Lord denning
JF-Expert Member
- Jun 3, 2015
- 13,226
- 26,047
Ya Mungu mengi. Naweza kuja kuwa Rais wako!Ungepewa uraisi ww bas ambae sio mpuuz
Ya Mungu mengi. Naweza kuja kuwa Rais wako!Ungepewa uraisi ww bas ambae sio mpuuz
Yeye kachambua kaona hakuna anayemfaa bora awarudishe walewale wa kale.wengine nyie mnastahili kuongozwa sio kuongoza acha kulalamika ushaambiwa Ccm ina wenyewe je? Wewe upo?Ndugu wakati wa jakaya ulijenga vibanda vigapi?ulikula Bata zaina aina gani au ni zile za wakina baba msofe? Nchi ilifungwa na nani? Sikatai kuweka watu naungana n uwekwaji watu ILa atubadilishie sura tunazo sura za kipigaji tunazijua za in Sasa nchi Ina watu zaidi ya milioni 60 sio lazima ziwe zilee zile.anaporudisha sura zile zile ni kumdhiaki mwendazake wakati yeye alikuwa ni Makamu wake tafusiri yake ni ipi?Kila siku tunawaona watendaji hao walimpiga porojo tu umeme hakuna,
Ww enzi hizo za jakaya ulikula Bata tu nduguYeye kachambua kaona hakuna anayemfaa bora awarudishe walewale wa kale.wengine nyie mnastahili kuongozwa sio kuongoza acha kulalamika ushaambiwa Ccm ina wenyewe je? Wewe upo?
Mimi nina kibanda cha urithi nataka awamu hii nipate kibanda cha kwangu maana fursa zimefunguliwa Mama anaupiga mwingi
Usihamaki boss, katiba inamruhusu kumteua atakaye.Mh Rais mtu ameisha kuwa Waziri Kiongozi wa Zanzibar na anakula pensheni mpaka afe, leo unamteua kuja kuwa mbunge wa kawaida au hata ukimpa Uwaziri kesho kweli inakuja?Zanzibari ni yeye tu hakunaga wengine? Yani mtu ashakuwa Waziri Mkuu Zenji, leo anakuja kuwa mbunge wa kuteuliwa najiuliza hiyo nafasi mlimpaga ili iweje huko? alivyokula akiwa hapo hakutosheka?
rojoooo la makunduchiHii nchi yetu watu wanahitaji tiba ya kisaikolojia Maana hatujuwi wanataka waongozwe na akina nani?.Ili waache kulalamika Mama kashasema anataka afanye kazi na watu ambao anaona naweza fanya nao kazi vizuri hata ungekuwa wewe ungefanya ivoivo.Hao wa mwendazake hawauziki kwa sasa maana
1) waliifunga nchi na sasa nchi inafunguliwa au wewe hupendi nchi ifunguliwe
2)Askofu wangu Ruachi wakati akiadhimisha musa ya marehemu JPM alisema nchi sasa inapumua maana waliokuwepo waliziba pua za nchi na watu wakakosa hewa Je? Wewe hupendi hewa safi ya nchi unataka tukumbatie waziba hewa ya nchi?
3)miaka mitano iliyopita kanisa au taasisi za dini ziliteseka sana na chumi zao zikaporomoka,sasa unataka tuendelee na wale wenye itikadi za kukandamiza taasisi za dini?.unataka kutupa machungu ya nyuma Ili watu washindwe kumtumikia Mungu?
4)Humu jamii forum kila siku mnalalamika kuwa JPM alikuwa muuwaji na mtu katili sana. Mama anaweka watu waungwana kama yeye aponye majereha ya wananchiJe? Ulitaka aendelee kuweka kizazi cha watu katili na wauwaji?
5)miaka mitano iliyopita hela mtaani zilipotea tukaishi kwa mateso,sasa mama anaweka watu ambao watatusaidia tupate hela kwa urahisi watu wale pata
Mimi binafsi mama naona anaupiga mwingi sanaa na soon maisha yatakuwa poa kama awamu ya nne,watu tule bata tuwe kujenga vibanda hata vya kuishi.malalamiko ya nini? .Mungu alishatujibu maombi yetu ya awali mwache mama apange safu yake nzuri watu tupumue
Ni wakati muafaka kwa Serikali kuandae kanzi data ya vijana wenye Elimu ya vyuo vikuu wenye ufaulu wa upper second na first class
-waandaliwe Kwenye masuala ya menejimenti na uongozi katika fani mbalimbali.
-Mwalimu Nyerere,wakati tunàpata Uhuru, Tanzania haikuwa na wasomi wengi,kwa hiyo alikuwa na changamoto ya kufanya uteuzi wa wasaidizi wake.
-Miaka 60 ya Uhuru, Tanzania ina vijana wengi , kwenye fani mbalimbali,
- wanahitaji kuandaliwa( kidogo ) kwenye masuala ya menejimenti na uongozi(Management trainee) kwenye nyanja mbalimbali.
-Mamlaka ya uteuzi,haina changamoto ya kupata watu sahihi wa kuongoza taasisi na idara mbalimbali za Serikali.
-Utaratibu wa kuwarejesha watendaji au viongozi walioachishwa au waliostaafu ni ishara kuwa hatuna mipango endelevu( succession plan).
-Serikali ianzishe kanzi Data ya vijana wenye vipaji ili kurahisisha mchakato wa uteuzi wa viongozi (wakuu wa mikoa, wilaya,wakarugenzi wa Halmashauri za wilaya na Manispaa,afisa Tawala, wakuu wa idara na vitengo mbalimbali Serikali).
-Mamlaka zinazohusika ziwe zimewafutilia mienendo yao, kuepuka kuteua watu ambao jamii,inawajua ndani na nje, kuwa siyo wasafi.