peno hasegawa
JF-Expert Member
- Feb 24, 2016
- 12,806
- 21,408
Leo Samia amefanya kosa kubwa sana kwa kitendo chake cha kujibu mashambulizi kwa Ndugai.
Hii mbungi ya Ndugai ndo ilikuwa chance kubwa ya mama kuwajua maadui zake kwa kirefu.
Mama angepaswa kuwa soft kabisa kwa siku ya leo. Na ingependeza kama angeanza kumshukuru kwa dhati Ndugai kwa kuomba msamaha.
Imagine kama angeongea haya maneno leo "Namshukuru sana kaka yangu Ndugai kwa kuonesha ukomavu na kurekebisha kauli yako ili tuendelee kujenga taifa la umoja na mshikamano"
Hivyo ndivyo mama angepaswa kusikika leo. Diplomatically and soft tone. Hii ingemfanya hata Ndugai aone kama amesamehewa kirahisi.
Hiyo maana yake ni kumpa adui false signal, halafu sasa akishajaa kwenye comfort zone, ndio unafanya severe atacks.
Kwa case kama hii, Samia amgeweza kuwa soft sana kama nilivyosema hapo mwanzo halafu baada ya kama wiki mbili au tatu mambo yakishapoa, ndio anafanya fujo za kuvunja baraza la mawaziri ikifuatiwa na taratibu za Ndugai kuvuliwa u spika.
Sasa kwa hii move ya kukunjua makucha asubuhi na mapema, maana yake ni kama ametangaza vita wazi wazi na kambi ya kina Ndugai kitu ambacho kwangu mimi tayari ni udhaifu kwa sababu sasa Ndugai ni kama naye hawezi kutulia tu hivi abondwe, lazima atataka kujibu mashambulizi na kurejesha nguvu yake hata ingekuwa mimi.