Rais Samia, kama uchumi umeyumba tangaza kupunguza mshahara wako pamoja na viongozi wako waandamizi na wabunge

Kiboko ya Jiwe

JF-Expert Member
Apr 7, 2020
12,693
36,080
Habari!

Kwakweli kama mtumishi ambaye sijapanda daraja tangu niajiriwe, siujui mshahara mpya nakaribia mwaka wa sita sasa hapa matumaini yanayeyuka. Naanza kufikiri nje ya duara.

Hata hayo madaraja mapya sijui kama nami nitakuwa mmoja wapo. Maana idadi ya wanaostahili kupanda madaraja ni wengi kuliko idadi tuliyotajiwa.

Pia kuna mambo mawili:
1. Kuahidiwa/kutajiwa jambo
2. Kutendewa.

Hapa kuna watu watanawa lakini hawatakula.

Ok, twende kwenye hoja.

Kama uchumi umeyumba tangaza kupunguza mshahara wako pamoja na mshahara wa viongozi waandamizi bila kuwasahau wabunge.
Hii itasaidia kumpunguzia mlipa kodi mwananchi mzigo mkubwa.

Uchumi utakapokaa sawa mtaendelea na utaratibu wenu wa kulipana mamilioni huku mkiendelea kulipana allowances kedekede.

Sisi watumishi na wananchi wanyonge hatuna shaka na nyie viongozi, tunajua umuhimu wenu katika taifa hili.
 
Naunga mkono hoja Mana wanao ongoza kwa kutumia kodi ya Watanzania bila kufanya kazi ni wabunge, mawaziri, wakuu wa mikoa, wa wilaya, wakurugenzi na wengine kimsingi mishahara yao ilibidi ipunguzwe kuonyesha uzalendo.
 
Njia nyingine ya kuokoa fedha ni kupunguza wabunge kutoka Zanzibar

Wabunge kutoka Zanzibar hufika mpaka 71

wabunge 71 x shilingi 11,000,000 'mapato ya mbunge mmoja kwa mwezi' = shilingi 781,000,000

781,000,000 ukigawanya kwa 50,000 unapata 15,620

Kwa hiyo walimu/watumishi 15,620 wanaweza kupata nyongeza ya shilingi 50,000 kila mwezi endapo wabunge kutoka Zanzibar watapunguzwa
 
Njia nyingine ya kuokoa fedha ni kupunguza wabunge kutoka Zanzibar

Wabunge kutoka Zanzibar hufika mpaka 71

wabunge 71 x shilingi 11,000,000 'mapato ya mbunge mmoja kwa mwezi' = shilingi 781,000,000

781,000,000 ukigawanya kwa 50,000 unapata 15,620

Kwa hiyo walimu/watumishi 15,620 wanaweza kupata nyongeza ya shilingi 50,000 kila mwezi endapo wabunge kutoka Zanzibar watapunguzwa
Hapo patamu.

Tena hiyo 11 milioni hujawawekea sitting allowance
 
Back
Top Bottom