Rais Samia, kuna dalili zote za kuwa na mafuta ziwa Tanganyika na Nyasa

Sasa wewe, unafikiri hadi wakaamua kukomesha matumizi ya mafuta yote hayo hawajafikiria? Wewe unaingilia field za watu na kutoa point ambazo hazina mshiko. Hiyo neclear power utatumia kwenye magari? Na unajua athari na gharama zinazotokana na nuclear power? Kwa taarifa yako nchi zilianza kuondokana na nuclear power kabla hata hawajaanza kufikiria kuondokana na mafuta.
Ulisoma vizuri nilichoandika au ulidandia tu? Rudia tena kusoma kwa utulivu.

Mafuta yataendelea kuchimbwa kwa miaka mingi tu ijayo na yatatumika.
 
Hi mbona watu wagumu sana kuelewa mambo madogo kama haya? Mbona nimejibu hoja yako hapo juu?

Ni hivi, matumizi ya mafuta kwenye magari ni karibu 70% ya mafuta yanayozalishwa. Sasa ukipunguza hiyo 70% kwenda labda 30%, bei ya mafuta itashuka sana, kwa kuwa unakuwa umepunguza demand ya mafuta. Exploration na production ya mafuta kwa ajili ya matumizi yaliyobaki inakuwa sio economically feasible kwa uzalishaji mdogo mdogo. Watakaoweza kuendelea kuzalisha mafuta ni makampuni makubwa ambayo wao economies of scale zinafanya production cost zao kuwa chini. Hivyo wazalishaji wadogo kama Tanzania, Uganda nk itabidi wafunge production zao kwa kuwa itakuwa hasara wao kuendelea kuzalisha mafuta.

Sasa kama shule yako ni ndogo hapo nitakuwa nimekuchanganya sana!
Wewe shule yako kubwa 300 acres.

Kwenye hii link inasema 26% ya mafuta duniani inatumika kwenye usafiri. How electric vehicles could take a bite out of the oil market kwaio 74% iko kwenye sekta nyenginezo. Kwa hapa Afrika magari ya mafuta yataendelea kuwepo kwa mda mrefu sana tu. Isitoshe, bei ya mafuta watu wanaamua tu mwezi huu tuzalishe machache, bei inapanda watu wanajilipa, ndio michezo inayochezwa kila kukicha na wazalishaji mafuta au hujui hilo? Unafikiri mafuta bei yanapanda kwa sababu imekuwa shida uchimbaji au watu wameamua tupunguze uzalishaji na tutengeze demand? shuleni umelishwa kwa kijiko.
 
Wewe shule yako kubwa 300 acres.

Kwenye hii link inasema 26% ya mafuta duniani inatumika kwenye usafiri. How electric vehicles could take a bite out of the oil market kwaio 74% iko kwenye sekta nyenginezo. Kwa hapa Afrika magari ya mafuta yataendelea kuwepo kwa mda mrefu sana tu. Isitoshe, bei ya mafuta watu wanaamua tu mwezi huu tuzalishe machache, bei inapanda watu wanajilipa, ndio michezo inayochezwa kila kukicha na wazalishaji mafuta au hujui hilo? Unafikiri mafuta bei yanapanda kwa sababu imekuwa shida uchimbaji au watu wameamua tupunguze uzalishaji na tutengeze demand? shuleni umelishwa kwa kijiko.
Kwa hii point wala sikubishii. Nimerudi kwenye reference yangu nikakuta inasema non-vehicle consumption ndio 74", kwa hiyo nakiri kufanya makosa hapo. Na you are right, global consumption ya transport ni 26%, hata kulingana na BP Outlook (angalia diagram chini hapa). Hata hivyo, note kwamba hiyo distribution ya matumizi ya mafuta haiko hivyo katika nchi zinazoendelea. Si ajabu nchi kama Tanzania matumizi ya mafuta kwenye transport sector ni zaidi ya 80%, industry 15%, buildings 5%.

Lakini sasa, angalia kwamba objective hapa ni kuondoa matumizi ya fossil fuel kama suluhisho la climate change. Wakati kuna nchi zinasema zitaondoa gari za mafuta, kuna nchi zinasema zitasimamisha uzalishaji wa mafuta, kwa kuwa objective ni kupunguza GHG emissions kutokana na matumizi ya mafuta. Hivyo basi, tutatarajia impact hata kwenye non-transport sectors ambazo zinatumia oil products, kama industry na buildings. Kwenye industry kwa mfano, matumizi ya mafuta kutengeneza plastics yatapungua kwa kuwa kuna kampeni za kuzuia matumizi ya plastics. Hata hapa Tanzania plastic bags sasa marufuku. Europe inaelekea ku-ban single use plastics. Synthetic lubricants pamoja na oil za magari sasa hivi ndio mtoto mpya na bora kuliko zinazotokana na mafuta. So all in all, demand ya oil itapungua, na hoja kwamba tuharakishe ku-develop mafuta yetu inabaki palepale.

Hongera kwa kubisha kisomi kwa hili.

1621672092531.png
 
Ulisoma vizuri nilichoandika au ulidandia tu? Rudia tena kusoma kwa utulivu.

Mafuta yataendelea kuchimbwa kwa miaka mingi tu ijayo na yatatumika.
Na wewe umesoma vizuri? Sijasema popote mafuta hayatachimbwa tena, nimesema matumizi yake yatapungua na hivyo kusababisha bei ya mafuta duniani kushuka sana, na haitakuwa economically feasible kwa nchi kama Tanzania kuchimba mafuta kutoka visima vyetu ikiwa reservoir ni ndogo na cost ya production na kuyasafirisha say toka Ziwa Nyasa hadi Dar es Salaam for export ni kubwa. Sana sana offshore productions ndio zita survive.

Nikasema watabaki oil producers wachache wenye production kubwa sana na hivyo kuhimili cost of production against world oil market price kwa sababu ya economies of scale au competitive advantages watakazokuwa nao. Ndio maana nikasema kama tunataka kufaidika basi tuharakishe kuendeleza mafuta yetu sasa, ndani ya miaka 10, kabla impact ya kushuka bei ya mafuta haijaikumba dunia kutokana na measures zilizopo za kuondokana na matumizi ya fossil fuels katiaka sector mbalimbali transport sector ikiongoza. Soma uelewe kabla ya kujibu
 
Na wewe umesoma vizuri? Sijasema popote mafuta hayatachimbwa tena, nimesema matumizi yake yatapungua na hivyo kusababisha bei ya mafuta duniani kushuka sana, na haitakuwa economically feasible kwa nchi kama Tanzania kuchimba mafuta kutoka visima vyetu ikiwa reservoir ni ndogo na cost ya production na kuyasafirisha say toka Ziwa Nyasa hadi Dar es Salaam for export ni kubwa. Sana sana offshore productions ndio zita survive.

Nikasema watabaki oil producers wachache wenye production kubwa sana na hivyo kuhimili cost of production against world oil market price kwa sababu ya economies of scale au competitive advantages watakazokuwa nao. Ndio maana nikasema kama tunataka kufaidika basi tuharakishe kuendeleza mafuta yetu sasa, ndani ya miaka 10, kabla impact ya kushuka bei ya mafuta haijaikumba dunia kutokana na measures zilizopo za kuondokana na matumizi ya fossil fuels katiaka sector mbalimbali transport sector ikiongoza. Soma uelewe kabla ya kujibu
Mnapokua mnaleta hoja mpitia kqanza vyanzo mbalimbali vta taarifa.
Hii hapa ni habari ya Egypt.
Screenshot_20210522-070155.png
 
Moderators wa JF mnazingua sana. Mmebadilisha kichwa cha thread na kutoka nje kabisa ya topic. Lengo haikuwa kusema kuna dalili za mafuta, bali kuweka mkazo kwamba lazima tuharakishe ku-utilize hii resource kwa kuwa kuna kasi ya kuacha kutumia mafuta duniani. Kwa nini mnafix vitu ambavyo havina tatizo, na kuishia kuharibu? Ndio maana kuna wakati niliacha kabisa kuandika thread kwa ajili ya mambo yenu kama haya


Raisi Samia, kuna dalili zote za kuwa na mafuta ziwa Tanganyika na Nyasa. Tusipoyachimba ndani ya miaka kumi ijayo hayatakuwa na faida tena kwetu

Raisi Samia, nadhani una taarifa kwamba kuna kila dalili za mafuta ndani ya Ziwa Tanganyika na Ziwa Nyasa. Hakuna maendeleo yaliyofanyika kuchimba mafuta katika maeneo haya kutokana na vikwazo viwili;
  1. Upande wa ziwa Tanganyika kuna kikwazo cha waasi wa DRC. Si rahisi kuendeleza mradi wa mafuta ziwani Tanganyika ikiwa waasi hawa wa DRC hawajaondolewa kabisa. Na mafuta haya yataendelezwa kwa ushirikiano kati ya Tanzania na DRC, ndio maana Tanzania ilikuwa tayari kupeleka jeshi DRC kusaidia kuondosha waasi ili tuchimbe haya mafuta kwa ushirikiano na DRC. Inaonekana zoezi la kuondoa waasi limekwama, na hiki kimekuwa kikwazo.
  2. Upande wa ziwa Nyasa kuna mafuta. Lakini pindi ilipoonekana Ziwa Nyasa lina mafuta tuliingia katika mgogoro wa mpaka kati yetu na Malawi. Wakijua rasilimali ya mafuta iloiyomo ziwani, Malawi walianza kudai ziwa Nyasa lote liko upande wa Malawi na ndio maana wao wanalitambua kama Ziwa Malawi. Nilipendekeza humu JF kwamba tuachane na suala la mgororo wa mpaka na jirani zetu Malawi tukubaliane nao kwamba rasilimali yoyote ya mafuta ndani ya ziwa tutagawana 50/50 bila kujali iko upande gani. Sijui kama nilisikilizwa.
Sasa kuna tatizo. Kutokana na tatizo la mabadiliko ya mazingira (climate change), mataifa makubwa duniani yameweka mkakati wa kuacha kutumia mafuta kwa ajili ya magari na mitambo. Norway kwa mfano, wanasema kufikia 2050 wataacha kabisa shughuli za kuchimba mafuta. Uingereza wanasema watapiga marufuku magari ya kutumia diesel kufikia 2025 nadhani. Japan, Germany na hata China, wote wanasema ndani ya miaka 15 ijayo wanataka kutoka kwenye kutumia mafuta kwenye magari na kuingia kwenye magari ya umeme (from internal combustion engines to electric vehicles)

Sasa hii inamaanisha nini kwa nchi kama Tanzania ambazo hadi sasa zimekalia tu uchumi wa mafuta bila kuuendeleza? Ina maana ndani ya miaka 20 ijayo, mafuta yatakuwa si mali kitu. Hata ukigundua una mafuta mengi kama bahari ya Hindi, hayatakusaidia tena kwa kuwa dunia imeanza kuondoka toka tekinolojia ya mafuta kwenda teknolojia ya umeme!

Hivyo basi, kama kweli tunataka kufaidika na rasilimali ya mafuta tuliyonayo, ni lazima iendelezwe ndani ya kipindi cha miaka kumi ijayo. La sivyo haya mafuta yatakuwa na rasilimali isiyohitajika tena duniani, na ndani ya kipindi cha miaka kumi ijayo tutaanza kushuhudia kuporomoka kwa bei ya mafuta kadiri magari ya umeme yanavyoingia sokoni. Leo hii hata Lamborghini wamesema wataacha kutengeneza gari za mafuta!

Kwa hiyo kaza mwendo tuweke mkakati wa kuchimba mafuta Lake Tanganyika na Nyasa. Tatua changamoto zinazokabili maeneo haya. Waambie TPDC waache ku-weka areas with the highest oil potential for last. Ikiwezekana, wafanye mkupuo mmoja wa kugawa vitalu vya kufanya oil and gas exploration kwa nchi nzima, time is of essence, waache mwendo wa bata.

Tukiweza kuchimba mafuta ndani ya miaka kumi ijayo, yatachangia sana kuinua uchumi wetu, tutakuwa na barabara za rami hadi vijijini! Tukichelewa, haya mafuta hayatatusaidia, yatakuwa obsolete resource!

Angalia pia:

Suluhisho la mgogoro na Malawi ni hili; sio suala la ziwa wala mpaka

Suala la uwepo wa mafuta katika ziwa Nyasa na kusababisha mgogoro wa mpaka kati ya Tanzania na Malawi limeishia wapi?

Katika awamu hii chini ya Rais mpya Malawi, Magufuli atumie fursa hii kutatua mgogoro wa mpaka kati ya Malawi na Tanzania
Hili ni suala jingine natamani sana Mama Samia angelisikiliza. Na labda Prof. Mwandosyaanaweza kusaidia
 
Back
Top Bottom