia ya Kisiasa tuna vyama vya Siasa, wana vyombo vyao, wanajadili mambo yao kwa mfano baraza la vyama vya siasa. Huko wanajichagua wao, wanajadili mambo yao ya kisiasa wanaelewana. Kuna kamati ya vyama vyenye wabunge Bungeni na wenyewe wana ya kwao, wakakaa wanazungumza wanajadiliana huko. Lakini kuna vyama vyenyewe vya siasa ambavyo vimeundwa na Katiba zao, na kwenda kwao au kufanya kwao kazi kunategemea katiba zao.
Kwa mfano chama changu cha Mapinduzi, Katiba yangu inaniambia labda katika mwaka nitakuwa na vikao viwili vya Halmashauri Kuu ya Chama, Labda Vikao 6 vya Kamati Kuu na vikao vingine katika ngazi za chini Mikoa na Wilaya. Na hivyo vikao vimeelezea wajumbe ni wakina nani na kila kitu. hivyo Vikao vinaendeshwa bila bugudha bila kuomba ruhusa polisi kwasababu Katiba imeshaelezwa na imeshapita kote na inajulikana. Na vivyo hivyo vyama vingine vyote vina katiba zao, zina system zao za Mikutano, wajumbe wao ni kina nani, hivyo wako free kufanya wakati wowote.
Kitu ambacho hakipendezi ni ile kutaka uhuru wa kufanya fujo za kisiasa, labda tumemaliza uchaguzi, Serikali imeundwa. kinachotakiwa kuendelea ni kujenga nchi uwe na chama gani wote mnakuja pamoja mnajenga nchi yenu, ndicho kinachotakiwa kuwa.
Lakini kinapotokea chama, wao wanataka tu kuitisha maandamano kila siku, maandamano yasiyo mwisho, sijui maandamano nini, labda leo mkutano huko, kesho mkutano huko fujo vurugu, aaah ile
Kikeke: Ndio Uhuru wa Demokrasia
Rais Samia: Hapana, kama uhuru wa Demokrasia mbona Marekani hawa-observe, mbona Ulaya hawa-observe? Wakimaliza chaguzi ni kimya, wanaendelea shughuli zao za maendeleo, nchi inapewa nafasi inafanya kazi zake wanajijengea nchi zao. Hatujasikia vurugu za kila siku za huko Marekani na Ulaya, kama kutatokea maandamano ni Constituency ndogo wamekosa umeme jana na juzi umeme umekuja low Voltage wanaandamana mtaa huo wanakwenda kwa huyo mwenye umeme huko, wanasema ya kwao wanarudi peacefully. Sasa haya ya kwetu ya vurugu, piga magari, choma.. ah aha
KESI DHIDI YA FREEMAN MBOWE
Kikeke: Nazungumzia suala hilo la kisiasa kwa sababu kiongozi wa upinzania Freeman Mbowe amefikishwa Mahakamani, amefunguliwa mashataka ya Ugaidi, wananchi wake wanasema mashtaka haya yamechochewa kisiasa
Rais Samia: Mimi sidhani kama yamechochewa kisiasa kwasababu navyojua Mbowe alifunguliwa Kesi mwezi wa Tisa mwaka jana (2020), kwa hiyo yeye pamoja na wengine na kama ulivyosema mashtaka ni ugaidi na kuhujumu uchumi. Nadhani wenziwe kesi zao zimesikilizwa na wengine wameshapewa sentence zao wanatumikia. Yeye (Mbowe) upelelezi ulikuwa haujeisha, uchunguzi ulikuwa unaendelea so amekwenda amefanya tumeingia kwenye uchaguzi, amemaliza uchaguzi nadhani sasa Polisi wamekamilisha uchunguzi wao, wamemuhitaji waendelee na kazi yao, Lakini kwa sababu na kama utakumbuka Mbowe hakuwepo nchini alikuwa Nairobi, sasa kwanini kakimbia sijui. Lakini alivyoingia tu nchini Kaitisha maandamano ya Katiba na madai ya katiba. Nadhani ni Calculation akijua kwamba ana kesi ya aina hiyo na hii vurugu ambayo ana-instigate akikamatwa aseme mmhh! kwasababu ya Katiba, kwasababu tumeitisha Katiba... nadhani sina hakika.
Lakini kwa sababu jambo liko mahakamani, sina uhuru wa kulizungumzia kwa sana. Nadhani tuache Mahakama zioneshe ulimwengu kwamba hizo shutuma walizomshutumu zilikuwa za kweli au siyo za kweli Mahakama itaamua.
KUKUTANA NA WAPINZANI
Kikeke: Na Katika Suala hilo hilo la Siasa za upinzani, ulivyoingia madarakani ulisema uko tayari kuzungumza nao na hata Mbowe alikuwa anauliza ni lini utakutana naye, lini utakutana na viongozi wa upinzani?
Rais Samia: Nimesema nitakutana nao lakini sikutana kukutana nao wakiwa wamechambuka chambuka, kama nilivyokueleza hawa watu wana vyama vyao vidogo vidogo, wana mabaraza yao. Nilitaka kwanza wajiunge kwenye mabaraza yao. Na Baraza la Demokrasia nadhani la Vyama vya siasa wamefanya uchaguzi wiki mbili zilizopita au wiki iliyopita ndio wamejiunda vizuri. Kwa hiyo kama wamejiunga vizuri, na hizi kamati zao ndogo ndogo zimejiunda vizuri, basi tutatafuta tu siku tuitane tukae tuzungumze kwasababu hata mimi nataka kuzungumza nao niwaambie mwelekeo wangu kwamba sasa tumemaliza uchaguzi twendeni tukajenge nchi.
Na kwenye kujenga nchi mimi sichagui, nikimuona mpinzani amekaa vizuri ana mwelekeo namuweka kwenye serikali yangu twende tukajenge nchi kwasababu hakuna pahala pamesema baada ya uchaguzi chama kilichoshinda peke yake ndicho kitajenga nchi, hapana.
Tumesema watanzania tutajenga nchi. So Mtanzania yeyote mwenye ideology yoyote ya kisiasa kama ni mzuri anaweza ku-deliver na kuleta yale ambayo wananchi wanataka mimi namtumia tu, namuingiza kwenye system zangu tu twende namtumia
Kwa hiyo nataka waje tukae tuone tunakwendaje na hili, kwa hiyo wakati ukifika nitawatafuta, nitawaambia karibuni njooni tukae.
Labda kwa vile yeye yupo huru anaona kila mtu yupo huru
Mpuuzi wewe unaongea nini! kaa kwa shemeji yako hukoUkifuata mipaka yako ya kujidai na kujimwayamwaya siku zote utakuwa huru.
Ngoja nikupe mfano, hata kwako huwezi kuwa huru kama umeamua ucheze na mkeo ndombolo huku mmevaa kaunda suti zasiku ya kuzaliwa sebuleni. Hata kama ni baba house, lazima uhuru hautakuwa nao. Uhuru bila mipaka ni fujo. Au wazia kila mtu barabarani anajihisi huru na kuamua kuendesha upande au site yoyote, je barabarani kutakuwa na USALAMA??