JanguKamaJangu
JF-Expert Member
- Feb 7, 2022
- 2,308
- 5,456
“Tulichofanya ni kuwatoa magereza yakapata kupumua, msipofanya haki, mnapochukua rushwa kumtia mtu hatiani ambaye hana hatia na mwenye hatia mkamuacha nje anaendeleza ubabe akiamini pesa yake itambeba, ambaye hana hela anaishia jela.
“Usiangalie Duniani, umechukua fedha sawa, imekufanya umekuwa nani, imekufikisha wapi, matatizo yako ya Dunia yameisha, ni ushawishi tu wa akili, itendeeni haki sheria.”
Amesema hayo Novemba 24, 2022 alipokuwa akizungumza katika ufunguzi wa mkutano wa wanasheria wa 27 Afrika Mashariki unaofanyika Jijini Arusha.