sheiza
JF-Expert Member
- Sep 29, 2010
- 7,564
- 11,478
Katika hali isiyo ya kawaida, jana imeshuhudiwa mheshimiwa rais akiwa mgeni rasmi kwenye birthday ya ndugu mr 2 au sugu au 2proud au Jongwe.
Hii imeibua maswali lukuki hasa ikichukuliwa na muda ambao hiyo shughuli ilikuwa inafanyika na ni tukio la kwanza la aina yake.
Lakini kiundani zaidi inaonekana ni kama mpango wa kumzima dr Tulia asionyeshe cheche zake za uspika awapo bungeni.
Ikumbukwe mara ya mwisho bunge kupitia spika lilitoa amri kwa serikali kuja na hatua za msingi ambazo inachukua kuhusiana na sakata la kupanda mafuta na ikatoa deadline hali iliyopelekea mh rais kuitisha kikao usiku wa manane ili waziri wa nishati akatoe tamko kwa niaba ya serikali kama alivyoamriwa.
Pia ikumbukwe siku aliyoapishwa dr Tulia kama spika hakusita kumtaja hayati Magu kama mtu aliyechangia yeye kufika hapo jambo lililoonekana halikumpendeza sana mama.
Sasa je harakati hizi za kuhudhuria hadi sherehe za usiku za sugu ni harakati za kumzima dr Tulia na kutaka kumuonyesha kuwa wana uwezo wa kummaliza jimboni na pengine awe spika wa kipindi kimoja?
Muda utasema.
Hii imeibua maswali lukuki hasa ikichukuliwa na muda ambao hiyo shughuli ilikuwa inafanyika na ni tukio la kwanza la aina yake.
Lakini kiundani zaidi inaonekana ni kama mpango wa kumzima dr Tulia asionyeshe cheche zake za uspika awapo bungeni.
Ikumbukwe mara ya mwisho bunge kupitia spika lilitoa amri kwa serikali kuja na hatua za msingi ambazo inachukua kuhusiana na sakata la kupanda mafuta na ikatoa deadline hali iliyopelekea mh rais kuitisha kikao usiku wa manane ili waziri wa nishati akatoe tamko kwa niaba ya serikali kama alivyoamriwa.
Pia ikumbukwe siku aliyoapishwa dr Tulia kama spika hakusita kumtaja hayati Magu kama mtu aliyechangia yeye kufika hapo jambo lililoonekana halikumpendeza sana mama.
Sasa je harakati hizi za kuhudhuria hadi sherehe za usiku za sugu ni harakati za kumzima dr Tulia na kutaka kumuonyesha kuwa wana uwezo wa kummaliza jimboni na pengine awe spika wa kipindi kimoja?
Muda utasema.