PostGE2025 Rais Samia: Lililotokea halikuwa jema kwa yeyote lakini walivyokamatwa kama mama nikasema waachieni. Yaliyotokea yametia doa kwenye Taifa letu

PostGE2025 Rais Samia: Lililotokea halikuwa jema kwa yeyote lakini walivyokamatwa kama mama nikasema waachieni. Yaliyotokea yametia doa kwenye Taifa letu

Conversations and stories after Tanzania's 2025 General Elections

McLaren

JF-Expert Member
Joined
Feb 19, 2025
Posts
993
Reaction score
3,152
Rais. Samia Suluhu Hassan, akizungumza na Wananchi wa Mkoa wa Dodoma, tarehe 08 Mei, 2026 amesema matukio yaliyotokea nyuma hayakuwa na manufaa kwa mtu yeyote na yalisababisha vijana wengi kuingia kwenye matatizo kwa kufuata mkumbo bila kuelewa madhara yake.

"Nililolotokea nyuma halikuwa jema kwa yeyote yule. Na mtego ule anaingia aliyekuwemo na asiyekuwemo... Kumbukumbu lile lilikumba vijana wengi sana na wengi waliingia kwa kutokujua kwa mkumbo. Lakini walivyokamatwa kama mama nikasema waachieni... waachieni watajifunza."

"Niwaombe sana vijana... katika vijiwe vyenu, katika kazi zenu, katika shughuli zenu zote, ambizaneni yasitokee tena. Yale yaliyotokea yametia doa kwenye taifa letu. Tanzania ni nchi ya amani, hayajawahi kutokea yale."

"Sasa tuonyeshe ulimwengu kwamba yaliyotokea si ya Kitanzania na si Utanzania. Ni mambo ya kupandikizwa yaliyotokea. Kwa hiyo sasa tuonyeshe ulimwengu, na nawashukuru mmesema hapana tena, Never Again, hatutaki kuyasikia."


 
siipendi ccm ila ni ujinga sana kuandamana eti kisa tume ya uchaguzi iwe huru.....siwezi kuandamana kwa matatizo ya ujumla ya watanzania...nimezaliwa nikasoma nikapata kazi nikapata mke na familia,pombe nakunywa,nyama nakula,mapenzi nafanya eti niingie barabarani kuandamana kisa tume ya uchaguzi iwe huru..never never ...maisha ni zaidi ya siasa
 
wewe unajua kabisa barabarani sio shwari unajipelekaje barabarani ni sawa na sasa hivi itokee vita halafu we unajipeleka maeneo ya public wakati unachotakiwa kufanya aidha ukajifiche porini au uchimbe handaki....akili ni kitu cha kutumia DR HAYA LAND
 
siipendi ccm ila ni ujinga sana kuandamana eti kisa tume ya uchaguzi iwe huru.....siwezi kuandamana kwa matatizo ya ujumla ya watanzania...nimezaliwa nikasoma nikapata kazi nikapata mke na familia,pombe nakunywa,nyama nakula,mapenzi nafanya eti niingie barabarani kuandamana kisa tume ya uchaguzi iwe huru..never never ...maisha ni zaidi ya siasa
Khuma wewe, kwa sababu unakula nyama na kut°mba unawaona wanaotekwa, kutatwa vichwa na kudhulumiwa haya kuhusu? Kwa ufupi hujasoma umesomewa, mimi nimesoma na nilichokisoma kuna uwezekano ukoo wako hakuna aliyekisoma na ninakipato ila barabarani nilikuwepo na nitaendelea kuwepo kikinuka mpaka tuelewane.
 
siipendi ccm ila ni ujinga sana kuandamana eti kisa tume ya uchaguzi iwe huru.....siwezi kuandamana kwa matatizo ya ujumla ya watanzania...nimezaliwa nikasoma nikapata kazi nikapata mke na familia,pombe nakunywa,nyama nakula,mapenzi nafanya eti niingie barabarani kuandamana kisa tume ya uchaguzi iwe huru..never never ...maisha ni zaidi ya siasa
It is true ,,ila Kuna wengine kamwe siasa ndo maisha, ni kama mtunisia aliyejichoma moto wewe huwezi ila wengine wanaweza
 
siipendi ccm ila ni ujinga sana kuandamana eti kisa tume ya uchaguzi iwe huru.....siwezi kuandamana kwa matatizo ya ujumla ya watanzania...nimezaliwa nikasoma nikapata kazi nikapata mke na familia,pombe nakunywa,nyama nakula,mapenzi nafanya eti niingie barabarani kuandamana kisa tume ya uchaguzi iwe huru..never never ...maisha ni zaidi ya siasa
Polepole 2019 ungemwambia kuna siku utatekwa angekataa.. Lakini si umeona kilichotokea hapo 2025?

Ni suala la muda hata hizo pombe utaziona chungu ukipewa unywe, hata mkeo akae mtupu hutosimamisha.
 
siipendi ccm ila ni ujinga sana kuandamana eti kisa tume ya uchaguzi iwe huru.....siwezi kuandamana kwa matatizo ya ujumla ya watanzania...nimezaliwa nikasoma nikapata kazi nikapata mke na familia,pombe nakunywa,nyama nakula,mapenzi nafanya eti niingie barabarani kuandamana kisa tume ya uchaguzi iwe huru..never never ...maisha ni zaidi ya siasa
Ulipo wewe sio walipo walioandamana, nyerere alitaka uhuru wa nini wakati tayari alikuwa mwalimu na mshahara anakula? Think outside the box
 
Ila watu kutekwa sawaaa
hivi ukitulia ukafanya kazi zako ukapata pesa hata kama kidogo ukaenda sokoni ukanunua vyakula ukarudi nyumbani mkala mkanywa na bia mambo ya serikali ukaawachia wenyewe nani atakuja kukuteka...serikali ni kama mashine ya kusaga ukijiingiza kwenye mashine utasagwa...ni kama kuchezea kiwembe...

jiulize kwanini wauza madawa hawakutafuti wakuue?kwani hawana uwezo wa kukuua?ni kwa sababu hujawaingilia kwenye mambo yao...mbona simple tu ...
 
Ulipo wewe sio walipo walioandamana, nyerere alitaka uhuru wa nini wakati tayari alikuwa mwalimu na mshahara anakula? Think out the box
nyerere alitaka uhuru wapi,,watu ndio walitaka uhuru na mwingereza alikuwa tayari kuachia watu uhuru nyerere alikuwa akifanya majukumu yake
 
siipendi ccm ila ni ujinga sana kuandamana eti kisa tume ya uchaguzi iwe huru.....siwezi kuandamana kwa matatizo ya ujumla ya watanzania...nimezaliwa nikasoma nikapata kazi nikapata mke na familia,pombe nakunywa,nyama nakula,mapenzi nafanya eti niingie barabarani kuandamana kisa tume ya uchaguzi iwe huru..never never ...maisha ni zaidi ya siasa
Akili za kindezi kweli kweli.. pun intended
 
Back
Top Bottom