Rais Samia: Majirani zetu wanazo The so called 'Tume Huru', hawana migogoro? Auliza nini kinafatwa kwenye tume huru

Mimi sitaki tume huru wala katiba mpya.

Nataka watu waelimishwe kwanza wajitambue kabla ya kuvipata vyote hivyo.

Hakuna tija ya kuwa na vifaa vipya kabla ya kujifunza kwanza kuvitumia.

Tuondoane ujinga kwanza ndio twende huko.
Kwani ile task force iliyokua inakwapua fedha za watu kwenye account na maduka ya kubadilishia fedha za kigeni ilianza kutoa elimu kwanza.

Ukweli ni kuwa kwa tume hii ambayo ni favourable kwa CCM hawawezi ikubali ibadilishwe imagine yule Mahera kada wa CCM ndio mkurugenzi wa tume na bila aibu mnamleta awe mgeni rasmi wa hiyo TCD.

Ndio maana hata Bashiru alikua bold enough kusema watashinda uchaguzi 2020 kwa msaada wa dola na ndio kilichotokea mkasema mmeshinda kwa kishindo na matokeo yoyote ya ngazi hiyo mmeyapiga ban kutohojiwa kortini.

There is no any means for CCM to sanitize the evils of the current regime.
 
Mama anaweweseka. Anajua hawezi kushinda urais wa Tanzania kwa haki...

Kura za kwenye vikapu lazima zitumike na hakuna kupinga matokeo mahakamani!!
Kwahiyo kumbe lengo kubwa la Tume huru ya uchaguzi na Katiba Mpya Ni kushinda uchaguzi🤣🤣🤣
 
Namkubali Mama lakini naona kuna maeneo kama ana U-mbogamboga badala ya kukaa nyutro akaishepu nchi,dawa ya kuondoa malalamiko ni kutia kinachodaiwa,mambo mawili huwa mbogamboga hawayakubali na huenda hawatayakubali kitahisi ni TUME HURU NA KATIBA MOYA KABISA,siyo iliyokarabatiwa.

Haoa Mama atupatie vyote viwili,awe na legacy yake.
ukisikia UWEZO WAKO NDIO ULIPOISHIA ndio hizo kauli za mama. Yaani hapo ndio SKY
 
Tume huru isipoendana na Katiba inayo wezesha tume huru kuwa tume huru tutakuwa hatujafanya kitu. Lingine la muhimu ni kuwa na viongozi na wananchi wapenda na wapigania HAKI.
 
Nashangaa mbona yeye ndie anakuwa kikwazo cha upatikanaji wa hiyo Tume Huru? anyway wengine hatutaki Tume Huru tunataka Katiba Mpya.

Halafu kama hajui maana ya Tume Huru kwanini asiulize akajibiwa kuliko kujitokeza hadharani na kuanza kutoa kauli zitakazoleta sintofahamu?

Vipi Zitto hawezi kumuelewesha rafiki yake kwenye hili?

Huyu Rais kama walivyo CCM wenzake hawana nia ya dhati ya kutupa Katiba Mpya wala Tume Huru ya uchaguzi, yote yanayoendelea kuunda timu zao za vikosi kazi vya uongo ni maigizo matupu, wananchi tusipoamua tutasubiri sana.
Tume inaongozwa na Hamad Rashid, apo ni usanii mtupu. Labda anadhani wananchi hawana uwezo wa kuchambua na kufahamu. Hata mie nisie na elimu kubwa ya sheria bado nina uwezo wa kujua mabadiliko yana usanii au ni mabadiliko ya kuchenguana.

Samia hadi sasa hana tofauti na watangulizi wake sarakasi, my basic definition sioni momentum ya mabadiliko ya sheria. Sheria ziko vile vile watu wanapiga soga na kujitokeza na vigurupu kazi.
 
Huenda kuna mambo yanakuchanganya sana kwenye demokrasia, wewe ni cynic wa kiwango cha juu, unafanya strawa man fallacy au appeal to extreme fallacy, lakini fahamu.

Hakuna kitu au mfumo perfect duniani,

Hakuna gari, ndege, treni,meli, rubani na dereva perfect lakini hiyo haiwafanyi binadamu rational wanaoweza kupata huduma za gari n.k kuendelea kutumia punda na farasi wakati huu.

Hakuna madaktari au dawa perfect lakini hilo halizuii watu kusisitizwa kwenda hospitalini zaidi badala ya kung'ang'ania mitishamba na waganga wa kienyeji.
Mifano iko mingi.

Ni uzwazwa na counterproductive kila mara watu wanapojaribu kuboresha jambo au hali halafu kuna mtu yeye anajaribu kuonyesha hakuna kitu perfect ili hali hakuna hata mtu mwenye madai hayo kwa kuanzia.
Huenda hao wana So called Tume Huru ila hawa Tume Huru

In short hata iliyopo duniani ni so called demokrasia lakini sio demokrasia ya kweli...

LAKINI..., faida ya hivi vitu ni kama wenzetu wanasheria wanavyosema -
Justice should not only be done but should manifestly and undoubtedly be seen to be done”.

Kwahio watu wakiona kwamba TUME ni huru hata malalamiko / sababu / excuses zitapungua hence huenda tukahamia kwenye malalamiko na Kero nyingine..., ila sababu ya kwamba fulani ingawa anacho hiki ila analalamika sio mtaji wa kutokufanya hilo jambo...

KAMA Tume sio Huru kwanini tuendelee kuwanayo ? Si bora isiwepo kabisa hili hivyo vijisenti vikafanye mengine ?
 
Huenda kuna mambo yanakuchanganya sana kwenye demokrasia, wewe ni cynic wa kiwango cha juu, unafanya strawa man fallacy au appeal to extreme fallacy, lakini fahamu.
Nani kasema mimi ni cynic wa demokrasia..., faida moja kubwa ya demokrasia ya kufanya watu waridhike na kutokufanya fujo au kulalamika is the price worth paid..., ila haimaanishi tuseme kwamba kinachopatikana katika muundo na utendaji ndicho kilicho kwenye theory..., democracy has its pros and cons kila mtu anajua ila hatuwezi tukabadilisha cons na kusema ni pros sababu tu its the best way of ruling....
Hakuna kitu au mfumo perfect duniani,
Nani kasema upo ?
Hakuna gari, ndege, treni,meli, rubani na dereva perfect lakini hiyo haiwafanyi binadamu rational wanaoweza kupata huduma za gari n.k kuendelea kutumia punda na farasi wakati huu.
Je inamaanisha huyo dereva asiendelee kupata mafunzo ya mara kwa mara au kuangalia kama anaweza kuboresha anachofanya.
Hakuna madaktari au dawa perfect lakini hilo halizuii watu kusisitizwa kwenda hospitalini zaidi badala ya kung'ang'ania mitishamba na waganga wa kienyeji.
Mifano iko mingi.
Kwahio doctors kila siku hawa-perfect their trade ? To perfect and look better ways ndio development, haimaanishi tuseme sababu demokrasia its not really power to the people haimaanishi turudi kwenye aristocracy hapana bali ni jinsi gani tunaweza tukamuwezesha mwananchi zaidi kwenye decision making
Ni uzwazwa na counterproductive kila mara watu wanapojaribu kuboresha jambo au hali halafu kuna mtu yeye anajaribu kuonyesha hakuna kitu perfect ili hali hakuna hata mtu mwenye madai hayo kwa kuanzia.
Hakuna Demokrasia ya kweli mpaka sasa thriving to reach that goal is the way to go..., Sasa ni Uzwazwa kusema tumefika wakati hatujafika sababu hapo hauwezi kuboresha....

Without knowing or admitting there is a problem how can one solve such problems ? Wewe una-thrive ili uwe kama USA, Canada na Ulaya mimi nakwambia even theirs is not perfect and can be perfected..., which means am thriving for something better than theirs.....
 
Inatakiwa Tume huru yenye uhuru kamili, na siyo uhuru isiyo na uhuru kama ile ya Jecha.
 
Ikiwa default setting ya mifumo ya tawala za kibinadamu ni uimla(autocraticism), kivipi demokrasia in it's purest form inaweza kuleta shida kama hizo za tyranny of majority? Kwamba kwenye autocraticism minority rights zina uhakika wa kuheshimiwa sana AU ulimaanisha demokrasia bado inaweza isiziondoe hizo shida?

Madhara ya Lobbying za interest groups na blah blah nyingine ulizozitaja hapo chini ni malalamiko yako tu(ambayo ni petty) dhidi ya mifumo ya demokrasia , sio kila mtu anaona Lobbying za makampuni/wafanyabiashara (kwenye kodi, udhibit , mazingira wezeshi n.k), Lobbying za vyama vya wafanyakazi n.k ni mbaya.
Naamisha decisions....
Matakwa na mahitaji ni moja ya shortcomings za democracy sababu kuna kitu kinaitwa the Tyranny of the Majority... ukizingatia sio kila kinachosemwa kinachopendwa na wengi ni sahihi..., hivyo demokrasia even in its purest form inaweza ikaleta shida hizo..., ila hapa naongelea decision making (uchaguzi wa kipi kifanyika na opportunity ya kila mmoja kufanya hivyo)

wote watakuwa wamefanya decisions sababu wote wame-vote na walioshinda ndio hivyo inabidi wapewe (ni watu ndio wamechagua)

Ila in real sense what happens kwenye representative democracy lobbyist wanaongea na wale few decision makers wanawashawishi whichever they want to pass and it will pass (be voted upon by the few); na kama wale wabishi wanaokwenda kinyume usishangae next election wakapigwa chini sababu ya wenye pesa ku-back their own candidate mwenye matakwa yao... Mbaya zaidi in most countries even the wanaokuja kugombea kushindanishwa ni wateule wa Chama Fulani (hence mpiga Kura / mtaka muwakilishi huenda hata katika choice hakuna chaguo lake)
 
Jibi swali na ikiwezekana jenga hoja...

Hoja ya mama ipo hapa, nini maana ya tume huru na je tufanyaje ili tume huru yetu kweli itatue matatizo maana zipo nchi zilitumia muda mwingi kuunda na kutafuta tume huru na katiba pia, lakini hizo nchi mpaka leo bado zina matatizo kwenye chaguzi na hiyo Katiba...

Nimekusaidia kudadavua, tujaribu kuwa positive ili kupata tiba ya matatizo yetu...
Mtu yeyote anayehisi hatuhitaji mabadiliko ya katiba Kama nchi ni MSALITI lazima tuweke baadhi ya vitu sawa. Hatutakiwi kuwaza Leo tu huo ni ubinafsi watu wanatetekeza mali za umma, watu wanatumia Nafasi zao vibaya wananchi hatuna chakuwafanya wote tunasubiri Rais ndo aamue this is not fair. Siungi mabadiliko ya katiba kwa sababu ya CHADEMA ila ni kwa mapenzi tu ya Taifa langu TANZANIA.
 
Rais Samia akiwa anapokea ripoti ya kikosi kazi alichounda ameongelea Tume huru ya uchaguzi na kuhoji uwepo wa kuendelea migogoro kwenye nchi za jirani zinazotajwa kuwa na tume huru.

Rais Samia ametaka kujua 'Definition' ya tume huru na ipi kiu itakayopatikana kwenye tume huru.

======

Samia Suluhu: Tume huru hizo na nini mtatulete mapendekezo, tume huru maana yake nini!

Iweje? Lakini angalieni na mifano ya waliokuwa na tume huru, Je hawana migogoro ya kisiasa? The so called 'Tume Huru'.

Kwa mfano majirani zetu wanazo The so called 'Tume Huru' lakini zinaendeshwaje? Hawana migogoro? Hawatangazi matokeo wakakimbia nchi kabisa?

Si hutangaza matokeo kisha wakakimbia! Nendeni nchi mbalimbali zenye hizo zinazoitwa tume huru, angalieni yanaendaje lakini tunaposema tume huru tunafata nini hasa huko kwenye tume huru.

Kitu gani kinatupa kiu tunahisi tutakipata kwenye tume huru huko na definition hasa ya tume huru ni nini?

===

Kuhusu maboresho ya sheria na kanuni za Uchaguzi, Rais Samia amesema watasema vipengele gani vinavyouma kwani inawezekana maboresho yakifanyika, kelele ya katiba inaweza ikaishia kwasababu zile kiu za watu zinapotaka katiba ibadilishwe ilishafanyiwa kazi.

PIA, Soma=> Ikulu, Dar es Salaam: Rais Samia apokea taarifa ya Kikosi Kazi cha Kuratibu Maoni ya wadau wa Demokrasia ya Vyama vingi vya Siasa
Kinachomfanya aogope tume huru sio migogoro ila kupoteza nafasi. CCM ni waoga sana kwenye kupoteza madaraka ya nchi maana wanajua uchafu wao huko ni mwingi na hawana uhakika atakayekuja kama atawaacha salama.
 
Mtu yeyote anayehisi hatuhitaji mabadiliko ya katiba Kama nchi ni MSALITI lazima tuweke baadhi ya vitu sawa. Hatutakiwi kuwaza Leo tu huo ni ubinafsi watu wanatetekeza mali za umma, watu wanatumia Nafasi zao vibaya wananchi hatuna chakuwafanya wote tunasubiri Rais ndo aamue this is not fair. Siungi mabadiliko ya katiba kwa sababu ya CHADEMA ila ni kwa mapenzi tu ya Taifa langu TANZANIA.
Wasiohitaji mabadiliko au katiba mpya ni wale wanufaika wa katiba iliyopo. Huwezi amini samia aliyekuwepo kwenye bunge la katiba 2014 eti leo anajifanya hamnazo na kudharau takwa hili kisa yupo madarakani.
 
Maana-Chombo free kitakachosimamia shughuli za uchaguzi na utangazwaji wa washindi.....Je ikiwa upinzani wamewahi kukiri kuwa; baadhi ya makada wake yenyewe, wakiwamo wenye nyazifa za juu; kununuliwa na CCM, hawatailalamikia tume hiyohiyo kuwa imehongwa na ccm? siku mambo yakiwa tofauti? coz being free sio kigezo cha kutohongeka.
 
Mtu yeyote anayehisi hatuhitaji mabadiliko ya katiba Kama nchi ni MSALITI lazima tuweke baadhi ya vitu sawa. Hatutakiwi kuwaza Leo tu huo ni ubinafsi watu wanatetekeza mali za umma, watu wanatumia Nafasi zao vibaya wananchi hatuna chakuwafanya wote tunasubiri Rais ndo aamue this is not fair. Siungi mabadiliko ya katiba kwa sababu ya CHADEMA ila ni kwa mapenzi tu ya Taifa langu TANZANIA.
Fikiria hizo ni kauli za mkuu wa nchi. Maana yake Mkuu wa Nchi haifikirii Tz ya kesho anawaza CCM Vs Chadema tu
 
Back
Top Bottom