Erythrocyte
JF-Expert Member
- Nov 6, 2012
- 117,343
- 217,371
Siku ya mwisho kila goti litapigwa , mmekwishaanza kujianika , Mamluki wakubwa nyie .Iwe ni kuwa na bunge lenye meno na ambalo litakuwa wajibu wa kuiwajibisha serikali lazima watanzania tukomae tupate katiba mpya.
Iwe ni kudhibiti wanasiasa waovu ambao walishageuza nchi yetu kama shamba la bibi kuvuna na kuiba mali za umma. Tunahitaji katiba mpya.
Kulinda na kutetea haki za kila mtanzania dhidi ya maovu ya udhalimu wa wakora wa kisiasa na wanaoua, kutesa na kuletea maumivu watanzania. Tunahitaji katiba mpya.
Katiba mpya itafutwe kwa kila namna, iwe kwa maandamano, makongamano, elimu na kuhamasisha watanzania wote bila kujali itikadi zao.
Katiba mpya ndio suluhu la matatizo ya taifa letu. Tupate katiba ambayo itaruhusu raisi, spika, waziri , Igp na kiongozi yoyote kushitakiwa kama akifanya kosa.
Wewe tulikuonya mapema sana lakini ulitoa mapovu yenye matusi , kiko wapi sasa ?