Rais Samia kwenda Zambia na Kikosi cha Viongozi mbalimbali wa CCM Je, ni mkakati wa kujenga Urafiki na kilichokuwa chama Pinzani?
Leo Rais Samia anatarajia kuondoka nchini kuelekea nchini Zambia kuhudhuria sherehe za kuapishwa Rais mpya wa nchi hiyo Hakainde Hichilema , miaka yote tumezoa Rais kuondoka na viongozi wachache wa Serikali lakini hii ya leo ni kama mpya juu ya msafara mkubwa uliobeba viongozi wa kichama zaidi kwa lengo la kuhudhuria sherehe za kuapishwa.
Viongozi wa CCM wanaoambatana na Rais ni pamoja na Naibu waziri mambo ya nje , Katibu NEC, Itikadi na Uenezi , Katibu Idara ya Oganaizesheni CCM, Waziri Mkuu mstaafu , Mjumbe wa Kamati Kuu CCM, ni kama maajabu safari hii imembeba mpaka Mbunge Comedian wa jimbo la Mtera.
Rais kuambatana na kikosi hiki inaonekana kuna ajenda maalum wanaenda kuiseti , mana serikali hii ni mpya na imeingia madarakani kwa mateso kupitia vikosi vya ulinzi ikiwemo jeshi la polisi wakati huohuo huku Tanzania kupitia utawala wa enzi za mwendazake ulisaidia mbinu mbalimbali za kumnyanyasa mzee Hichilema, sasa naona CCM wanaenda kuweka mambo sawa kwa kujinasibu kuwa kwasasa ni serikali nyingine sio ile.
Vyama vya upinzani nchini na nyie mchangamke msilale lale muwe na plan zaidi ya moja wakati mnapambania Katiba Mpya , kuwe na mkakati mwingine wa masaa 24 day and night , siku 360 , all seasons.