Pulchra Animo
JF-Expert Member
- Jun 16, 2016
- 3,398
- 2,990
Sijui hii hoja itabadili nini katika mhjadala. Ikiwa kuna senator 100 na VP kama tie breaker kinabadili vipi mantiki ya nilichozungumzia? trivial
Kwani muundo wa sasa upoje? Si tuna Zanzibar na Tanzania! hii Tanzania inahudumia nini na inapata wapi kodi
Tofauti itakayokuwepo ni uwajibikaji wa Zanzibar , kwamba, hawatakuwa katika mbeleko na hilo litapunguza mzigo kwa Watanganyika. Otherwise gharama za ''fed' ya sasa anazibeba Mtanganyika! kwanini huoni hili?
Tulifanya ulinganifu wa Feds ya Warioba na ya US ambayo wewe unadhani tunaweza kufanya copy and paste
Ndipo nimejaribu kukuonyesha kuwa House of rep ya Fed na ile ya Warioba ni tofauti kutokana na population na usidhani kuwa gharama zitakuwa kubwa kwa jicho la US m India au kwingine
Kwani kufanya taxing kwa Feds itaongeza gharama?
Hivi unahabari kwamba US states zinachangia Feds! halafu kuna Fed tax ! unajua hili?
Kwa wingi wa states ukilinganisha na Tanzania unafanya comparison gani ndugu yangu?
FYI leo Rais wa Zanzibar kamteua Jai mkuu wa Zanzibar! Sijui huyu wa Tanzania ana kazi gani
Unaweza kuona kwanini Waioba alishauri mambo 7 tu na 3 ndiyo yenye gharama kubwa
Unapotosha sana. Governing system ya Marekani imegatua madaraka extensively. Unawezaje kulinganisha representation ya watu 330+ million wenye 535 federal legislators na 7,410 state legislators (for a total of 7,945 federal and state legislators) na representation ya watu 60+ million wenye 75 federal legislators na less than 400 state legislators (for a total of less than 475 federal and state legislators)? Hii ni hesabu rahisi ya uwiano, tuliyosoma shule ya msingi! Ili comparison yako iwe meaningful, representation ya wale watu 60+ lazima ibadilike sana, either at the federal level or at the state level. Na kufanya hivyo, maana yake kuongezeka kwa gharama za uendeshaji wa nchi ya Tanzania as a whole.
Una maana gani unaposema U.S. states zinachangia Feds? Marekani, federal taxes have nothing to do with state taxes. Zipo states ambazo hazina hata state income tax, lakini raia wake bado wanalipa income taxes to the federal government kama tu wafanyavyo raia wa states zingine. Mfano wa hizo states ni Texas na Florida.
Uwepo wa multiple layers of taxation (federal, state, local) maana yake ongezeko la gharama. Hata usipoipa federal government mamlaka ya kutoza kodi (taxing authority), kwa kufuata ile flawed setup inayopendekezwa na Draft ya Katiba ya Tume ya Warioba, lazima kuwe na compensating effect kwenye state (na pengine local) taxes.
Zanzibar ina mahakama zake yenyewe (isipokuwa haina court of final appeal) na ina Chief Judge wake. Huyo Chief Judge ana hadhi sawa na Principal Judge wa Mahakama Kuu yetu ya huku mainland. Chief Justice wa JMT ndiye boss wao wote wawili, na Court of Appeal ya JMT ina jurisdiction katika pande zote za JMT, tofauti na ilivyo kwa mahakama kuu zilizomo kwenye hizo pande mbili.