Rais Samia kusema yeye na Hayati JPM walikuwa kitu kimoja sio tiketi ya JPM kufananishwa na malaika, alikuwa mwanadamu tu.

Phillipo Bukililo

JF-Expert Member
Dec 29, 2015
18,488
13,608
Ninamuelewa sana Rais Samia anaposema kuwa yeye na Hayati JPM walikuwa kitu kimoja. Kwamba ni maamuzi ya Hayati yaliyompa yeye nafasi ya kuwa mgombea mwenza.

Kwamba yeye na Hayati walihangaika majukwaani na wakapigwa na jua pamoja mwaka 2015 ili waingie ikulu, hivyo haupo uwezekano wa wao wawili kutenganishwa kiuongozi.

Baada ya kifo cha JPM wanaibuka watu na kumpaisha mpaka makamu wake anaonekana sio sehemu ya ufanisi wake wote wa kazi. Ni lazima Rais Samia akwazike kila anapoona anadharauliwa wakati ipo sehemu ya jasho lake katika hiyo heshima anayopewa kiongozi aliyetangulia mbele za haki.

Na Rais kusema kwamba yeye na Hayati ni kitu kimoja haina maana kwamba hata kama yalifanyika makosa basi yafumbiwe tu macho eti kwa kigezo cha kutoichafua kazi nzuri iliyofanyika.
Rais wa sasa afanye kazi kwa kutazama nini kinaweza kufanyika leo na kesho, afanye kazi kwa kutegemea nini haswa washauri wake wanasema.

Aitengeneze Tanzania akiwa na mitazamo kwamba zile dakika moja za watu kusimama kwa ajili ya kumkumbuka Hayati JPM zinapomalizika na watu kuwa wameshakaa vitini mwao, kila kinachofuatia kinasimamiwa na maamuzi yake mwenyewe, ambayo yatamhukumu yeye kama yeye mwaka 2025.

Yeye kuwa kitu kimoja na mtangulizi aliyelala usingizi wa milele hakumaanishi kuwa walichokifanya pamoja hakikuwa na udhaifu na wala hakistahili kurekebishwa pale inapobidi. Wakosoaji (critics) hawakwepeki, waliwakosoa mitume kina Mohamed na Yesu Kristo sembuse wanasiasa wanaoingia ikulu kwa kupigiwa kura!.

Ameongelea ATCL kutakiwa kuwa na wabunifu watakaokuja na mitazamo ya kibiashara zaidi, na utekelezaji wake uanze mara moja. Mashirika yote yenye kutakiwa kupeleka gawio hazina na yawe na aina ya watendaji wabunifu wenye kufanya kazi bila ya presha za kisiasa.

Kuna fursa nyingi tu ukanda ule wa mikoa ya Kigoma, Rukwa, Katavi, ukanda wote ule kwa kuambaa usawa wa ziwa Tanganyika ni fursa tupu za kiuchumi. Ni mikoa yenye utajiri mwingi lakini bado haijaanza kuchangamka. Uwekezaji unapolegezewa masharti yake, serikali ije na mpango mkakati wa kiuchumi wenye kuonyesha namna mikoa ile inavyoweza kuinuka.

Ajikite katika kuangalia namna ambayo bandari inayopanuliwa kule Mtwara itakavyoweza kulitumia vyema soko la Malawi na Zambia. Namna ambavyo bandari ya Tanga inaweza kuwa na mzigo wa uhakika, siku zijazo ambazo pengine corona itakuwa imepatiwa ufumbuzi.

Rais Samia afanye kazi pasipo kuwafikiria wale wote wanaomlinganisha na Hayati. Hawezi kufanana na Hayati na hana sababu ya kuwa mtumwa wa mitazamo au maoni ya wenye kumlinganisha nae. Awe na nafsi huru kila anapoingia ofisini asubuhi, anapofanya kazi mchana kutwa na jioni wakati anaondoka.

Binadamu hajawahi kuridhika tangu aanze kuishi juu ya ardhi na hatakuja kuridhika. Na hatakuja kuzaliwa mwanaume au mwanamke mwenye kipawa cha kumridhisha kila anayemzunguka.
 
Mwinyi alipoteuliwa kuwa Mwenyekiti wa CCM alisema yeye ni kama Kichuguu Tu mbele ya Mlima Kilimanjaro ...akimaanisha Nyerere..

That was smart move..

Siku zote kwenye leadership wanasema
'avoid great wearing great man's shoes'..

Ndo maana Samia anasisitiza hii ni awamu ya Sita...Hilo Tu maanake 'mambo yamebadilika'
 
Sijajua kwanini safari hii pamekuwa na kelele nyingi sana kati ya Rais aliepo na mtangulizi wake tofauti na miaka iliyopita.
 
Mwinyi alipoteuliwa kuwa Mwenyekiti wa CCM alisema yeye ni kama Kichuguu Tu mbele ya Mlima Kilimanjaro ...akimaanisha Nyerere..

That was smart move..

Siku zote kwenye leadership wanasema
'avoid great wearing great man's shoes'..

Ndo maana Samia anasisitiza hii ni awamu ya Sita...Hilo Tu maanake 'mambo yamebadilika'
Kosa tunalolifanya sisi watanzania (waafrika) ni kukariri maisha. Tunasahau kuwa kwa mtu mmoja kujaribu kumuiga mwingine ndio anavyopoteza ile identity yake mwenyewe.

Tunakosa ule msukumo wa kuamsha vipaji vya watu binafsi, na hapo tatizo ni aina ya elimu zetu kuwa za jumla jumla zisizokuza udadisi tangu utotoni.

Diamond Platinums miaka ya mwanzoni akiwa ndio anaanza kujulikana kukaibuka msanii mwingine anayesema kuwa anaigwa staili yake ya uimbaji. Lakini kadri siku zilivyopita na Diamond akaanza kuonyesha alivyokuwa mnyumbulifu (flexible) kimuziki ndivyo huyo msanii mwingine alivyopotea na kusahaulika.

Rais asimame katika ubunifu wa kwake mwenyewe na atafika mbali katika kuiongoza hii nchi.
 
Ninamuelewa sana Rais Samia anaposema kuwa yeye na Hayati JPM walikuwa kitu kimoja. Kwamba ni maamuzi ya Hayati yaliyompa yeye nafasi ya kuwa mgombea mwenza.

Kwamba yeye na Hayati walihangaika majukwaani na wakapigwa na jua pamoja mwaka 2015 ili waingie ikulu, hivyo haupo uwezekano wa wao wawili kutenganishwa kiuongozi.

Baada ya kifo cha JPM wanaibuka watu na kumpaisha mpaka makamu wake anaonekana sio sehemu ya ufanisi wake wote wa kazi. Ni lazima Rais Samia akwazike kila anapoona anadharauliwa wakati ipo sehemu ya jasho lake katika hiyo heshima anayopewa kiongozi aliyetangulia mbele za haki.

Na Rais kusema kwamba yeye na Hayati ni kitu kimoja haina maana kwamba hata kama yalifanyika makosa basi yafumbiwe tu macho eti kwa kigezo cha kutoichafua kazi nzuri iliyofanyika.
Rais wa sasa afanye kazi kwa kutazama nini kinaweza kufanyika leo na kesho, afanye kazi kwa kutegemea nini haswa washauri wake wanasema.

Aitengeneze Tanzania akiwa na mitazamo kwamba zile dakika moja za watu kusimama kwa ajili ya kumkumbuka Hayati JPM zinapomalizika na watu kuwa wameshakaa vitini mwao, kila kinachofuatia kinasimamiwa na maamuzi yake mwenyewe, ambayo yatamhukumu yeye kama yeye mwaka 2025.

Yeye kuwa kitu kimoja na mtangulizi aliyelala usingizi wa milele hakumaanishi kuwa walichokifanya pamoja hakikuwa na udhaifu na wala hakistahili kurekebishwa pale inapobidi. Wakosoaji (critics) hawakwepeki, waliwakosoa mitume kina Mohamed na Yesu Kristo sembuse wanasiasa wanaoingia ikulu kwa kupigiwa kura!.

Ameongelea ATCL kutakiwa kuwa na wabunifu watakaokuja na mitazamo ya kibiashara zaidi, na utekelezaji wake uanze mara moja. Mashirika yote yenye kutakiwa kupeleka gawio hazina na yawe na aina ya watendaji wabunifu wenye kufanya kazi bila ya presha za kisiasa.

Kuna fursa nyingi tu ukanda ule wa mikoa ya Kigoma, Rukwa, Katavi, ukanda wote ule kwa kuambaa usawa wa ziwa Tanganyika ni fursa tupu za kiuchumi. Ni mikoa yenye utajiri mwingi lakini bado haijaanza kuchangamka. Uwekezaji unapolegezewa masharti yake, serikali ije na mpango mkakati wa kiuchumi wenye kuonyesha namna mikoa ile inavyoweza kuinuka.

Ajikite katika kuangalia namna ambayo bandari inayopanuliwa kule Mtwara itakavyoweza kulitumia vyema soko la Malawi na Zambia. Namna ambavyo bandari ya Tanga inaweza kuwa na mzigo wa uhakika, siku zijazo ambazo pengine corona itakuwa imepatiwa ufumbuzi.

Rais Samia afanye kazi pasipo kuwafikiria wale wote wanaomlinganisha na Hayati. Hawezi kufanana na Hayati na hana sababu ya kuwa mtumwa wa mitazamo au maoni ya wenye kumlinganisha nae. Awe na nafsi huru kila anapoingia ofisini asubuhi, anapofanya kazi mchana kutwa na jioni wakati anaondoka.

Binadamu hajawahi kuridhika tangu aanze kuishi juu ya ardhi na hatakuja kuridhika. Na hatakuja kuzaliwa mwanaume au mwanamke mwenye kipawa cha kumridhisha kila anayemzunguka.


Mahali pa kuanzia observation ya hao wanaosimama dakika moja kumuenzi JPM ni pale Mama alipohutubia Bunge na walipofanya uchaguzi wa CCM Dodoma mwisho utaona viashiria vingi tu vya usanii achilia mbali hiyo dakika moja wala huwa haifiki na kama kuna mtu anayo clip inayooweka ushahidi wa dakika moja kamili atuwekee hapa maana mie kila nikihesabu nakuta ni chini ya hapo kila wanapofanya jambo hilo au saa yangu ni mbovu? Rais Samia anapohutubia mazuri ya JPM makofi ya kiunafiki ni mengi sana lakini anapokuja kugusa responsibility yao kwa umma watu haohao huwa kama baridi kama kiporo kilichotoka kwenye jokofu
 
Mahali pa kuanzia observation ya hao wanaosimama dakika moja kumuenzi JPM ni pale Mama alipohutubia Bunge na walipofanya uchaguzi wa CCM Dodoma mwisho utaona viashiria vingi tu vya usanii achilia mbali hiyo dakika moja wala huwa haifiki na kama kuna mtu anayo clip inayooweka ushahidi wa dakika moja kamili atuwekee hapa maana mie kila nikihesabu nakuta ni chini ya hapo kila wanapofanya jambo hilo au saa yangu ni mbovu? Rais Samia anapohutubia mazuri ya JPM makofi ya kiunafiki ni mengi sana lakini anapokuja kugusa responsibility yao kwa umma watu haohao huwa kama baridi kama kiporo kilichotoka kwenye jokofu
Msiba unapomalizika watu huvua mavazi meusi ya uombolezaji na kila kitu huendelea kama kawaida. Kubakia kule kule ndani ya mawazo ya maombolezo ni kielelezo cha udhaifu wa nafsi moja moja na jamii nzima.
 
Mtu anyejihami kuvaa viatu vya mtu mwingine, sijui mimi na mtangulizi wangu ni kitu kimoja inaonyesha huna vision na unaficha udhaifu wako wa kiuongozi kwenye kivuli cha mtu mwingine ambaye tayari ni marehemu, kifupi hujajiandaa kuwa kiongozi...
 
Mtu anyejihami kuvaa viatu vya mtu mwingine, sijui mimi na mtangulizi wangu ni kitu kimoja inaonyesha huna vision na unaficha udhaifu wako wa kiuongozi kwenye kivuli cha mtu mwingine ambaye tayari ni marehemu, kifupi hujajiandaa kuwa kiongozi...
Vision anayo tatizo ni presha za kisiasa za wanaomzunguka.

Zilianzia bungeni Ndio maana akawakemea kwa kutumia neno kudemka.

Aliyempa ugombea mwenza 2015 alimuamini na alimjua kiutendaji yupo vipi.
 
Back
Top Bottom